MADAKTARI na wauguzi katika hospitali Cottege ya Kivunge wilaya ya Kaskazini "A" Mkoa wa kaskazini Unguja wameingia lawamani baada ya kudaiwa kufanya uzembe uliosababisha kifo cha mtoto mchanga, ambaye inasemekana alifariki kabla ya kuzaliwa.
Hayo yameelezwa na mzee Daudi Pili Daudi
ambaye ni baba mzazi wa mgonjwa aliyefikishwa hospitali kwa ajili ya kujifungua
wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi
wa habari hizi huko nyumbani kwake Mkokotoni Kibaoni Mkoa wa Kaskazini
Unguja.
Alisema uzembe na dharau iliyowatawala
waguzi na madaktari wa hospitali hiyo katika wodi ya wazazi kumesababisha
kumpoteza maisha ya mtoto huyo ambaye yeye ni mjukuu wake, bila ya kuzingatia
na kujali kwamba wananchi wanahitaji kupewa huduma bora.
Akisimulia mkasa huo ulivyokuwa Daudi
alisema kuwa alimfikisha mtoto wake Anisha Daudi hospitalini hapo August 27,
majira ya saa 6:00 za usiku, mara tu baada ya kuuguwa hasa baada ya kuzingatia
kuwa mtoto huyo ni mimba yake ya kwanza hivyo amuwahishe kituo cha afya mapema
ili kwa lengo la kuepusha matatizo ambayo yangeweza kujitokeza.
Aidha alisema ilipofika siku ya pili mnamo
majira ya saa 5:00 asubuhi wakati huo aliikuta hali ya mtoto wake ikiwa mbaya
sana na aliamua kuwatafuta wauguzi ili waweze kumsaidia lakini alishindwa
kuwasiliana nao kwani hakujua wapi walipojichimbia wauguzi hao.
"Nilipomuona mtoto wangu anapiga kelele
akiita madaktari wamsaidie niliranda kila sehemu kuwatafuta lakini
ilishindikana sikuweza kuwajua walipo nikafika hadi maabara nikakutana na mtu
wa maabara nikamuelezea akawapigia simu, na hapo walichukuwa saa moja na nusu
hawakutokezea huku hali ya mtoto ikiendelea kuwa mbaya", alisema baba
mzazi.
Alisema kuwa jambo lililomshangaza kwa
wauguzi hao kudai shilingi elfu kumi za vifaa kwa ajili ya kujifungulia na
baada ya kutoa pesa hizo yeye hakuwaona kutoka kwenda kununua na alipohitaji
risiti yake waligoma kumpatia.
Sambamba na hayo alidai kuwa Agosti 29 majira ya saa 12:30 alifika hopitali kwa kumkaguwa mtoto wake na
akakuta hajapatiwa huduma yoyote hali ambayo ikamsababishia kulalamika kwa
muuguzi na hatimae akatakiwa kuondoka na mgonjwa wake akamtafutie haspitali
nyengine.
Kwa upande wake Daktari dhamana Dk. Tamimu
Hamad Said amekiri kuwepo kwa kesi hiyo ya kufariki kwa mtoto kabla ya kuzaliwa
hali ambayo alidai kuwa ni suala la
kawaida kutokea kwenye uzazi.
"Nimeikuta hiyo kesi ilitokezea mtoto
alifariki kabla ya kuzaliwa na baada ya kuzaliwa sco imeonesha"
0",kwa maana tayari mtoto huyo alikuwa amekufa tangu tumboni",alisema
Daktari huyo alikanusha madai ya baba huyo
kwamba waliweka kikao cha dharura, kwa vile jambo hilo kwao ni desturi kufanyika kikao cha asubuhi,
ili kutathimini taratibu za kazi, pia kutolewa chumba cha kuzalia na kupelekwa
wodini ni utaratibu wa kawaida na kila mzazi baada ya kujifunguwa.
Akizungumzia suala la mama mjamzito
kulalamika wakati anapokuwa akikaribia kujifungua alisema ni jambo la kawaida
hivyo hakuona kama polikuwepo na kitendo
cha kudharauliwa au kapuunzwa.
"Mtu akiwa na maumivu huachiwa aendelee
mpaka wakati unapofika wa kijifungua, na yeye amefanyiwa huduma zote baada ya
kufika hospitali"alisema.
Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi Tiba, Dk.
Mohamed Dahoma alikiri kupokea kwa taarifa hiyo kutoka kwa mlalamikaji na
hatuwa za kisheria zitachukuliwa baada ya kuthibitika kutokea kwa kosa hilo.
Kaimu huyo alisema kuwa serikali imeweka huduma
kwa wananchi hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kupatiwa huduma bora bila ya
kikwazo chochote hususan kinamama wajawazito.
"Taarifa hiyo imenifika muda sio mrefu
na tayari nimeshaanza kuifanyia kazi, nimewaita maofisa wangu waifatilie kwa
kina na ikithibitika hali hiyo imefanyika hatiwa zitafata na hasa linapoimngia suala la uzazi hakuna
kumfumbia macho atakae fanya uzembe wa makusudi", alisema.
No comments:
Post a Comment