Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali
itaendelea kuchukua juhudi maalum kuhakikisha inapunguza kasi
ya ongezeko la Maradhi yasiombukiza hapa nchini
Rais Dk,Mwinyi ametoa tamko hilo alipozungumza baada ya Kuongoza matembezi ya Afya yalioandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Taasisi ya Pharm Access ikiwa ni kampeni maalum ya kudhibiti Maradhi yasioambukiza kwa jamii yalioanzia Kiembe Samaki kwa Boutros hadi Uwanja Mao Tse Tung Wilaya ya Mjini.
Rais Dk,Minyi amefahamisha kuwa Tafiti zimeonesha kuwa Mazoezi yanasaidia kwa kiasi kikubwa kujenga Afya ya Mwili ,afya ya akili na kuondosha Msongo wa Mawazo na kusisitiza jamii kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi kila siku
Aidha Dk, Mwinyi ameeleza kuwa Takwimu za Wizara ya Afya zimeeleza kuwa kuna Ongezeko la Maradhi Yasioambukiza kwa kiwango kikubwa ikwemo Kisukari, Presha , Uzito na Unene uliopitiliza na shinikizo la damu kunakosababishwa na watu wengi kutofanya mazoezi.
Rais Dk, Mwinyi ameeleza kuwa kutofanya Mazoezi kwa Wananchi walio wengi kunarejesha nyuma juhudi za Serikali za kudhibiti Maradhi hayo na kupunguza kasi ya kuleta Maendeleo.
Aidha Rais Dk,Mwinyi amesisitiza kuwa Serikali imeendelea kushirikiana na taasisi za Afya kutoa Elimu na kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa kufanya mazoezi kwa ajili ya kuimarisha afya zao.
Amefahamisha kuwa Mazoezi yanasaidia kuondoa Msongo wa Mawazo , kuimarisha Usingizi na kuleta furaha.
Ameeleza kuwa wizara ya Afya imeendelea kutoa matibabu bora katika Vituo 60 viliopo Unguja na Pemba na Kuwasisitiza wananchi kuvitumia Vituo hivyo kupata ushauri wa Kitaalamu wa afya zao.
Rais Dk, Mwinyi ametoa wito kwa kila mmoja kuchukua hatua ya kupunguza Mafuta na matumizi ya vyakula vya wanga kukabiliana na maradhi hayo.
Ameeleza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Taasisi Gez Health Initiative inaendelea kutoa Elimu ,kufanya Uchunguzi wa Awali wa Maradhi ya Saratani kupitia Mradi wa miaka mitano wa kudhibiti Saratani pamoja na Ujenzi wa kituo cha Umahiri cha Saratani hapa Zanzibar.
Rais Dk, Mwinyi ameshauri kuendelezwa na kupangiwa Utaratibu mzuri wa Matembezi ya pamoja na mazoezi .
Aidha Amezipongeza Taasisi mbalimbali zinazoshirikiana na Serikali kufanikisha juhudi za Kudhibiti Maradhi yasioambukiza
Waziri wa Afya Nassor Ahmed Mazrui amesema Dhamira ya Serikali ni kuona wananchi wote wana afya njema na kutambua kuwa suala la kufanya mazoezi sio anasa na Wizara najiandaa kuwa na siku maalum ya mazoezi kila mwezi.
Ametoa rai kwa Taasisi za Umma na binafsi kuandaa utaratibu wa kuwa na siku maalum ya kufanya mazoezi.
Mkurugenzi wa Pharm Access Kheri Marwa ameeleza kuwa tatizo la Maradhi yasioambukiza ni kubwa duniani kote hivyo juhudi kubwa zinapaswa kuchukuliwa kuhamasisha ufanyaji wa mazoezi kwa wananchi.
Matembezi hayo ya Afya yamebeba Kaulimbiu inayosema "Chagua Mazoezi kuwa Sehemu ya Maisha ".
No comments:
Post a Comment