Habari za Punde

Dk.Hussein Ameahidi Kuyafanyia Kazi Mapendekezo Yaliyotolewa na Tume ya Maboresho ya Mifumo ya Taasisi za Haki Janai

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taarifa za Haki Jinai Tanzania , ukiongozwa na Mwenyekiti wa Tume Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu Mohammed Othman Chande (kulia kwa Rais) na Makamu Mwenyekiti wa Tume Mhe.Balozi Ombeni Sefue, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 9-9-2023.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameahidi kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na Tume ya Maboresho ya mifumo ya taasisi za Haki jinai ambayo itatoa mwangaza kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu kuboresha mifumo na taasisi zinazohusiana na masuala hayo kwa nia ya kupatikana haki kwa ufanisi.

Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na tume hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Mstaafu Mohamed Othman Chande na Makamu Mwenyekiti Balozi Ombeni Sefue walipomkabidhi ripoti ya tume hiyo.

Alieleza Serikali zote mbili ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeyapokea mapendekezo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi kwa kina ili kuleta mabadiliko na mageuzi makubwa kwa nia ya kupatikana kwa haki nchini.

Alisema utekelezaji wa mapendekezo hayo kwa kiasi kikubwa unaendana na kutegemeana na taasisi zote za haki jinai za Bara na  Zanzibar.

Rais Dk. Mwinyi alizungumzia ushirikiano mzuri uliopo baina ya taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa ya Zanzibar ZAECA na ya kupambana na dawa za kulevya, zimepata msaada wa kujengewa uwezo na wenzao kutoka Bara kwa kupewa mafunzo.

“Bila shaka ni sahihi kabisa lazima kuwe na kubadilishana ujuzi na uzoefu, ushirikiano wa karibu” alisifu Rais Dk. Mwinyi.

Kuhusu mahakama ya rufani kufanya kazi zake Zanzibar, alisema tayari suala hilo linashughulikiwa pamoja na kuisifu Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuongeza nguvu kwenye ujenzi wa miundombinu ya Mahkama kuu ya Zanzibar.

Naye, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Othman Chande, alimueleza Dk. Mwinyi kwamba tume ilifanikiwa kuzifanyia kazi changamoto za taasisi 15 zilizopendekezwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zikiwemo Jeshi la Polisi, Ofisi ya taifa ya Mashitaka, Jeshi la Magereza.

Taasisi nyengine ni Mamlaka ya kuzuia na kupambana na Rushwa, Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya, Mahakama ya Tanzania, kitengo cha kudhibirti fedha haramu Uhamiaji, Mkemea Mkuu wa Serikali na taasisi nyengine zinazohusu masuala ya jinai kwa kutathmni ushirikiano wa taasisi hizo na kuangalia nidhamu, mifumo ya ajira, viwango vya weledi, tume ya upandishaji vyeo, ufanisi mahusiano, nidhamu, ufamnisi matumizi ya teknolojia na motisha.

Tume ya maboresho ya mifumo ya taasisi za Haki jinai imeundwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, Januari 31 mwaka huu na ilianza kazi zake mapema mwezi Februari kwa lengo la kutathmni mifumo ya haki jinai na kutathmini taasisi za haki jinai.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taarifa za Haki Jinai Tanzania , ukiongozwa na Mwenyekiti wa Tume Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu Mohammed Othman Chande (kulia kwa Rais) na Makamu Mwenyekiti wa Tume Mhe.Balozi Ombeni Sefue, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 9-9-2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa Ripoti ya Tume ya Kuangalia Jinsi ya Maboresho ya Taarifa za Haki Jinai na Mwenyekiti wa Tume Mhe.Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mohammed Othman Chande, baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 9-9-2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taarifa za Haki Jinai Tanzania na (kulia kwa Rais) Mwenyekiti wa Tume Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mohammed Othman Chande na Katibu wa Tume Ndg.Al Khalil Mirza (kushoto kwa Rais) Makamu Mwenyekiti wa Tume Balozi Ombeni Sefue na Mjumbe wa Tume Msafiri Ramadhan Msafiri
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Mwenyekiti wa Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taarifa za Haki Jinai Tanzania Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mohammed Othman Chande, baada ya kumaliza mazungumzo na kukabidhi ripoti ya Tume, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 9-9-2023. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.