Na
Rose Chapewa, Morogoro
JESHI
la polisi mkoani Morogoro linamshilikia Joyce Kodi (24) mkazi wa kijiji cha
Ngweranga, kilichopo Malinyi wilayani Ulanga kwa tuhuma za kujifungua mtoto wa
kike kisha kumfukia nyuma ya nyumba yake akiwa hai na kusababisha kifo chake.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, John
Laswai alisema mwanamke huyo alitenda kosa hilo Mei 7 mwaka huu majira ya saa
1: 30 asubuhi nyumbani kwake katika kijiji cha Ngweranga.
Alisema
alijifungua mtoto huyo akiwa hai, na katika hali isiyokuwa ya kawaida aliamua
kuchimba shimo nyuma ya nyumba yake kisha kumfukia na kusababisha kifo chake.
Alisema
polisi wanaendelea na uchunguzi, pamoja na madaktari kumfanyia uchunguzi wa
kiakili mwanamke huyo, na kwamba atafikishwa mahakamani wakati wowote mara
baada ya uchunguzi kukamilika.
Alisema
katika tukio jingine mtoto mwenye umri wa miaka mitatu aliyefahamika kwa jina
la Issa Bakari mkaazi wa Mafisa manispaa ya Morogoro alikufa baada ya kuzama
kwenye mto Ngerengere.
Kamanda
Laswai alisema tukio hilo lilitokea Mei 8 mwaka huu saa 3:45 asubuhi, kwenye
mto huo eneo la Mafisa na kwamba uchunguzi unaendelea zaidi.
Wakati
huo huo mpiga deba aliyefahamika kwa jina la Nelson Haule (31) mkazi wa Mtawala
mjini hapa alifariki akiwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro akipatiwa
matibabu baada ya kulazwa baada ya kuanguka ghafla.
Alisema
mpiga debe huyo alianguka ghafla katika eneo la Hamjuki, ambapo alikimbizwa
hospitali na Mei 5 majira saa 5 usiku alifariki dunia, uchunguzi unaendelea.
No comments:
Post a Comment