Habari za Punde

Matukio ya Hapa na Pale Mitaani Zenj.

 Mambo ya Dada Njoo Darajani hayo yakiwa yameshamiri kwa bidhaa mbalimbali  zikiwa zimewekwa katika henga kuvutia wateja na wapita nijia katika eneo hilo lilioko mkabala na Skuli ya Sekondari ya Vikokotoni ikiwa ukuta wa skuli hiyo ndio henga ya bidhaa hizo.
 Wanafunzi wa Skuli ya Msingi ya Kisiwandui wakiwa katika maeneo ya michezani  wakirudi majumbani baada ya kumaliza vipindi vya masomo kwa siku hiyo. mdau wewe unakumbuka ulivyokuwa na umri huu ulikuwa na mchezo mwingi na kuchelewa kurudi nyumbani kwa mchezo wa njia na wanafunzi wezako kama wilovyo wanafunzi hawa wakiwa katika mchezo wakati wakirudi majumbani.
Mfanyakazi wa Baraza la Manispa Zanzibar  akitunza usafi wa mazingira ya marikiti ya mbogamboga, ili kuweka eneo hilo safi, kwa wananchi wanaofika katika soko hilo kukuta  mazingira ya usafi wanapofata bidhaa katika soko hilo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.