Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Amekabidhiwa TUZO Maalum ya Muhamasishaji Bor wa Uwekezaji Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akielekea katika ukumbi wa mkutano wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kuembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar kwa ajili ya hafla maalumu ya chakula na utoaji wa Tuzo kwa Wawekezaji mbalimbali waliowekeza Zanzibar, iliyoandaliwa na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) iliyofanyika jana usiku 17-6-2025,na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Idrisa Kitwana Mustafa na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi.Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Shariff Ali Shariff.
WAWEKEZAJI mbalimbali na wageni waakikwa wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichai) akihutubia katika hafla maalumu ya Chakula cha usiku na utoaji wa TUZO kwa Wawekezaji,iliyoandaliwa na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B”Unguja Jijini Zanzibar jana usiku 17-6-2025


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa TUZO Maalumu ya kuwa Muhamasishaji Bora wa Sekta ya Uwekezaji Zanzibar,akikabidiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi,Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Shariff Ali Shariff (kushoto kwa Rais) wakati wa hafla ya chakula maalumu na utoaji wa Tuzo kwa Wawekezaji Zanzibar,iliyoandaliwa na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar jana usiku 17-6-2025
















 



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.