Na Mwashamba Juma na Gilbert Massawe AJTC
WIZARA wa Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Vijana, Wanawake na
Watoto imesema jumla ya kesi 215 za udhalilishaji watoto kijinsia zilifikishwa
wizarani hapo katika kipindi cha 2012 /
2013.
Kesi hizo zikiwemo za kubaka, kulawiti, kupewa
ujauzito, kukashifiwa pamoja na kudhalilishwa kimwili ziliripotiwa sambmba
na kesi 689 za udhalilishaji watoto
zilizoripotiwa katika kituo cha mkono kwa mkono pamoja na idadi ya kesi 393 za
malalamiko yanayohusu matunzo na kugombania watoto Unguja na Pemba.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Wizara hiyo, Zainab
Omar Mohammed katika hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka
wa fedha 2012/2013 barazani mwishoni mwa wiki.
Waziri Zainab alisema katika mwaka wa fedha
2012/2013 wizara yake inaendelea kupokea malalamiko ya wanawake na watoto
kuhusu udhalilishaji, na unyanyasaji watoto, ambapo kwa mwaka wa 2011/2012
jumla ya malalamiko 132 yalipokelewa
wizarani hapo, na kupatiwa ushauri na malekezo yanayofaa katika maeneo ya
Unguja na Pemba.
Alifahamisha kuwa baadhi ya malalamiko
yaliyopokelewa wizarani hapo ni pamoja na kutelekezwa watoto, kwenye mgawanyo
wa mali, mimba nje ya ndoa, kupigwa, shambulio la matusi, kukashifiwa pamoja na
shambulio la vitisho.
Aidha alisema wizara yake ilizindua rasmi
matokeo ya utafiti wa udhalilishaji watoto (VAC) mwezi Juni 2011 ambapo wadau kutoka sekta za Afya,
Elimu, Polisi, Ustawi wa jamii pamoja na asasi za kiraia walichukuliwa dhamana
ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji kupitia taasisi zao.
Akizungumzia suala la utekelezaji sera ya
maendeleo ya vijana, Waziri Zainab alisema wizara yake imelenga kuwawezesha
vijana kwa kujiimarisha kiuchumi, kiutamaduni na kijamii.
Wakichangia hutuba ya wizara hiyo wajumbe wa
baraza la Wawakilishi walisema wizara hiyo licha ya kupiga hatua kimaendeleo
lakini inakabiliwa na changamoto ya kutokuwa na washine ya vya vipimo vya
vinasaba vya DNA.
Mwakilishi wa Muyuni, Jaku Hashim Ayoub alisema
haoni sababu ya wizara hiyo kushindwa kuwa na mashine hiyo wakati kesi nyingi
za udhalilishaji watoto hasa za ubakaji zinashindwa kufikiwa kwa kukosekana kwa
mashine hiyo.
Aidha waziri Zainab aliwataka wajumbe wa baraza
la wawakilishi kuijadili hutuba yake pamoja na kuwapa ushauri ikiwa ni pamoja
na maelekezo ili wapitishe makadirio na kuidhinisha jumla ya shilingi
2,409,000,000 zikiwa ni fedha za kazi za kawaida na ikiwemo mishahara.
Sambamba na shilingi 1,606,600,000 fedha za kazi
za maendeleo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013.
No comments:
Post a Comment