IDADI
ya watuhumiwa wa tukio la kuripua kanisa la Mt. Joseph Mfanyakazi mkoani
Arusha, imeongezeka hadi kufikia 12, kati yao majina tisa yametajwa na matatu
bado ni siri kwa ajili ya uchunguzi.
Aidha
jeshi la Polisi nchini kupitia Mkuu wa Polisi,(IGP) Saidi Mwema, wametangaza donge
nono la shilingi milioni 50 kwa mtu yoyote atakayefanikisha kufichua mtandao wa
kigaidi nchini.
Kauli
hiyo imetolewa na Kamanda wa polisi Mkoani Arusha, Liberatus Sabasi, wakati
akitoa taarifa juu ya hatua walizochukua tangu kutokea kwa mripuko wa bomu hilo
Mei 5 mwaka huu, majira ya saa 4.30, ambapo watu watatu walifariki dunia na 66
kujeruhiwa.
Kamanda
Sabasi aliwataja watuhumiwa tisa kuwa ni Victor Ambrose Kalisti (20) mkazi wa
kwa Mromboo Arusha, Joseph Yusuph Lomayani (18),George Bathoromeo Silayo (23)
mfanyabishara na mkazi wa Olasiti na Mohamed Sulemani Said (38) mkazi wa
Ilala Dar es Salaam ambae ndie mwenyeji
wao aliyewafuata kwa gari binafsi uwanja wa ndege Dar es Salaam na kuwachukua
hadi Arusha katika hoteli ya Aquline.
Wengine
ni Said Abdallah Said (28), Said Mohsen na Foud Saleem Ahmed (28) raia wa Falme za Kiarabu, Abdulaziz Mubarak
(30) raia wa Saudi Arabia na Jassini Mbarak (29) mkazi wa Bondeni Arusha.
Alisema
kuwa watuhumiwa hao bado wanaendelea na mahojiano na tayari jalada la mashtaka
yao limepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwa ajili ya maamuzi ya
kisheria.
Alisema
katika hatua za awali zinaonesha bomu hilo siyo la kienyeji na pia wageni hao
walikutwa na viza halali ya kukaa
nchini, kwa madai walikuja harusini.
“Watuhumiwa
hawa wa UAE tulipowahoji walidai wamekuja harusini, lakini tunaendelea nao,” alisema.
Aidha
alisema ulinzi umeimarishwa katika kanisa lilikotokea mripuko huo.
KWA KWELI NCHI IPO KTK WAKATI MGUMU!
ReplyDeleteMcha mwana kulia mwisho humnyea nyimbo za kuashiria ugaid na siasa chafu zimezoeleka hapa Tanzania ya kitufika mtumlilie nani?
ReplyDelete