Na Haji Nassor, Pemba
ZAIDI ya shilingi 50 milioni zinahitajika ili kuwafidia wananchi kadhaa wa kijiji cha Tumbe
Wilaya ya Micheweni na Madungu Wilaya ya Chake chake Pemba, ambao walipatwa na
maafa ya kuunguliwa nyumba na mali zao.
Hayo yameelezwa
jana na Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed
Aboud Mohamed kwa wakati tofauti huko
Tumbe na Mdungu wakati alipokuwa akizungumza na majeruhi wa ajali hiyo.
Alisema kuwa tathimi
ya kujua fidia hiyo, imefanywa na maafisa wake wa kitengo cha Maafa kwa
kushirikiana na waathirika wenyewe, mara baada ya kutokezea ajali hiyo na
kitengo hicho kupata taarifa hiyo.
Alieleza kuwa
Serikali ilipokea taarifa hiyo kwa masikitiko na huzini kubwa kutokana na
wananchi hao kukumbwa na janga hilo
la kuunguliwa na moto nyumba zao.
‘’Kwakweli
Serikali ilipokea taarifa hii ya kuunguliwa moto kwa wananchi wa Tumbe na ile
ya Madungu na kuhuzunishwa kutokana na wananchi kukosa makaazi na kupoteza mali zao’’,alifafanua.
Hata hivyo
amewataka wananchi hao, kuwa na moyo wa ustahamilivu kutokana na kukumbwa na ajali hiyo na
Serikali inaangalia uwezekano wa kuwasaidia.
Mara baada ya
kuwafariji wananchi hao, alikabidhi jumla ya shilingi milion tano na laki moja
(1500, 000) kwa wananchi hao wa shehia za Tumbe na shehia ya Madungu ikiwa ni
ubani wa kutoka kwa Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein .
Alifafanua fedha hizo waliokabidhiwa sio fidia
ya maafa bali ni mkono wa pole kutoka kwa Rais na suala la fidia kwa sas
atalifikisha Serikali kuu ili kuwatafautia na zikipatikana kuwakabidhi.
‘’Tuelewane vizuri
hizi nilizokabidhi leo sio fidia bali ni mkono wa pole kutoka kwa rais wetu
mpendwa amenituma niwakabidhi za fidia inaenda kutafutwa ‘’,alizidi kufafanua
Katika hatua Waziri
Aboud alieleza kuwa, kwa sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
haina mfuko wala bajeti maalum kwa ajili ya maafa ingawa kwa sasa hilo liko katika hatua za
mwisho kuwepo.
Alifahamisha kuwa
muda mfupi ujao Afisi hiyo ya Makamu wa Pili wa rais inaandaa taratibu za
kufikisha tamko lakuanzishwa mfuko maalum wa kukabiliana na maafa pamoja na
kuandaa sera na sheria.
Nae Mkuu wa Mkoa
wa Kaskazini Pemba Dadi Faki Dadi aliwataka wananchi hao, kuwa wastahamilivu
kutokana na kukumbwa na janga hilo
na kuwataka wamuekee Muumba zaid.
‘’Msijefanya
lolote kutokana na kukumbwa janga hili, na badala yake mumuelekee Mwenyenzi
Muungu ili mjiombee dua ili lisitokezee tena’’,alifafanua Dadi.
Kwa upande wake
Mwakilishi wa Jimbo la Tumbe Rufai Said Rufai aliwataka wananchi wake kuwa
wastahamilivu kutokana na kukumbwa na janga hilo na kila mmoja limemgusa kutokana na
uzito wake.
Baadhi ya shehia
za Tumbe Wilaya ya Micheweni na Madungu Wilaya ya Chake chake walipatwa na
tatizo la kuunguliwa na moto nyumba zao ambapo kiasi ya nyumba 14 zilikumbwa na
mkasa huo.
No comments:
Post a Comment