Habari za Punde

Kampeni ya Daladala kwa Watoto Yazinduliwa Zenj katika Juma la Siku ya Mtoto wa Afrika.

Mshereheshaji  Robert akihamasisha Wananchi katika kutowa maoni yao na jinsi ya kumlinda Mtoto na Unyanyasaji wa Kijinsia Zanzibar, wakati wa Kampeni ya Unyanyasaji wa Watoto Kijinsia, inayofanyika katika Kituo Kikuu cha Daladala Darajani.

Makonda wa Daladala Zenj wakifuatilia uzinduzi huo katika kituo kikuu cha daladala darajani wakimsikiliza mwananchi akichangia jinsi ya kumlinda mtoto na janga la unyanyasaji wakati wa kupanda daladala.
Wananchi wakifuatilia mijadala inayochangiwa na wananchi dhidi ya watoto.
Mwananchi akichangia katika uzinduzi huo wa Kampeni ya Kumlinda Mtoto na Unyanyasaji na Madhila anayoyapata, Uzinduzi huo umeandaliwa na Umoja wa Wanafunzi wa Zanzibar waliosoma Marekani.


2 comments:

  1. Mi nauliza hio ni Zanzibar Association au Tanzania Association ? Mbona kuna bendera ya tanzania na U.S

    Hivi kwa nini bendera ya zanzibar haitumiki ? Au shein ndo katoa kauli ?

    ReplyDelete
  2. Kama ikitumika wewe itakusaidia nini?
    Kule osifi ya viambulisho mazizini inatumika na na baadhi ya W'bari hadi hii leo hawajapewa vitambulisho.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.