Habari za Punde

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Akutana na Kuzungumza na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Abdullah Bin Al Nahyan

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdullah Bin Zayed Al Nahyan tarehe 05 Mei, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdullah Bin Zayed Al Nahyan, wakishuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano baina ya Wizara ya Afya na Wizara ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuhusu uwezeshaji wa ujenzi wa Hospitali ya The Emirates – Tanzania Bukoba mkoani Kagera, tarehe 05 Mei, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdullah Bin Zayed Al Nahyan, wakishuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuhusu ushirikiano katika uwekezaji kwenye sekta ya madini, tarehe 05 Mei, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdullah Bin Zayed Al Nahyan, wakishuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano baina ya Shirikisho la Vyama vya Biashara na Viwanda vya UAE na Barazala la Taifa la Biashara kuhusu uanzishwaji wa Baraza la Pamoja la Biashara kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu na Tanzania tarehe 05 Mei, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.