Habari za Punde

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Kairuki Kujenga Kisima katika Shule ya Kibacha Wilayani Same

Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (wa pili kulia mstari wa mbele) katika picha ya pamoja na wahitimu wa Kidato cha Nne katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  ya  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro Oktoba 5, 2023.  Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni (kushoto), Katibu Tawala wa Wilaya ya Same, Upendo Wella (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Annastazia Tutuba (kulia)

Na Happiness Shayo-Same

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) ameahidi kujenga kisima kikubwa cha maji katika Shule ya Sekondari  Kibacha Wilayani Same, kwa lengo la kuendeleza kilimo cha mbogamboga na kuboresha lishe bora shuleni hapo.

Ameyasema hayo leo Oktoba 5, 2023 katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  katika  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro.

"Nimeguswa na ujumbe wa igizo la Watoto hawa kuhusu changamoto ya maji, naomba nitamke kuwa nitaijengea shule hii Kisima kikubwa cha maji ambacho pia kitawezesha kuendeleza kilimo cha mboga mboga na viazi lishe kwa ajili ya kuchangia lishe ya watoto wetu na hivyo kutimiza azma ya Serikali ya kuhakikisha suala la lishe shuleni linapewa kipaumbele" Mhe. Kairuki amesisitiza.

Mhe. Kairuki amefafanua kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu na ilishaiona changamoto ya maji wilayani hapo hivyo, ipo kwenye hatua nzuri ya ukamilishwaji hadi kufikia mwaka 2024 Wilaya ya Same itakuwa na maji ya kutosha.

Aidha, ameipongeza Serikali kwa kutoa fedha za miradi  mbalimbali  ya elimu  ili kuboresha sekta hiyo.

" Serikali kupitia Mradi wa Lipa kulingana na matokeo imetoa shilingi Billioni 7.5 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni, vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika Shule za Sekondari za Kidato cha Tano na Sita kote nchini."

Ameongeza kuwa Serikali pia imetoa shilingi Billioni 48 kujenga Shule za Wasichana za Bweni katika mikoa 16 Tanzania Bara na kupitia Mradi wa SEQUIP.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kairuki  amewaasa vijana wanaohitimu Kidato cha nne kuzingatia maadili ya  Mtanzania na kuzingatia masomo.

"Vijana mnaohitimu Kidato cha Nne  mwaka huu, mnapaswa kuelewa kuwa wazazi wenu na Taifa lina matarajio makubwa kutoka kwenu. Mnapaswa kuweka jitihada katika masomo yenu na kuwa na maadili mema kwa ajili ya ustawi wa Taifa letu ma msijiingize katika maadili yanayofedhehesha utamaduni wetu ikiwemo ushoga na mengineyo." Mhe. Kairuki amesema.

Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza  katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  katika  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro leo Oktoba 5, 2023 ambapo ameahidi kuwajengea Kisima cha maji kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji shuleni hapo.
Baadhi ya wahitimu wa Kidato cha Nne wa  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb)(hayupo pichani) akizungumza  katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  katika  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro yaliyofanyika  Oktoba 5.
Baadhi ya wazazi , ndugu, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliohitimu  Kidato cha Nne katika  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro wakifuatilia matukio katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  ya shule hiyo yaliyofanyika Oktoba 5.
Baadhi ya washiriki wa mahafali ya saba ya Kidato cha Nne ya katika  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro wakifuatilia matukio katika mahafali hayo yaliyofanyika Oktoba 5, 2023.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibacha, Ngoka Manongi akitambulisha  baadhi ya wageni walioshiriki Mahafali ya saba ya Shule ya Sekondari Kibacha, Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro leo Oktoba 3,2023. Katikati ni Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Angellah Kairuki (Mb) na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni.
Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kulia) akimkabidhi cheti mmoja wa Wahitimu wa Kidato cha Nne mwenye changamoto ya ulemavu wa miguu, Naomi Mathayo katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  ya  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro Oktoba 5, 2023.
Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akimkabidhi cheti Mhitimu wa Kidato cha Nne, Shabani Ibrahim katika mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  ya  Shule ya Sekondari Kibacha,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro Oktoba 5, 2023.  Anayeshuhudia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibacha, Ngoka Manongi.
Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akiangalia maonyesho ya kisayansi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Kibacha akiwa ameongozana na uongozi wa shule pamoja na uongozi  kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Same, kabla ya  mahafali ya 7 ya Kidato cha Nne  ya  Shule hiyo iliyopo,  Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro Oktoba 5, 2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.