Habari za Punde

Kificho:Watanzania wanastahiki sifa kufanikisha utoaji maoni ya katiba kwa amani


WATANZANIA wanastahili sifa kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa kuandaa mchakato wa maoni ya katiba mpya bila ya kuzuka migogoro ambayo ingeliweza kuleta uvunjifu wa amani.
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, aliyasema hayo jana wakati akizindua kitabu cha elimu ya katiba kwa wananchi wa Zanzibar , kilichoandaliwa na Baraza la Wawakilishi, kituo cha huduma ya sheria Zanzibar na Ubalozi wa Norway.


Spika Kificho alisema, mchakato wa mabadiliko ya katiba ya nchi umekuwa ukitekelezwa na nchi mbali mbali duniani lakini humalizia kwa migogoro mikubwa ya kuhatarisha amani.
Alisema hali hiyo inawezekana imetokana na mchakato huo kuasisiwa na wanachi wenyewe kwa kuiomba serikali yao kuandaa katiba mpya jambo ambalo lilikubaliwa.
Alisema kwa vile Baraza la wawakilishi ni chombo kinachosimamia wananchi kimeona haja ya kusaidia mchakato huo kwa kuwapatia elimu ya katiba waananchi ili waweze kutoa maoni yao.

 Alisema kitabu hicho ni muhimu kwani kitaweza kuwafanya wananchi kuyaelewa maeneo muhimu ya kuyafanyia kazi ili kuifanya Tanzania kupata katiba bora.
Aliupongeza Ubalozi wa Norway nchini Tanzania na kituo cha huduma cha sheria kwa kufanikisha kupatikana kwa kitabu hicho amabapo aliahidi baraza hilo kuendeleza ushirikaino na taasisi hizo.
Nae Balozi wa Norway nchini Tanzania , Ingunn Klepsvik, alisema suala la madailiko ya katiba nchini Tanzania ni moja ya jambo la msingi na elimu ndio njia pekee itakayowawezesha Watanzania kuwa na katiba bora.
Mapema Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya kituo cha huduma cha Sheria Zanzibar, Profesa Criss Peter Maina, alisema kituo hicho kimeweza kupata mafanikio mbali mbali ya utoaji elimu ya sheria katika majimbo 50 ya Unguja na Pemba.
Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Yahya Hamad, akitoa shukrani zake alisema kufanikiwa kwa mradi huo kwa kiasi kikubwa utaweza kuwasaidia wajumbe wa baraza hilo pamoja na wananchi wa Zanzibar .
Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Iddi, mabalozi waliopo Zanzibar  na watendaji wa serikali wakiwemo mawaziri na watendaji wa baraza la wawakilishi. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.