Habari za Punde

Akutwa amekufa ufukweni


Na Bakar Mussa, Pemba
MTU mmoja alietajwa kwa jina la Faki Juma Faki (60) mkaazi wa Kangagani Wete, amekutwa amekufa  katika ufukwe wa bahari ya Mjini Kiuyu Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Yahya Rashid Bugi alisema marehemu   aliondoka kwake tarehe 23 mwezi huu majira ya saa moja asubuhi, kwenda kuvua uvuvi wa miguu na hakurudi tena hadi maiti yake ilipokutwa ufukweni.
Bugi, alieleza marehemu ambae alikuwa na maradhi ya kuanguka alipotea baharini ambapo watu wake wa karibu walimtafuta bila mafanikio.

Daktari Abdalla Omar Hassan, alieifanyia uchunguzi maiti, alisema kifo chake kimesababishwa na kunywa maji mengi.
Bugi aliwataka wavuvi kuacha tabia ya kwenda kuvua peke yao hasa wakati huu wa upepo.
Wakati huo huo nyumba moja ya Faki Juma Rashid (35) mkaazi wa Wingwi Mjananza, imeunguwa moto na kusababisha hasara kubwa ambayo thamani yake haijapatikana.
Kamanda Bugi, alithibitisha kutokea moto huo na kueleza chanzo cha moto huo ni mke wa Faki kusafisha jaa la nyumba yao na kuchoma moto takataka hizo zilizokuwa karibu na choo cha makuti na kusababisha moto kuripuka.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.