Na Rajab Mkasaba
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amemtumia salamu za
rambi rambi Mfalme Abdullah bin Abdulaziz Al-Saud wa Saud Arabia, kufuatia
kifo cha Prince Nayef bin Abdulaziz al-Saud aliyetarajiwa kurithi kiti
cha Mfalme na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Saud Arabia.
Katika salamu
hizo za rambi rambi Dk. Shein alisema kuwa yeye mwenye binafsi wananchi wa
Zanzibar wamepata mshtuko na huzuni kubwa baada ya kupata taarifa ya kifo cha
Prince Nayef bin Abdulaziz al-Saud.
Kwa upande wake
Dk. Shein pamoja na wananchi wa Zanzibar wanatuma salamu za pole na rambi rambi
kwa wananchi wa Saud Arabia kufuatia kifo cha kiongozi huyo.
Aidha, salamu
hizo za rambirambi ziliwapa pole familia, marafiki, ndugu na jamaa pamoja na
wananachi wote wa Saud Arabia na kueleza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana
na ndugu zao hao wa Saudi Arabia katika msiba huo.
Salamu hizo
zilieleza kuwa Price Nayef atakumbukwa kwa wema wake mkubwa kwa umma wa Wailamu
walio wengi katika juhudi zake za kuendeleza na kuiimarisha din i ya Kiislamu
pamoja na kuimarisha maendeleo katika nchi yake.
Sambamba na hayo
salamu hizo zilimuomba Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amin.
Prince Nayef
alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Saudia Arabia tangu mwaka wa 1975, na mwezi
Oktoba mwaka jana, akiwa na umri wa miaka 78, aliteuliwa kuwa ndiye
atakayemrithi Mfalme wa sasa, Mfalme Abdullah.
No comments:
Post a Comment