Tunakutakia kazi yako iwe nyepesi na rahisi
Usafiri wa anga pia utafutiwe ufumbuzi
The International Airlines of Zanzibar (IAZA)
izaliwe
Na
Geofrey Kimbitikiri
Wazanzibari waishio nje ( wana diaspora) na ambao jamaa zao
walipoteza maisha yao na wengine kuathirika katika msiba wa kuzama boti ya MV Skagit wamejitokeza, kwa kumpa mkono wa hongera waziri
mpya wa Mawasiliano na Miundombinu Bw. Rashid Seif, pale walipopeleka barua
pepe kwa Wagagagigikoko News Network (WANENE).
"Tunampongeza Mhe Rashid Seif kwa
kuikubali kazi hii ngumu kwa moyo mkunjufu hasa kwa wakati huu mgumu. Sisi sote
Wazanzibari tunaoishi nje tunamtakia waziri mpya kila la kheri katika kazi yake
hii ngumu na Mola amsaidie ili iwe nyepesi na rahisi", walielezea Wazanzibari hao.
"Pamoja na hongera zetu tunamuomba
waziri Rashid Seif aangalie pia usafiri wa anga kwa umakini na kwa jicho la karibu
zaidi.
Tunajua baadhi ya ndege za charter zinazokuja Visiwani zinasajiliwa Bara, lakini madamu
wanatumia anga na uwanja wetu ni lazima utendaji wao wa kazi utizamwe vizuri
ili usije kutuathiri huko mbele", waliendelea Wazanzibari hao.
"Wengine tuliwahi kupanda charter
kuenda Dar ambayo kioo kilikuwa kimevunjika na upande wa ubao ulikuwa umepachikwa.
Hii ni hatari na hatujui ndege kama hii vipi iliruhusiwa kupaa angani.
Safety
equipments kwenye ndege na kwenye airport yetu ya Zanzibar pia ziangaliwe, ili
tuwe tayari kwa lolote lile", waliendelea Wazanzibari hao.
Walisisitiza tuliwahi kuona siku za nyuma yakifanyika mazoezi eneo la bandari (Malindi) kama kungelitokea ajali ( Drill) lakini hatujawahi kuona hata mara moja mazoezi ya aina hii kufanyika viwanja vyetu vya ndege ili kuangalia uwezo wetu na kasoro zetu kukabiliana na ajali za aina hii.
"Mhe Rashid, sisi Wazanzibari tuliopo
nje tupo nyuma yako na tupo tayari kununua hisa kama Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
itaanzisha kampuni ya Taifa ya ndege na kuanza japokuwa kwa ndege moja ya kuaminika
ili shida na usumbufu wa wananchi wanaosafiri kwa anga uondolewe pia.
Ahadi hii iliwahi kutolewa huko nyuma kwamba na Makamu wa kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad kwamba Zanzibar iwe na shirika lake la ndege.
Wenzetu
Ethiopian Airlines walianza kidogo kidogo hivi hivi na leo ni shirika la ndege
la Afrika ambalo wengi wa wanadiaspora huwa tunalitumia tunaposafiri kuja nyumbani na sehemu nyengine za dunia.
Japokuwa nia iwe ni kuwa na 'The International Airlines of Zanzibar (IAZA)' lakini tunaweza kuanza na ndege ndogo ambazo zitaruka kati ya
Unguja, Pemba na Tanzania Bara", walimalizia Wazanzibari hao kwenye barua
yao pepe.
Source: Wagagagigikoko News Network
(WANENE)
No comments:
Post a Comment