Habari za Punde

Kuwanyang’nya mali wanawake baada ya kuachwa ni kuunawirsiha umaskini miongoni mwao

Migogoro ya ndoa bado kikwazo, watoto ndio waathirika wakubwa

Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Kisiwani Pemba Khalfan Amour Mohamed, akimsikiliza mama ambae jina halikupatikana matatizo yaliomkuba ili apatiwe msaada ya kisheria, katika siku maalum ya kuadhimisha siku ya msaada ya kisheria Duniani ambapo halfa hiyo ilifanyika  Skuli ya Sekondari Uweleni Mkoani Pemba (picha na Haji Nassor, Pemba)
Na Haji Nassor, Pemba 
TABIA ya wanawake kutelekezwa na kisha kunyang’nywa mali hasa baada ya kuachwa, imekuwa ni tatizo sugu hapa visiwani, licha ya taasisi mbali mbali kupigia kelele suala hilo.
 
Tabia hii ambayo mwishowe huwaweka mazingira magumu wanawake na watoto wetu, imekuwa ikifanyika bila ya aibu kwenye jamii zetu ambazo zinawasomi waliobobea wa kila nyanja na kila fani.
 
Kitabu kitakatifu cha Quran kimeleeza wazi kwamba ‘daima hawawi sawa kati ya aliesoma na asie soma’’ hili kwa haraka haraka ni rahisi kulitafisiri lakini vitendo vyake huchekeshwa kwa jamii yetu.
 
Wapo wanaume huoa kwa furaha, shangwe, ngoma, nderemo na vifijo vikiambatana na nyimbo na udi wa asumini, mwanamme akiamini kwamba kampata amtakae kwenye ndoa.
 

Sawa, lakini mbona kadri siku zikisongo mbele kuna vitendo vya ukatili na utelekezaji kwa mpendwa wako, tusemeje uliomuoa kwa mkataba kwamba akianza kupoteza uzuri wake umtenge na kumkosesha baadhi ya huduma, kama ni hivyo ,sio sahihi.
 
Leo tumekuwa tukishuhudia korja za kesi katika vyombo vya sheria ambazo zinahusiana na wanawake na watoto kutelekezwa na hasa baada ya mwanamme kutoa talaka.
 
Ukubwa wa tatizo untaisha hasa kwa vile wakosaji hawatiwi adabu kama wao wanavyowatekeleza wanawake na watoto na kuwaacha bila ya msaada wowote.
 
Kwa mfano Wilaya ya Chake chake Kisiwani Pemba, kwa mwaka 2011 kuliripotiwa kesi 18 ambazo zote zinahusiana na utelekezwaji wa wanawake na watoto, na kesi mbili (2) zilihusiana na kudai mahari.
 
Kesi sita (6) zilihusiana na kudai mali baada ya mwanaume kuchuma mali kisha kumtolea nje mwanamke ambae kama nilivoeleza awali alimumoa kwa udi na asumini.
 
Pia Wilaya ya Chake chake katika mwaka huo wa 2011 kulikua na kesi mbili (2) zinazohusiana na migogoro ya familia ingawa sulhu kwa kesi hizi ilipatikana na wanamue kuanza kupeleka huduma.
 
Matendo haya ni yale tu wanawake walioshindwa kuvumilia na kuamua kuyafikisha Wizarani, mbali ambayo hayakuripotiwa kwa sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuona aibu na haya.
 
Lakini suala la utelelezaji wa familia kwa wanaume pia kulikua na kesi nane (8), na sulhu nayo ikapatikana , ambapo kwa Wilaya Mkoani kulikua na migogoro miwili (2) ya ndao na ufumbuzi ilipatikana .
 
Kutokana na wanaume kuwatelekeza wake zao na watoto, Wizara ya Uastawi wa Jamii Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto imekua ikipokea shilingi 139,000/= toka kwa wanaume sita ambao walilalamikiwa Wizarani hapo.
 
‘Shilingi laki moja zaidi, kila mwezi tunakusanya na kuwakabidhi wanawake ambao walikuwa tayari wameshatelekezwa na waume zao kwa kutopatiwa huduma mbali mbali humibu’’,alisema Afisa Maendeleo ya Wanawake na Watoto Wilaya ya Chake chake Salma Khamis Haji alipokua akizungumza na mwandishi wa makala haya.
 
Afisa huyo alisema miongoni mwa sababu inayopelekea wanaume kuwatelekeza wanawake na watoto ni kusahau wajibu wao baada ya kufunga ndoa.
 
‘’Wanaume, wanaamua kuoa wakiwa hawajai thamani ya ndoa wala thamani ya mwanamke na watoto, hivyo ni mwepesi kuwatelekeza na kuwakatia huduma za lazima ‘’,alisema Salma.
 
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Wizara ya Ustawi wa Jamii Maendeleo ya vijana, Wanawake na Watoto Pemba, ilionyesha kulikuwa na makosa 51 ambayo yaliripotiwa kwa upande wa Mkoa wa Kusini Pemba.
 
Kati ya makosa hayo yamo ya udhalilishaji na utelekezaji wa wanawake na watoto, Wilaya ya Chake chake pekee ilibeba makosa 38 na 13 Wilaya ya Mkoani.
 
Kwa mfano kulikua na kesi ya kuwafungia ndani watoto wawili ,ambayo ilifikishwa kituo cha Polisi cha Chake chake Juni, 2011, (no CHC /PCR.136) ambayo baada ya wazazi kuaicha Serikali ililamikia, lakini kutokana na kukosa ushirikiano na wahusika, Julai, 17, ilifungwa na RCO Kusini Pemba.
 
Katibu wa Mtandao wa Polisi wanawake Kusini Pemba Sajenti Zuwena Hamad Ali, alisema baadhi ya wazazi wamekuwa wakishindwa kushirikiana  vyema na vyombo vya kisheria zinapotokezea kesi za aina hii.
 
‘’Sisi Dawati la wanawake na watoto na hata Jeshi la Polisi tumekuwa tujitahidi kuzifuatilia kesi za aina hii, lakini kesi ikianza kuwa nzuri mashahidi huingia mitini na kutuvunja moyo’’,alisema Sajent Zuwena.
 
Kadhi wa mahakama Wilaya ya Chake chake Daud Khamis Salum yeye alisema suala la wanawake kunyang’anywa mali baada ya kuacha lipo kwa kiwango kikubwa kutokana na wanake kutofahamu haki zao.
 
‘’Kitabu kitakatifu cha Qur-an ,kimeeleza wazi kwamba vi vyema wanawake wakapewa haki zao mara anapoaachwa ili iwe nusra katika maisha yake’’,alisema Kadhi huyo.
 
‘’Kitoka nyumba ‘sheikh’ ni lazima na ni wajibu kwa mwanamme kumpa alie kuwa mke wake, hata kama hakuchangia, ilimradi iwe umekichuma wakati ukiwa na mke tu……….wapewa chao’’,alisema huku akinukuu aya ya Qu-ran.
 
Kuna kesi 18 zizazohusiana na migogoro ya ndoa na wanawake na watoto kutelekezwa, ambapo ndoa hizo pia zimeshavunjwa na Mahakama ya Kadhi kwa mujibu wa sheria na mamla ilionayo.
 
Kadhi hakusita kueleza kuwa, wanawake na watoto waliotelekezwa moja kwa moja ni kesi 12, ambazo zimejumuisha watoto 30 na hatua za kisheria zilichukuliwa kwa mujibu wa taratibu.
 
Kwa upande wa shehia ya Msingini Wilaya ya Chake chake kulikuwa na kesi tatu (3) ambazo wanawake na watoto walitekezwa na waume ,kwa sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na uhamisho wa kikazi.
 
Mzee Juma Seif ni sheha wa shehia hiyo, alisema sababu kubwa inayofanya baadhi ya wanaume kuzitelekeza familia zao ni pamoja na kuoa zaidi ya wake wawili na kukosa kuelewa wajibu wao.
 
‘’Wapo wanaume ambao wakiongeza mke tu, hujaribu kuzitelekeza familia zao bila ya kujali athari zake’’,alifafanua sheha huyo.
 
Hata hivyo alisema kesi za aina hiyo haziripotiwi ipasavyo kutokana na wanawake kuogopa kuachwa na wanaume zao na kusemwa  na jamii husika.
 
Mkuu wa Wilaya ya Chake chake Mwanajuma Majid Abdallah alisema kesi za kuwatelekeza wanawake na Watoto na kuwakosesha mali naada ya kuachwa, hufanya na wanaume kutokana na kutowapendelea maendeleo.
 
Fatuma Sahibu Ali wa kijiji cha  Kilimahodi Wilya Chake chake  ambae alitelekezwa na mumewe, na kwa sasa amekuwa akichukua fedha Wizarani kutokana na kutopewa huduma za lazima na aliekuwa mumewe .
 
Kesi za wanawake na watoto kutelekezwa na kunyang’anywa mali haziripotiwi ipasavyo katika vyombo mbali mbali huku sababu ikitajwa kuwepo kwa mzunguruko wa taratibu za kufuatlia kesi hizo
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.