Habari za Punde

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Amefungua Mkutano Mkuu wa Tisa wa Lishe Arusha

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Richard Ngemela kuhusu mashine ya kusaga nafaka na kuongeza virutubishi kwenye nafaka inayosagwa wakati alipotembelea banda la maonesho la kampuni ya Gain Tanzania kabla ya kuhutubia Mkutano Mkuu wa Tisa wa Lishe   kwenye ukumbi wa hoteli ya Mount Meru jijini Arusha, Oktoba 26, 2023. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Jenista Mhagama.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Bebes Products , Joyce Singo kuhusu  vyakula mbalimbali vyenye virutubishi muhimu kwa afya ya binadamu alipotelea mabanda ya maonesho kabla ya kuhutubia Mkutano Mkuu wa Tisa wa Lishe   kwenye ukumbi wa hoteli ya Mount Meru jijini Arusha, Oktoba 26, 2023. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Jenista Mhagama.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofunga Mkutano  Mkuu wa Tisa wa Lishe   kwenye ukumbi wa hoteli ya Mount Meru jijini Arusha, Oktoba 26, 2023.


(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.