Na
Mwandishi wetu
WAZIRI
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi amewaagiza Makamanda wa Polisi
Mikoa, Wilaya na Wakuu wa vituo nchini, kuwakamata na kuwafikisha mbele ya
vyombo vya sheria watu wote wanaotumia majukwaa ya dini kukashifu dini
nyengine.
Akinukuu
msemo wa Kiswahili kuwa ‘ukicheka na Kima utavuna mabuwa’, Dk. Nchimbi alisema
serikali haitacheka tena na watu wanaotaka kuitumbukiza Tanzania katika
migogoro ya kidini, na kusema yeyote atakaefanya hivyo sasa atakamatwa.
Aliwaonya
watendaji hao wa polisi kwamba watafukuzwa kazi, iwapo serikali itasikia kwenye
mkoa, wilaya au kituo kuna matukio hayo huku viongozi hao wakishindwa kuchukua
hatua.
“Tukisikia
kwenye eneo lako matukio haya yamefanyika bila ya kuchukua hatua, utakwenda na
maji, hatuwezi kucheka na watu wanaochochea chuki na kutaka kutugawa,”alionya
Dk. Nchimbi.
Aidha
aliwaonya watumiaji wa mitandao ya kijamii kujiepusha na lugha za chuki na
uchochezi huku akisisitiza kuwa serikali imekubaliana na taasisi husika kuanza
kuwakamata watu wanaotuma ujumbe mfupi wa simu (sms) unaochochea chuki.
Safi sana mkuu, lazma tuwape moyo wenzetu, maafa sio ya upande mmoja.. ni yetu sote!
ReplyDeleteMungu awape subra wafiwa na awasaidie majeruhi wapone haraka...kwa uwezo wake!
Kama kweli serikali imedhamiria kuleta amani ya kweli nchini waanze na kuufugia mtandao wa JAMII FORUM.
ReplyDeleteHuu ni mtandao wa CHADEMA ambao kazi yake kubwa ni kulaani, kudharau na kuwashambulia WAISLAMU kuwa hawana akili, hawakusoma ni magaidi, hawana ajira n.k.
Dharau za namna hii ndio zimetufanya tuanze kuhoji vigezo vitumikavyo ktk utowaji wa elimu, ajira mbali mbali pamoja na nafasi za uongozi hadi wengine wapate kiburi cha namna hii!
Leo lisha tota mh, unasema hayo?
ReplyDelete