Na Hamad Hija-Maelezo Zanzibar 07/05/2012
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Tawi
la Tomondo Wilaya ya Magharibi Mjini Zanzibar jana walifanya uchaguzi katika
nafasi mbali mbali za tawi ambapo Hassan Kipanga Abdulla alichaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa Tawi hilo .
Katika uchaguzi huo Hassan Kipanga
Abdulla (Pomporipo) alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa tawi hilo baada ya kupata kura 116 na kumshinda
mpinzani wake Said Ramadhan Nundu aliyepata kura 53.
Kufuatia matokeo ya uchaguzi huo msimamizi
wa uchaguzi wa tawi hilo Waziri Omar Salim
alimtangaza rasmi Hassan Kipanga Abdulla kuwa Mwenyekiti mpya wa tawi hilo la Tomondo
Aidha katika uchaguzi huo wanachama
walimchaguwa Hemed Ibrahim Masuod kuwa Katibu wa tawi hilo kwa kupata kura 35 na kumshinda mpinzani
wake Khamis Hamza Abdulla aliyepata kura 22.
Nafasi nyengine iliyogombaniwa ilikuwa ya Katibu
mwenezi ambapo katika nafasi hiyo Siajabuni Ali Mpate aliwashinda wapinzani
wenzake kwa kupata kura 30 ambapo wapinzani wake Rose Merry alipata kura 24
wakati Mohd Ali Mpate aliambulia kura 4.
Katika uchaguzi huo uliofanyika kwa
aman na utulivu ulimchagua pia Amina
Issa kuingia katika mkutano mkuu jimbo kwa kupata kura 90 na kumshinda mpinzani
wake Benard Litope aliyepata kura 69.
Awali kulifanyika uchaguzi mwishoni mwa
wiki hii ambapo Amri Said Hongo alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Wazazi wa tawi hilo baada ya kupata kura
24 na kumshinda mpinzani wake Clementina Faustine Mapuri aliyepata kura 16 kati
ya kura 44 zilizopigwa.
Kufuatia Hassan Kipanga Abdulla kuchaguliwa
kuwa Mweyekiti mpya wa tawi la Tomondo kulimuwezesha kutoa shukurani kwa
wanachama wenzake waliomuamini kumpa dhamana hiyo ya uongozi.
Kipanga alisema kuwa uongozi ni dhamana na
hivyo kuahidi kuitumikia nafasi hiyo kwa moyo wake wote akiwa Mwenyekiti mpya
wa Tawi la Tomondo.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 07/05/2012
No comments:
Post a Comment