Habari za Punde

Mkutano wa dharura wa 26 wa baraza la mawaziri ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wamalizika


jamhuri ya muungano wa tanzania

WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MKUTANO WA 26 WA DHARURA WA BARAZA LA MAWAZIRI LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Mkutano wa 26 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki umekwisha leo jijini Arusha. Mkutano huo ambao ulianza kwa ngazi ya Wataalam tarehe 22-23 Aprili, 2013 na kufuatiwa na wa Makatibu Wakuu tarehe 24 Aprili, 2013 umepokea taarifa ya hatua zilizofikiwa katika majadiliano ya Itifaki ya Umoja wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo inatarajiwa kutiwa saini na Wakuu wa Nchi Wanachama katika Mkutano wao wa 15, mwezi Novemba, 2013.

Aidha, Mkutano ulijadili pia pendekezo la kuongeza wigo wa Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki. 

Vilevile, Baraza la Mawaziri limepokea na kujadili mapendekezo ya bajeti ya Jumuiya kwa mwaka 2013/14 na limeridhia mapendekezo ya bajeti ya Jumuiya kwa mwaka 2013/14 kuwa Dola za Marekani 117,238,966.

Mkutano huu umejadili pia hatua iliyofikiwa katika uandaaji  wa   Itifaki ya  Hadhi na Kinga kwa watumishi wa Jumuiya na Taasisi zake.

Imetolewa na 

KATIBU MKUU

WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.