Habari za Punde

Waziri Mhe.Hamza Ashirki Katika Dua ya Kumuombea Rais Mstafu wa Zanzibar Marehemu Sheikh Idrisa Abdulwakil Iliyofanyika Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais Sera ,Uratibu na Baraza la Wawakilishi Uamza Hassan Juma (Mwenye koti jeusi) akiwa pamoja na Viongozi mbalimbali wakiomba Dua katika Kaburi la Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdulwakil hafla iliofanyika Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni  Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi Mhe Hamza Hassan Juma amesema Serikali imeanzisha utamaduni wa kuwaombea dua waasisi na Viongozi waliiotangulia ili kuwaenzi viongozi hao.

Ameyasema hayo huko Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja  katika ziara ya kumuombea Dua aliyekua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi awamu ya nne Marehemu Idriss Abul_Wakil.

Amesema kuwa utamaduni wa kuwaombea Dua viongozi hao ni njia moja ya kurithisha vizazi vijavyo kwani walikua na sifa njema  hivyo ipo  haya ya kujifunza ili  kua na mustakbali mwema wa maisha.

Waziri Hamza amefahamisha kuwa wazee hao walikua na sifa njema , umoja na mshikamano  katika kuipigania Amani ya Nchi ili vizazi viweze kuwa salama.

"Wazee wetu hawa walitumia hekma na busara  wakati wa kuapambania Nchi yetu na sisi tujifunze kupitia Hawa ili kua na muatakabali wema" alisema

Aidha amewasisitiza wananchi kuilinda na  kudumisha Amani na utulivu uliopo nchini  katika kipindi Cha Uchaguzi na baada ya Uchaguzi ili kuepusha athari zinaowwza kukitokeza.

Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja  Othman Ali  Maulid amesema maisha  ya wanadamu ni hadithi hivyo ni vyema kufanya mema ili kukumbukwa kwa wema pindi atakapoondoka duniani.ae mmoja wa wana Familia ambae ni mtoto wa Marehemu  Yahya Idissa Abdul_ Wakil amesema kuwa wao binafsi wamefarajika kuona wanakumbukwa kila mwaka na kuiomba Serikali ya Mapinduzi kuendeleza jambo hilo la kheri.
Mkuu wa Wilaya ya Kusini Othman Ali Maulid akitoa hotuba kumkaribisha Mgeni Rasmi katika hafla ya Dua ya kumuombea Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdul wakil hafla iliofanyika katika kaburi lake Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.
Baadhi ya Wananchi mbalimbali waliohudhuria katika Dua ya kumuombea Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdul wakil hafla iliofanyika katika kaburi lake Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni  Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais Sera ,Uratibu na Baraza la Wawakilishi Uamza Hassan Juma akitoa hotuba katika hafla ya Dua  ya kumuombea Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdul wakil hafla iliofanyika katika kaburi lake Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni  Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais Sera ,Uratibu na Baraza la Wawakilishi Uamza Hassan Juma akitikia Dua  ya kumuombea Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdul wakil hafla iliofanyika katika kaburi lake Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni  Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.
Kadhi wa Wilaya ya Kusini Abubakar Ali Mohamed akiongoza Dua ya kumuombea Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdul wakil hafla iliofanyika katika kaburi lake Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.
Kiongozi wa Familia Yahya Idriss Abdulwakil akitoa neno la Shukrani baada ya Dua  ya kumuombea Rais Mstaafu Awamu ya Nne Sheikh Idriss Abdul wakil hafla iliofanyika katika kaburi lake Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni  Wiki ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu wa Kwanza wa Chama cha Afro shirazi pamoja na siku ya kumbukumbu ya Marehemu shekh Abeid Amani Karume.




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.