Habari za Punde

Mahakamani kwa tuhuma za kutaka kumtorosha mtoto


Haji Nassor na Asha Abdallah, ZJMMC Pemba

KIJANA Khamis Ali Othuman (32) Mkaazi wa Muharitani Wilaya Chake chake Pemba, amepandishiwa katika kizimba cha Mahakama ya Wilaya hiyo kwa tuhuma za kumtorosha mtoto wa kiume (7) kwa lengo la kumuingilia kinyume na maumbile.

Akisomewa tuhuma hizo mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo Omar Hamza Mcha, na Mwendesha Mashitaka Gongo Shaaban Gongo, alidai kuwa Augosti, 19 mwaka huu, majira ya saa 11:00 jioni huko Skuli ya Michakaini  mtuhumiwa huyo, aligundulika akiwa na mtoto bila ya ruhusa ya wazazi wake.

 Mwendesha Mashitaka huyo alidai kuwa mtuhumiwa huyo alifanya kosa hilo ambalo ni kosa kwa mujibu kifungu 130 (b) cha sheria namba 6, ya mwaka 2004 ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 Aidha Mwendesha Mashitaka huyo alidai kuwa upelelezi wa kosa hilo bado huajakamilika na kuiomba Mahakama kulipangia siku nyengine ili  kuendelea kusilikizwa wakati ukiwa upelelezi umeshakamilika.

 Mapema mthumiwa huyo aliiomba Mahakama kupelekwa hospitali kutokana na afya yake kudhoofu siku hadi siku kutokana na kipigo alichadai kupata kutoka kwa Polisi jamii wakati alipokutwa katika eneo la tukio akiwa na mtoto huyo.
 Alidai kuwa kwa sasa hawezi kula vizuri kutokana na kutapika damu, hivyo hawezi kuishi rumande na kuomba apunguziwe muda wa kuweko huko badala ya wiki mbili iwe wiki moja na hasa kwa vile ni hivi karibuni alitoka jela.

 ‘’Mheshimiwa Hakimu, hali yangu mbaya sana, maana nimerudi jela hivi karibuni, hivyo kutokana na kipigo cha Polisi Jamii nilichokipata naomba nipewe dhamana na kupelekwa hospitali kwa matibabu’’, alidai Mtuhumiwa huyo.
 Hata hivyo Mtuhumiwa huyo ameomba kupatiwa dhamana, ombi ambalo lilipingwa na Mwendesha Mashitaka kwa madai kuwa, endapo mtuhumiwa atapewa dhamana anaweza kudhuriwa na walalamikaji wa shauri hilo kutokana na ukubwa wa kosa lenyewe.
 Hakimu wa Mahakama hiyo Omar Hamza Mcha aliagiza kupelekwa hosptali ili apatiwe matibabu na ameamuru mtuhumiwa huyo kurejeshwa rumande hadi Septemba 4, mwaka huu na kesi yeke itakapotajwa tena na siku hiyo dhamana yake itakuwa wazi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.