·
Maafisa wa Serikali waombwa kuzipa ushirikiano
·
Wajumbe wahaha
uwenyeviti wa Kamati hizo.
·
Wenyeviti kujulikana wiki ijayo
·
Hamza kuongoza tena Kamati ya Afisi za viongozi.
Na
Himid Choko, BLW
Kamati za Kudumu za Baraza la
Wawakilishi zitaendelea na kazi zake za kawaida kuanzia Mei 13 hadi Mei 24 2013.
Katibu wa Baraza la wawakilishi la
Zanzibar, Yahya Khamis Hamad amesema
Kamati ya Kusimamia Afisi za
Viongozi Wakuu wa Kitaifa na Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala, Kamati ya Kuchunguza
na Kudhibiti Hesabu za Serikali
na Mashirika (PAC), pamoja na Kamati ya
Fedha , Biashara na Kilimo zitafanyakazi zake Unguja.
Aidha ndugu Hamad amezitaja Kamati zitakazofanya kazi zake Pemba
kua ni Kamati ya Ujenzi na Mawasiliano, Kamati
ya Maendeleo ya Wanawake na Ustawi wa Jamii pamoja na Kamati ya Mifugo, Utalii , Uwezeshaji na Habari.
Amesema Miongoni mwa kazi zitakazofanywa na Kamati hizo ni Uchaguzi wa Wenyeviti na Makamo wenyeviti wa Kamati hizo pamoja na Kufuatilia Utekelezaji wa Bajeti ya Kila Wizara na
taasisi zake kwa Kipindi cha Januari- Machi 2013.
Wakati huo huo katibu huyo wa za Baraza la Wawakilishi amewaomba maafisa na
watendaji wa kila wizara Wizara na
taasisi zao kutoa mashirikiano ya kutosha
kwa Kamati hizo ili kuweza kufanikisha vyema majukumu ya Kamati hizo .
Amesema Kamati hizo zimeundwa
kihalali kutafuta taarifa zitakazoliwezesha Baraza la Wawakilishi ambalo ndio
chombo chenye uwakilishi wa moja kwa
moja wa wananchi kuweza kusimamia vyema
utendaji wa shughuli za serikali.
“Kwa msingi huo , watendaji wa
Mawizara wana jukumu la kutoa taarifa sahihi
juu ya mambo wanayoyashughulikia katika utumishi wote wa umma ili
kuwawezesha wananchi kupitia wawakilishi
wao kujua mambo yanayofanywa kwenye Mawizara
ya serikali kwa maslahi yao” alisisitiza Katibu huyo wa Baraza la
Wawakilishi.
Amesema hiyo ndio dhana kubwa inayojenga wajibu wa Serikali na Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi kuhusiana na haki za Kamati.
Kwa mujibu wa kifungu cha 88 (d) cha
Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 Miongoni mwa kazi za Baraza la Wawakilishi ni
kuidhinisha na kusimamia mipango ya maendeleo ya Serikali katika njia ile ile ambayo Bajeti ya mwaka
inaidhinishwa.
Hata hivyo amesema
Kamati ya Viongozi Wakuu wa Kitaifa tayari imeShafanya Uchaguzi kwa Dharura Maalum na kumrejesha tena
Mheshimiwa Hamza Hassan Juma (Kwamtipura) kuendelea kuwa
Mweyekiti wa kamati hiyo.
Aidha
Kamati hiyo imemchagua Mheshimiwa
Saleh Nassor Juma (Wawi) kuwa Makamo mwenyekiti wa kamati hiyo.
Mapema Mwezi uliopita Spika
wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho
aliZIpanguwa Kamati za Kudumu za Baraza hilo na kuzipanga
upya .
Wajumbe hao wapya watazitumikia Kamati hizo
kuazia Mwezi Mei 2013 mpaka kuvunywa kwa Baraza hapo mwaka 2015.
Kwa
upande wa Kamati ya Kusimamia Afisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ni Hamza Hassan Juma (Kwamtipura), Subeit Khamis
Faki (Micheweni), Ali Mzee Ali ( Kuteuliwa) , Shadya Mohammed Suleiman ( Viti
Maalum), Makame Msimba Mbarouk (Kitope),
Saleh Nassor Juma (Wawi) na Ashura Sharif Ali (Viti Maalum).
Kwa
Upande wa Kamati ya Katiba , Sheria na Utawala ,
walioteuliwa ni Mansour Yussuf Himid ( Kiembe Samaki), Wanu Khafidh
Ameir (viti Maalum) , na Suleiman Hemed Khamis
(Konde). Wengine ni Abdullah Juma Abdullah (Chonga) , Bikame Yusuf Hamad
(Viti Maalum) na Nassor Salin Ali (Rahaleo). Kamati hii hapo kabla ilikua
ikiongozwa na Mwakilishi wa Mfenesini ALI Abdullah Ali.
Aidha
katika uteuzi huo Mwakilishi wa Mji
Mkongwe Ismail Jussa Ladhu amehamishwa
kutoka Kamati yake ya awali ya Katiba, Sheria na utawala na sasa anatumikia Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi . Wengine
walioteuliwa kuunda Kamati ya hii ni
Marina Joel Thomas ( Kuteuliwa), Mohamed Haji Khalid (Mtambile) , Hussein Ibrahim
Makungu (Bububu), Mahamoud Moh,d Mussa
(Kikwajuni) , Salma Mohammed Ali (Viti Maalum) na Mheshimiwa Panya Ali Abdullah
( Viti Maalum). Kamati hii ilikuwa ikkua ikiongozwa na Makame Mshimba Mbarouk
(Kitope)
Kwa
upande wa Kamati ya Maendeleo ya Wanawake na Ustawi wa Jamii ambayo ilikuwa ikiongozwa na Amina Idd
Mabrouk ( Viti Maalum ) sasa inaundwa na
Mgeni Hassan Juma ( Viti Maalum), Mwanaidi Kassim Mussa (Viti Maalum), Hassan
Hamad Omar (Kojani), Farida Amour
Mohammed ( Viti Maalum), Addi Mossi Kombo (Matemwe), Ali Salum Haji
(Kwahani) na Mohammed Mbwana Hamad (Chambani).
Aidha
katika uteuzi huu Mheshimiwa Spika amewabakisha
Omar Ali Sheikh (Chake Chake), Mbarouk Wadi Mtando (Mkwajuni), Shamsi
Vuai Nahodha (Mwanakwerekwe), Fatma Mbarouk Said (Amani) kuwa Wajumbe wa Kamati
ya Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za
Serikali na Mashirika (PAC). Wengine walioteuliwa katika Kamati hiyo ni Rafai
Said Rufai (Tumbe), Mwajuma Faki Mdachi (Viti Maalum) na Salma Mussa Bilal (Viti Maalum) na Salim
Abdullah Hamad (Mtambwe). Kamati hio ilikua ikiongozwa na Omar Ali Shehe.
Wanaounda Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo
ni pamoja na Salmin Awadh Salmin (Magomeni), , Hamad Masoud Hamad (Ole ), Viwe
Khamis Abdullah (Viti Maalum), Asha Abdu Haji (Viti Maalum), Hija Hassan Hija
(Kiwani) na Raya Suleiman Hamad ( Viti
Maalum), na Jaku Hashim Ayoub (Muyuni).
Katika
Kamati ya Mifugo, Utalii na Uwezeshaji na Habari walioteuliwa ni Asha Bakari Makame (Viti Maalum) ambae alikua
mwenyekiti wa Kamati hiyo hapo kabla, Mlinde Mabrouk Juma (Bumbwini) na Kazija
Khamis Kona ( Viti Maalum). Wengine ni Asaa Othman Said (Wete), Abdullah
Mohammed Ali (Mkoani), Amina Iddi
Mabrouk (Viti Maalum), Mussa Ali Hassan ( Viti Maalum) na Mohammedraza Hasanali
Dharamsi (Uzini).
Habari
kutoka ndani ya Baraza Wawakilishi
zinasema kwamba wajumbe wengi wamekuwa
wakihaha na kupiga kampeni za chini kwa chini huku wakionyesha nia ya kugombea
nafazi za uongozi wa Kamati hizo.
Wenyeviti
na Makamo wenyeviti wa Kamati zote watajulikana wiki ijayo baada ya kamati hizo
kufanya uchaguzi wa viongozi wao.
No comments:
Post a Comment