Habari za Punde

Equity Bank Zanzibar Yaahidi Kusaidia Sekta ya Elimu

Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equity Tanzania Isabella Maganga akiangalia hatua za utengenezaji wa sabuni ya maji kutoka kwa wanafunzi wa Skuli ya Trifonia Academy wakati aliposhiriki mahafali ya 15 na kumbukizi ya kutimiza mioaka 25 ya kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.

Na Fauzia Mussa         Maelezo

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kutoa elimu bora kwa wanafunzi Benk ya Equity imesema itaendelea  kusaidia huduma zinazohitajika ikiwemo vifaa vitakavyowezesha wanafunzi kusoma katika mazingira rafiki.

 

Akizungumza  katika Mahafali ya 15 na Sherehe ya kutimiza miaka  25 tangu kuanzishwa kwa Skuli ya Trifonia Academy Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equit Tanzania Isabella Maganga  amesema hatua hiyo itawasaidia walimu kuwasomesha wanafunzi katika mazingira yaliobora ili kuongeza ufaulu mzuri kama ilivyo adhma ya Serikali .

 

Aidha aliwasisitiza wazazi na walezi kuwa tayari kuwapokea watoto wao,  kwa kuwa nao karibu na kufuatilia nyendo zao ili  kuwakinga na vitendo vya udhalilishaji mara tu  wanaporudi majumbani mwao.

 

Alisema malengo ya mtoto wa kike ni makubwa Sana hivyo ipo haja wazazi kushirikiana na walimu katika   kuwaendeleza na  kuhakikisha wanafikia malengo waliyoyatarajia.

 

Vilevile aliiwashauri Walimu kuwafundisha wanafunzi  kazi za mikono za kujishughulisha wanaporudi katika jamii ili kuepuka kukaa katika vikundi viovu.

 

“Tujitahidi kuwafundisha kazi za amali na ujasiriamali ili wapate maarifa yatakayowasaidia baada ya kumaliza masomo na kuchanganyika na jamii”alisistiza Isabella

 

 Hata hivyo Aliwataka mabinti  kutokuuchezea muda ambao watakua wanasubiria  hatua nyengne ya masomo na kuwataka kujiendeleza katika kazi za mikono ili wawe Wanawake wa mfano  watakapoanza maisha ya uraiani 

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Skuli yaTrifonia Grese Peter Myamba aliwasisitiza wanafunzi kujiandaa vyema na Mitihani yao ya Taifa na kuwashukuru wazazi na walezi kwa mashirikiano yao  hadi kufikia kutimiza miaka 25.

 

Mapema akisoma risala ya wanafunzi  Mwanafunzi Rauhiya Othman Ali amesema Skuli ya Trifonia imepata mafanikio mengi ikiwemo kuwa na mahusiano chanya kati yao  na  jamii.

 

Mbali na hayo alieleza kuwa  skuli inakabiliwa na changamoto ya  uhaba  wa vifaa vya kusomea kwa vitendo pamoja  na vitabu vya ada na kiada.

 

Alifahamisha kuwa  skuli hiyo ipo pembezoni mwa barabara  finyu ,hivyo waliiomba Serikali kuongeza alama za barabarani,matuta na kuweka Askari wakuongoza wanafunzi  wakati wa kwenda na kurudi Skuli  ili kuepusha ajali za mara kwa mara.

 

Katika mahafali hayo jumla ya Wanafunzi 68 wa kidato cha nne, 74 wa darasa la saba walikabidhiwa vyeti vya kuhitimu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equit Tanzania Isabella Maganga akiangalia hatua za uchujaji wa maji taka kutoka kwa wanafunzi wa Skuli ya Trifonia Academy wakati aliposhriki mahafali ya 15 na kumbukizi ya kutimiza mioaka 25 ya kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equit Tanzania Isabella Maganga akiangalia hatua za uchujaji wa maji taka kutoka kwa wanafunzi wa Skuli ya Trifonia Academy wakati aliposhriki mahafali ya 15 na kumbukizi ya kutimiza mioaka 25 ya kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.
Wanafunzi wa Skuli ya Trifoni wakicheza  Ngoma ya mganda wakati wa sherehe ya mahafali ya 15 na kumbukizi ya kutimza mika 25 tangu kuanzishwa kwa Skuli hiyo.

Wahitimu wa Darasa la Saba Skuli ya Trifonia wakiimba wimbo maalum wakati wa sherehe ya mahafali ya 15 na kumbukizi ya kutimza mika 25 tangu kuanzishwa kwa skuli hiyo.

Muhitimu wa kidatu cha nne  Skuli ya Trifonia Rauhiya Othman Ali akizoma Risala ya wanafunzi wakati wa sherehe ya mahafali ya 15 na kumbukizi ya kutimza mika 25 tangu kuanzishwa kwa skuli hiyo.

Mkurugenzi wa Skuli yaTtrifonia Grese Peter Myamba akizungumza machache wakati akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equity Tanzania Isabella Maganga kuzungumza na wahitimu wakati wa sherehe ya mahafali ya 15 na kutimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwa Skuli hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equity Tanzania Isabella Maganga alipokua akizungumza na wahitimu wa Skuli ya Trifonia wakati wa mahafali ya 15 na sherehe ya kutimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equity Tanzania Isabella Maganga akikabidhi msaada wa Komputa kwa Mkurugenzi skuli ya Trifonia Academy Grace Peter Myamba wakati wa mahafali ya 15 na sherehe ya kutimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equity Tanzania Isabella akimkabidhi cheti muhitimu wa kidatu cha nne Abubakar Issa wakati wa mahafali ya 15 na sherehe ya kutimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benk ya Equity Tanzania Isabella akimkabidhi cheti muhitimu wa kidatu cha nne Awatif  Malik wakati wa mahafali ya 15 na sherehe ya kutimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwa skuli hiyo huko Mambosasa Zanzibar.

PICHA NA FAUZIA MUSSA –MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.