Na Mwantanga Ame
JUMLA ya Wazanzibari 10,578 wamepatiwa
vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi baada ya kukamilisha masharti ya kisheria ya
kuweza kupata vitambulisho hivyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Mwinyihaji Makame, aliyasema hayo jana wakati
akisoma hotuba ya bajeti ya Mapato na
Matumizi ya Ofisi kwa mwaka wa fedha 2012/2013, huko katika ukumbi wa Baraza la
Wawakilishi, Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Waziri Mwinyihaji, alisema ndani ya kipindi
cha mwaka huu wa fedha Wazanzibari 10.578 wamefanyiwa usajili kwa ajili ya
kupatiwa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi.
Alisema katika
usajili huo jumla ya vitambulisho vipya 3,923 vilitengenezwa baada viliopo
kumaliza muda wake wa matumizi huku wafanyakazi wa serikali waliopatiwa huduma
hiyo walifikia 10,393.
Alisema hivi
sasa Idara hiyo pia imeshaandaa rasimu kwa ajili ya kuifanyia marekebisho
sheria namba 7 ya 2005 ikiwa ni hatua ya kutoa vitambulisho kwa wageni wanaoishi
hapa nchini.
Alisema rasimu
hiyo tayari imeshapitishwa na Baraza la Mapinduzi na hivi sasa inasubiri
kufikishwa katika Baraza la Wawakilishi ili kuweza kuanza kujadiliwa.
Alisema tangu
mfumo huo kuanza kutumika Idara hiyo imeweza kuhakikisha inatimiza masharti ya
kimataifa kwa mara ya sita mfululizo na imeweza kushinda kufikia viwango bora
duniani.
Alisema kwa ujao
wa fedha itaendelea kusajili Wazanzibari 10,500 wanaotimiza masharti ya usajili
na kuwapatia vitambulisho pamoja kutengeza vitambulisho kwa waliomaliza muda.
Akizungumzia juu
ya Idara ya Usalama Kazini (GSO), Waziri huyo alisema jumla ya wafanyakazi 554
kutoka katika taasisi mbali mbali za serikali walifanyiwa upekuzi na taasisi 12
zilikaguliwa kuangalia utunzaji wa siri za seriakali.
Akizungumzia
Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Uratibu wa shughuli za Wazanzibari
Wanaoishi Nchi Nje, alisema kimeweza kufanya ziara mbali mabali katika nchi za
falme za kiarabu kwa Oman na Dubai ikiwa ni hatua kukutana na Wazanzibari ili
kuwashajiisha katika kushiriki kuchangia maendeleo ya Zanzibar
Akizungumzia juu
ya mradi wa mageuzi ya Serikali za Mitaa Waziri huyo alisema sera yake
imekamilika baada kupitishwa kwa wadau tofauti zikiwemo taasisi binafsi ikiwa
ni hatua ya kupata maoni yao.
Aidha, upande wa
uratibu wa Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa, Waziri huyo, alisema tayari
kuna mradi ambao utahusisha ujenzi wa misingi ya maji ya mvua kwa ajili ya
maandalizi ya kutafuta mkandarasi ataeifanya kazi hiyo ambayo inatarajiwa
kuyanufaisha maeneo ya ziwa la Sebleni, Ziwa la Mtumwajeni na Ziwa la kwa binti
Amrani.
Maziwa mengine
yatayofaidika na mradi huo Waziri huyo alisema ni la Mantenga, Kwamtipura,
Kilima hewa karakana, Sogea, Mpendae, Jang’ombe, Uwanja wa Demokrasia na Shauri
Moyo.
Akizungumzia juu
ya shughuli za Mikoa yote ya Unguja na Pemba Waziri huyo alisema walifanikiwa
kwa kiai kikubwa kutekeleza bajeti zao huku wakisimamia utekelezaji wa utoaji
wa huduma za kijamii kwa kushirikia katiika kampeni mbali mbali za chanjo kwa
watoto pamoja na kuimarisha hali ya ulinzi na usalama, kusimamia mapato pamoja
na kutoa mchango wa kupambana na maradhi ya ukimwi.
Akizungumzia juu
ya shughuli za Idara Maalum za SMZ, alisema nazo zimeweza kutekeleza vyema
majukumu yao ya kiulinzi na kutoa huduma mbali mbali katika jamii.
Akifafanua
waziri huyo alisema katika Idara ya Mafunzo serikali iliweza kuwahudumia
wanafunzi 479 ambapo kati ya hao 17 ni wanawake ikiwa ni ongezeko wanafunzi 17
waliopokelewa kwa mwaka 2010/2011 huku mahabusu wakifia 2,620 ambapo kati ya
hao 2,510 wanaume na wanawake ni 110 ambapo makosa yao makubwa ni wizi kutumia
nguvu, kubaka, kunja nyumba na kuiba wizi wa mazao na shambulio.
Upande wa Idara
ya Zimamoto Waziri huyo alisema, nayo imeweza kufanya kazi vizuri ikiwa pamoja
na kupata kifaa kipya cha kuzimia moto cha Dry Sprinkler Power Aerosal (DSPA).
Idara ya
Valantia, Waziri huyo alisema kimeweza kuisaidia serikali katika kusimamia
vyema kazi za uchumaji wa karafuu katika msimu uliomalizika.
Kuhusu Kikosi
cha JKU, Waziri huyo alisema, kimefanya mapitio ya uendeshaji wa shamba la
Bambi la mboga mboga ili liweze kuwa na tija iliyokusudiwa.
Akizungumzia juu
ya kikosi cha KMKM, alisema serikali kwa mwaka uliopo wameweza kukipatia vifaa
kiasi cha kuweza kukamata mafuta ya dizeli lita 25,950 petro ;o lita 1,790 sukari kilo 20,250,
mchele kilo 76,800 na karafuu mbichi 200
Waziri huyo
aliwaomba Wajumbe wa baraza hilo kumuidhinishia shilingi 50,698.1 milioni kati
ya hizo shilingi 46,654.1 milioni kwa matumizi ya Kawaida na kazi za maendeleo
ni shilingi 1,906.0 milioni na shilingi 2,138 milioni ni ruzuku kwa Baraza la
Manispaa na Mabaraza ya Miji.
No comments:
Post a Comment