Habari za Punde

Mwakilishi Viti Maalumu CCM Akabidhi Mifuko ya Saruji Minanasini

Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharibi 'Kichama Mhe. Fatma Ramadhan Mandoba akikabidhi Mifugo ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Maskani ya Chama cha Mapindizi huko Mwera Minanasini Wilaya ya Maghatibi 'A'Unguja.
Baadhi ya Viongozi na Wanachama wa Maskani ya Minanasini wakimsikiliza kwa makini Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharibi 'Kichama Mhe. Fatma Ramadhani Mandoba (hayupo pichani) mara baada ya kukabidhi Fedha taslim katika Jimbo la Mtoni Wilaya ya Maghatibi 'A'Unguja.
Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharibi 'Kichama Mhe. Fatma Ramadhan Mandoba akizungumza na Wanachama na Wakereketwa wa Maskan ya Mwera Minanasini Wilaya ya Magharibi "A" Unguja.

Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharibi Kichama Mhe. Fatma Ramadhan Mandoba amewataka Wanachama wa Chama cha Mapindizi kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Viongozi wao katika kuimarisha Chama na kuwaletea maendeleo Wananchi.

Ameyasema hayo huko Mwera Minanasini Wilaya ya Magharibi 'A' wakati akikabidhi Mifuko ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Maskan ya Mwera Minanasini.


Amesema Wanachama hao, iwapo watadumisha Upendo, Umoja na Mshikamano wataweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuongeza idadi ya Wanachama wanaojiunga na Chama hicho.


"Uchaguzi ni namba, hatuwezi kuendelea kushinda bila ya kuwa na idadi kubwa ya Wanachama, watakaoweza kukipigia kura Chama Chetu ifikapo 2025 ili kiendelee kushika Dola” alisema Mwakilishi huyo.


Amesema Chama cha Mapinduzi ni Chama imara na kipo msatari wa mbele katika kutekeleza ahadi zake kwa Wananchi na kuwaomba Wananchi kuendelea kukiamini na kukiunga mkono ili kiendelee kuwatumikia Wananchi.


Aidha aliwapongeza Viongozi na Wanachama wa Maskani ya Minanasini kwa kuamua kuanzisha Maskani hiyo jambo ambalo limewaunganisha pamoja na kuimarisha uhai wa Chama na Jumuiya zake.


Wakati huo huo Mhe. Mandoba alikabidhi Fedha taslim kwa Uongozi wa UWT Jimbo la Mtoni ili waewze kuongeza Mitaji ya vikundi vya Ujasiriamali walivyovianzisha.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.