Na Himid Choko
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi,
Pandu Ameir Kificho amewahimiza Wajumbe wa baraza hilo kufuatilia
kwa makini hotuba zanazowasilishwa, sambamba na kukemea taabia ya baadhi ya wajumbe kuchelewa wakati
wa vikao ya baraza hilo.
Alisema hali hiyo inasababisha
wajumbe kukosa umakini wa kusikiliza na kufuatilia hotuba
zinazowasilishwa na hivyo, kushindwa kuchangia ipasavyo wakati wa mijadala ya vikao vya baraza.
Spika Kificho alikua
akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo kwaWajumbe wa Baraza la Wawakilishi
katika hoteli ya Coconut Tree Village Marumbi, Mkoa wa Kusini Unguja.
“Kuna mtindo unaojitokeza wakati Waziri anaanza kuwasilisha hoja yake
, ukumbi unakuwa mtupu, sasa njoo ikiwa
hakuna yule aliyesikiliza kwa makini,inapelekea
hoja hiyo kukosa wachangiaji hasa
mwanzoni wa mjadala wa hoja,” alisema.
Alisema ni vyema wajumbe wakawepo
muda wote wakati wa uwasilishaji wa hotuba ndani ya baraza hilo , kwani
kuwepo kwao kunasaidia kuwajengea uelewa mpana zaidi wa hoja inayowasilishwa.
Kuhusu jinsia, Spika Kificho amesema akinamama ni kundi muhimu katika
jamii hivyo mipango imara inahitajika wakati wa kupanga bajeti ya serikali.
Alieleza kutoridhika kwake na baadhi ya waajiri hasa makampuni binafsi ambao wamekuwa wakiwanyanyasa
wanawake katika ajira kutokana na maumbile yao.
Alisema maumbile ya akinamama yasitumike kama ni kigezo cha
kuwakosesha ajira badala yake waajiri
kwa wingi ili kulisaidia kundi hilo ambalo ndilo mara nyingi walezi wa
familia katika jamii.
Wakitoa mada kuhusiana na stadi za mawasiliano, Wahadhiri kutoka Chuo
Kikuu cha Taifa Cha Zanzibar (SUZA) Said
Khamis Juma na Haroun Maalim walisema tatizo kubwa linalowakabili wachangiaji
ni kupambanunua kati ya ukweli na dhana
kwa kushindwa kuthibitisha hoja zao
kwa kutumia taarifa halisi.
“Hata ukweli unaweza kukosa nguvu , unaweza usikubalike pale
panapokosekana hoja au taarifa za kuunga
mkono , badala yake watu wakahisi kuwa ni fikra ama mawazo ya mtu tu,” alisema
Haroun.
Hivyo Mhadhiri huyo aliwahimiza Wawakilishi hao kujenga hoja zao kwa kutumia takwimu, mifano
na nukuu wakati wa mijadala kwa lengo la
kuvuta ushawishi nakuaminika kwa hoja zao.
Nae ndugu Said Khamis Juma amewahimiza Wawakilishi hao kuzingatia
uteuzi wa maneno, kujiamini na kudhibiti jazba
hasa wakati wa vikao vya baraza.
Wakiwasilisha mada inayohusu
jinsia na masuala ya bajeti, wanaharakati wa jinsia, Asha Aboud na
Munira Hamoud wamesema ni muhimu kwa Wawakilishi kuibua hoja za masuala ya
jinsia katika sekta muhimu kwani zitasaidia wakati wa uaandaaji wa mipango na
ugawanaji wa rasilimali ziliopo katika kila sekta.
Walisema mapengo ya jinsia yanapoonekana katika kufanya upembuzi
yakinifu inasaidia pia kutambua mahitaji
ya wanawake na wanaume pamoja na makundi mengine katika sekta mbai mbali.
Mapema akitoa maelezo kuhusiana
na mafunzo hayo, Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Yahya Khamis Hamad alisema
afisi ya Baraza la Wawakilishi itaendelea na juhudi za kuwajenge uwezo Wajumbe
wa baraza hilo ili waweze kutekeleza vyema majukumu yao waliyokabidhiwa na
wananchi.
Mafunzo hayo ni mfululizo mafunzo yanayoandaliwa na afisi ya Baraza la
Wawakilishi kwa lengo la kuwajengea uwezo wajumbe wake chini ya ufadhili wa
shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)
katika mradi wake wa kusaidia mabunge LSP.
No comments:
Post a Comment