Habari za Punde

CMC Automobiles Sao Hill Forest Rally of Iringa Kufanyika 13/5/2023 hadi 14/5/2023

Kaimu muhifadhi mkuu wa shamba la miti Saohill PCO Tebby Yoramu akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mashindano ya mbio za magari zitakazofanyika Misitu ya asili Saohill.Mmoja ya magari ambayo yatashiriki Mashindano ya mbio za magari yatayofanyika Iringa yenye jina la CMC Automobile Saohill Forest Rally of Iringa yanatarajiwa kuanza tarehe 13na 15 mwezi wa tano katika Misitu ya asili Saohill .Mmoja ya magari ambayo yatashiriki Mashindano ya mbio za magari yatayofanyika Iringa yenye jina la CMC Automobile Saohill Forest Rally of Iringa yanatarajiwa kuanza tarehe 13na 15 mwezi wa tano katika Misitu ya asili Saohill .

Na Fredy Mgunda,Iringa.                                                                                                                      

Mashindano ya mbio za magari yanayofahamika kwa jina la CMC Automobile Saohill Forest Rally of Iringa yanatarajiwa kuanza tarehe 13 mwezi wa tano katika Misitu ya asili Saohill .

Kwa mujibu wa Robert Maneno muandaaji mkuu wa mashindano hayo amesema kuwa wamedhamiria kufanya mashindano ya mbio za magari tarehe 14  mwezi wa Tano yanayohusisha washiriki kutoka Tanzania na nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na washiriki kutoka Tanzania ,Kenya ,Uganda na Zambia .

" Tarehe 13 kutakuwa na maonyesho pale uwanja wa Samora alafu tarehe 14 itakuwa ni kilele hapa katika shamba la Saohill na mashindano yamekamilika tunashukuru pia kwa muhifadhi kwa kufanya maandalizi mpaka saa hizi Kuna gari 12 na washiriki kadhaa mwingine kutoka Tanzania wengine kutoka nchi za jirani Kama Zambia,Kenya na mwingine kutoka Uganda na wameanza safari Yao kuja hapa Iringa na Kuna gari ambao nafikiri tunategemea italeta vionjo japo zote zitaleta vionjo Ila gari itakayokuwa Kali ni Fordfiesta R5 ambao itatumiwa na mtu kutoka Uganda " .

Alisema kuwa katika maandalizi ya mashindano hayo wanatarajia tarehe 13 kufanya maonyesho ya magari katika viwanja vya Samora huku kukiwa na magari yenye viwango vikubwa kulinganisha na mashindano yaliyopita .

Amjad Khan ni mwenyekiti wa mashindano ya mbio za magari zitakazofanyika Misitu ya Saohill alisema kuwa pamoja na mashindano hyao kufanyika wanatarajia kupokea ugeni mkubwa huku aliwataka washiriki kutumia vizuri sheria watakazopatiwa n mamlaka ya Misitu .

"Mpaka Sasa tumefikia asilimia 90 safari hii tunategemea kupata ugeni mkubwa Sana wanakujaniwa sababu sio mashindano tuu Bali wankauja kuangalia pia mashindano katika shamba kwa hiyo hiyo siku itatujengea jina kubwa tunashukuru kwa watu wa Saohill kwa kutupokea mashabiki wa gari karibuni Sana haya ni tofauti na Yale tuliyokuwa tukifanya zamani kikubwa tuzingatie sheria tutakazopewa ikiwemo sigara hapa marufuku mazingira tuache yakiwa safi ".

Naye PCO Tebby Yoramu Kaimu muhifadhi mkuu wa shamba la miti Saohill alisema kuwa mashindano hayo yatakuwa fursa ya kuonyesha utalii uliopo ndani ya shamba la miti Saohill ikiwa ni pamoja na utalii wa nyuki , uvuvi na maporomoko yaliyopo ndani ya Hifadhi ya shamba Hilo .

Alisema pamoja na kuwepo kwa mashindano hayo bado ni fursa kwa waandaji wa mashindano baiskeli ,mashindano ya riadha kwani Kuna kilomita nyingi zinazotoa fursa za ufanyikaji wa mashindano hayo .

"Tunashukuru na kufirahi kwa kuona Saohill inafaa kwa mashindano ya mbio za.magari hii ni fursa za vivutio kwa ajili ya utalii wa tiolojia kwa sababu ukitaka kuangalia hapa tunavyanzo vya utalii vingi ikiwamo tunamizinga ya nyuki ,Manzuki , na hapa Kuna uoto wa miti ya kupandwa ,wanyama pia mimea ,pia itakuwa chanzo Cha utalii kwa sababu Kuna maporomoko ya maji ,bwawa la ngwazi,uvuvi wa kurejesha pia utalii wa makasia na mashindano haya huenda yakafungua pia fursa ya mashindano mengine Kama mashindano ya baiskeli, marathon".

Shamba la miti Saohill sio tuu kwa ajili ya mashindano ya mbio za magari pia utalii wa uoto wa asili na usio wa asili ,utalii wa bwawa la ngwazi ,Uvuvi wa kurejesha ,utalii wa makasia na mto Ruaha huku ikiwa na fursa kwa wawekezaji wengine.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.