Na Ramadhan Makame
ZECO Yaagizwa Kuzifungia Tukuza Taasisi za Serikali
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha Uchumi na Mipango ya
Maendeleo, Omar Yussuf Mzee amelitaka shirika la umeme Zanzibar (ZECO),
kuzifungua mita za tukuza taasisi zote za serikali.
Alisema chini ya utaratibu huo, ambao utaliwezesha shirika hilo kupata fedha za kwa
wakati na kuepuka kukopwa, ni likaeupuka kufunga mita hizo kwenye taasisi nyeti
na zenye umuhimu mkubwa ikiwemo hospitali.
Waziri huyo alieleza hayo jana katika ukumbi wa Baraza la
Wawakilishi alipokuwa kijibu suali lililoulizwa na Mwakilishi wa nafasi za
Wanawake Salma Mussa Bilal.
Alisema kufungwa kwa mita hizo kutalifanya shirika hilo kutopata hasara inayotokana
na kutolipwa huduma za utoaji wa umeme kwa taasisi za serikali.
Katika suali lake la msingi Mwakilishi huyo alitaka kujua
mikakati ya iliyopo kwa taasisi za serikali kulipa madeni ya shirika la umeme
kutokana na huduma ya nishati hiyo inavyotumiwa katika taasisi hizo.
Alisema wizara pamoja na taasisi zote za serikali zinapaswa
kufahamu kwamba sheria ya fedha za umma ya mwaka 2005 inasisitiza wizara na
taasisi za serikali kutotumia huduma ya aina yeyote ile kwa njia ya mkopo.
Alisema wizara na taasisi za serikali zinapaswa kutumia
huduma kutokana na mpango kazi wa mwaka husika na kulipia huduma inazozipata
kutoka kwa taasisi nyengine ikiwemo umeme.
Alisema wizara fedha itahakikisha inazipatia fedha taasisi
za serikali kwa mujibu wa mpango kazi ili ziweze kukidhidhi na manunuzi ya
huduma ikiwemo ya umeme.
Hisa za Zanzibar BoT hazieleweki
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha Uchumi na Mipango ya
Maendeleo, Omar Yussuf Mzee amesema kuwa moja ya kero ya Muungano ambayo
haijapatiwa ufumbuzi ni usahihi wa hisa za Zanzibar
kwenye Benki Kuu ya Tanzania
(BoT).
Waziri huyo alieleza hayo jana katika ukumbi wa Baraza la
Wawakilishi alikuwa akijibu suali la nyongeza lililoulizwa na Mwakilishiwa
jimbo wa Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu.
Katika suali lake Mwakilishi huyo pamoja na mambo mengine alikataka
kujua usahihi wa hisa za Zanzibar
katika uanzishwaji wa benki hiyo.
Waziri huyo alifahamisha kuwa kero ya kutambuliwa kwa
usahihi wa hisa za Zanzibar
katika uanzishwaji wa BoT, bado haijapatiwa ufumbuzi na majadala wa mazungumzo
ya kero hiyo yanaendelea.
Katika hatua nyengine waziri huyo alisema kuwa muundo wa kiuongozi
katika benki hiyo hauna sura ya kimuungano.
Alisema mbali ya uongozi wa juu wa benki hiyo kuwa
unateuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, lakini pia nafasi za chini na za
utendaji hazina sura ya kimuungano.
Matemwe Kupatiwa Maji Safi, Salama
WIZARA ya Ardhi Makaazi Maji na Nishati, imesema kuwa
wananchi wa Matemwe wako mbioni kumaliziwa kero inayowakabili ya upatikanaji wa
maji safi na
salama.
Naibu waziri wa wizara hiyo, Mwadini Haji Makame alieleza
hayo jana katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi alipokuwa kijibu suali la
Mwakilishi wa Nafasi za Wanawake, Kazija Khamis Kona.
Katika suali lake Mwakilishi huyo alitaka kujua mipango iliyopo ambayo
itahakikisha wananchi wa Matemwe wanapatiwa ufumbuzi dhidi ya tatizo la maji safi na salama.
Naibu huyo alisema tatizo la maji katika eneo hilo litamalizika kutokana
na Mamlaka ya Maji (ZAWA), kuchimba kisima kipya ambacho kipo katika hatua za
mwisho za kumalizika na kutoa huduma.
Alisema kisima hicho kiko kwenye hatua za mwisho ikiwemo
kufungwa pampu hali ambayo kwa kiasi kikubwa itamaliza tatizo la maji katika
eneo hilo.
Naibu huyo alifahamisha kuwa suluhisho la kudumu la
matatizo ya maji kwa wananchi wa Matemwe litamalizika kabisa baada ya mradi
huyo unaofadhiliwa na AFDB kukamilika.
Alisema mbali ya Matemwe maradi huo utahudumia vijiji
vyengine vinne.
Barabara Mjini Kiuyu – Pengewani Hufanyiwa Matengenezo
NAIBU waziri wa Miundombinu na Mawasiliano, Issa Haji Ussi
amesema barabara ya Mjini Kiuyu – Pengewani imekuwa ikifanyiwa matengenezo kila
mwaka.
Naibu huyo alieleza hayo jana katika ukumbi wa Baraza la
Wawakilishi alipokuwa akijibu suali la Mwakilishi wa Nafasi za Wanawake, Viwe
Khamis Abdalla.
Katika suali lake la msingi, Mwakilishi huyo alitaka kujua
mpango ulipo wa ujenzi wa barabara hiyo ili kuwaondoshea kero ya usafiri
wananchi wa Mjini Kiuyu.
Naibu huyo alisema katika mwaka wa fedha uliomalizika
wizara iliweka kalvati mbili, ikiwa ni hatua ya kuiwezesha barabara hiyo
kupitika.
Aidha alisema kiasi cha shilingi milioni 4,106,000
zimetengwa kwa ajili ya kuifanyia matengenenzo barabara hiyo hasa kwenye sehemu
korofi.
Naibu huyo alifahamisha kuwa serikali itaifanyia
matengenezo ya mara kwa mara barabara hiyo ili iweze kutumiwa vyema na wananchi
wa Mjini Kiuyu.
No comments:
Post a Comment