Habari za Punde

Maskani mama ya CCM kisonge yachomwa moto



 Wafanyakazi wa Kikosi cha Zima Moto wakijitahidi kuuzima moto uliokuwa ukiwaka ndani ya Jengo la Maskani ya kisonge lililochomwa moto na watu wanaodaiwa ni wafuasi wa Sheikh Faridi wakisindikiza kuachiwa kwa Sheikh wao huyo ambae wanadhani amekamatwa na Polisi baada ya kutomuana kwa siku Nzima,Jeshi la Polisi limekanusha kumkamata Sheikh huyo na kuwaomba wananchi kushirikiana kumtafuta



 Tukio la kuchomwa Moto Maskani ya CCM Kisonge limesababisha pia mali na baadhi ya Vyombo vilivyokua hapo kuteketea kwa Moto kama inavyoonekana Vespa iliowekwa eneo hilo ambayo mmiliki wake hajajulikana ikiteketea.

Jeshi la Polisi lilionekana likifanya Doria katika sehemu hio ilikuweka hali ya Usalama.
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI -MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.