Na Mwandishi wetu
VURUGU kubwa
zimetokea jijini Mwanza kati ya polisi na waendesha bodaboda.
Vurugu hizo zilianzia
katika mtaa wa Mission barabara iendayo uwanja wa ndege wa Mwanza.
Ghasia hizo zimeibuka
baada ya polisi kuanzisha operesheni ya kuwasaka na kuwakamata waendesha
bodaboda wasio na leseni na helmeti.
Waendesha bodaboda
wanapiga operesheni hizo zinazofanyika nyakati za usiku ambapo bodaboda kadhaa
wamekamatwa.
Vurugu zilipozidi,
polisi walilazimika kutumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwatawanya
bodaboda hao ambao walikuwa wamefunga barabara ya kuelekea uwanja wa ndege kwa
kutumia mawe.
Watu walikuwa
wakikimbia ovyo kuwekwa moshi wa mabomu ambao ulihanikiza eneo lote la kuelekea
uwanja wa ndege.
Vurugu hizo
zilisababisha huduma za usafiri kusimama kwa takribani masaa mawili.
Kamanda wa polisi mkoani humo,
Arnest Mango alisema polisi itaendelea kukabiliana na boda boha hao na kamwe
hawawezi kuogopa.
Polisi imethibitisha
kuwakamata watu wanane watu wanane kuhusika na vurugu hizo.
Aidha askari polisi
wawili walijeruhiwa kwa mawe wakati wakikabiliana na waandamanaji hao.
No comments:
Post a Comment