Habari za Punde

SMZ yachangia 30m/- waathirika wa bomu Arusha

Na Mwantanga Ame, Dodoma
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imetoa shilingi milioni 30  kuwafariji wananchi walioathirika na shambulizi la bomu lililotokea katika kanisa la Mt. Joseph Mfanyakazi mjini Arusha.
Akizungumza na gazeti hili, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif, alisema serikali imetoa  hundi ya kiasi hicho cha fedha kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha ikiwa ni  mchango wa SMZ katika tukio hilo.
Alisema serikali imeguswa kwa kiasi kikubwa na  tukio hilo na inaendelea kulaani tukio hilo la kinyama.

Alisema serikali inaamini tukio hilo ni la kigaidi na itahakikisha inashirikian na serikali ya Jamhuri ya Muungano kuwasaka wahusika wote ili kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Balozi Seif, mwanzoni mwa wiki hii alifnya ziara ya kuwakagua majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Mount Meru mjini  Arusha.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.