RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya Finland kwa jitihada zake za
kuiunga mkono Zanzibar na kuisaidia kwenye masuala mbalimbali ya uchumi na
Maendeleo.
Dk. Mwinyi alitoa
shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Balozi wa Finland nchini,
Theresa Zitting.
Alisema hatua
ya Serikali ya Finlanda kuisaidia Zanzibar kwenye sekta mbalimbali ikiwemo
Elimu, Kilimo, Afya, masuala ya wanawake hasa mapambano dhidi ya udhalilishaji
wa jinsia kwa kushirikiana na taasisi na wanaharakati mbalimbali wanaopinga
udhalilishaji wa wananwake na watoto.
Akizungumzia
sekta ya utalii, Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi huyo juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuiimarisha
sekta hiyo inayochangia asilimia 30 ya pato la taifa.
Alisema, Zanzibar inaimarisha Sera yake kuu ya Uchumi wa Buluu inayobeba mambo
matano ikiwemo Utalii, Uvuvi, Usafiri wa vyombo vya bahari, Bandari, Mafuta na
gesi na kumueleza Balozi huyo kuangalia fursa za uwekezaji kwenye maeneo hayo.
Alisema sekta
ya Utalii inajumuisha fukwe nzuri nyenye
mvuto wageni pamoja na utalii wa urithi na kuongeza kuwa kuna fursa nyingi za
uwekezaji hivyo alimueleza Balozi hyo kuangalia namna ya kuzitumia fursa hizo.
Akizungumzia
sekta ya Uvuvi, Rais Dk. Mwinyi alimweleza mgeni huyo kwamba Zanzibar imejikita
zaidi kwenye kilimo cha viumbe wa baharini ikiwemo ufugaji wa samaki na
vifaranga, matango ya bahari na ukulima wa mwani ambao umewamuisha sehemu kubwa
ya wanawake na vijana na kupunguza changamoto za ajira.
Kuhusu Usafiri
wa vyombo vya baharini Dk. Mwinyi alieleza unajumuisha bandari za Zanzibar, Dar
es Salaam Pemba na Tanga kwa kusafirisha abiria na mizigo hivyo alieleza kuna
fursa nyingi za uwekezaji kwenye eneo hilo.
Pia Rais Dk.
Mwinyi alimueleza balozi huyo, kuangalia ushirikiano wa kuiungamkono Zanzibar
kwenye miundombinu ya elimu, afya na nishati hasa kwenye masuala ya mifumo na
vitendea kazi.
Naye, Balozi
Theresa Zitting alimueleza Dk. Mwinyi kwamba Serikali ya Finland inafanyakazi
kwa karibu zaidi na Serikali ya Zanzibar ambayo wanashikiriana kwenye Masuala
mbalimbali ya maendeleo.
Alisema Finland
imeshirikiana sana na Tanzania hasa kwenye sekta za Elimu, na kuimarisha miradi mingi ikwemo uhifadhi wa mazingira, ardhi, misitu na masuala mengine ya maendeleo.
Balozi Zitting alisema Finland inathamini sana uhusiano na ushirikiano
uliopo baina yao na Tannzania ikiwemo Zanzibar pamoja na nchi zote zilizopo
Afrika Mashariki.
Balozi Theresa
Zitting yupo nchini tokea mwezi Septemba mwaka 2022 kwenye ubalozi wao uliopo
Dar es Salaam.
IDARA YA
MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment