Habari za Punde

Fungua Dimba Ligi Daraja la pili Mkoani - Cossovo yaidabisha Maendeleo


WACHEZAJI wa klabu ya Cossovo ya Chumbageni, wakiwa katika furaha nono baada ya kujipitia goli la pili na ushindi, lililofungwa na Juma Mchunga Bakar, kwenye mchezo wa fungua dimba wa ligi daraja la pili Wilaya ya Mkoani, uliochezwa uwanja wa Aston Villa Wambaa ambapo katika mchezo huo, timu ya Cossovo iliwabugiza watani wao hao timu ya Maendeleo nayo ya Chumbageni kwa magoli 2-1 (picha na Haji Nassor, Pemba)
 
Na Haji Nassor, Pemba
HATIMAE ule ubishi uliokuwa umetawala, takriban wiki tatu zilizopita kwa timu za Cossovo na Maendeleo zinazoishi mtaa mmoja wa Chumbageni ambazo zinashiriki ligi daraja la pili Wilaya ya Mkoani, umemalizika jana baada ya timu ya  Cossovo kuwakoromea watani wao hao kwa 2-1.
 Katika mchezo huo wa fungua dimba uliopigwa uwanja wa Aston Villa Wambaa na kuhudhuriwa na mamia ya wapenda soka wakiwa pamoja na wanawake, ulinaza kwa kasi huku kila mmoja akitafuta njia ili aondoke na ushidi uwanja hapo.
 Cossovo ambapo kwa mara ya mwisho walipokutana na Maendeleo ililala kwa idadai kama hiyo ya magoli, jana hiyo iliakuwa ya mwanzo kuzichana nyavu za Maendeleo kwa kujipatia goli safi lililowekwa kimiani na Juma Mchunga Bakar dakika ya 20, baada kuunganishiwa jaro safi toka masharki mwa uwanja huo.

 Kuingia kwa goli hilo Maendeleo walikuja juu, na kuhamia mfululizi langoni mwa Cososovo kwa nia kusawazisha, lakini walijikuta wakipunguzwa nguvu baada ya Juma Mchunga tena, dakika ya 30 kuiandikia timu yake goli la pili lililodumu hadi mapunziko.
 Kipindi cha pili kilianza kwa mkosi kwa timu ya Cossovo, baada ya mshambuliaji wao hatari Mohamed Bakar (Ngasa), kulima kadi nyekundu na mwamuzi wa mchezo huo  Mwalimu Hussien ambapo hilo liliwapa faraja Maendeleo.
 Dakika 49 baada ya kufanya mabadiliko ya kumtoa Abdull-karim Omar na kumuingiza mkongwe Suleiman Ali, kuliamsha ari kwa wachezaji hao, hali ambayo ilisababisha kujipatia goli la kufutia machozi, lililowekwa kimiani kwa ufundi na Mohamed Abrhaman baada kuachia fataki zito.
 Kuingia kwa goli hilo, timu ya Maendeleo ilionekana kupata uhai na kusakata kambumbu vyema, lakini dakika 90 zikamalizika kwa Cossovo kutoroka na alama tatau muhimu, ambapo pia katika mchezo mwengine uliopigwa uwanja wa Mpikatanga timu ya Aston villa iliangukia pua kwa kuchupwa magoli 2-1 na News scard kutoka Mtambile.
Timu ya Cossovo itatupa katarata yeke tena Oktoba, 21 kwa kuumana na Aston Villa, kwenye uwanja wa Wambaa, huku kaka zao timu ya Maendeleo wakijaribu bahati yao tena siku hiyo hiyo uwanja wa Makombeni kwa kutibuana na Jiondeni .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.