Maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliofanyika katika viwanja vya Victoria Garden Zanzibar yalipambwa na burudani ya Utenzi utenzi uliosomwa na Vijana kutoka Urowa Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja Asha Silima (Kulia) na Khdija Abdalla
Wanakikundi wa Sanaa ya Ngoma kutoka chuo cha Mafunzo wakitumbuiza kwa ngoma ya Kibati katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliofanyika Kitaifa hapo katika Viwanja vya Victoria Garden Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Fatma Abdullhabib Fereji akizindua Sera ya Mazingira Kitaifa hapo katika Viwanja vya Victoria Garden Mnazi mmoja Mjini Zanzibar katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Fatma Abdullhabib Fereji akimkabidhi zawadiya pesa Taslim sh,3,00000/ ndugu Yustina Ezekiel kutoka skuli ya sekondari ya Kiembe samaki baada ya kushinda katika Debate ya kuzungumzia Mazingira katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliofanyika Kitaifa hapo katika Viwanja vya Victoria Garden Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Fatma Abdullhabib Fereji katikati akiwa katika Picha ya Pamoja na viongozi wa Idara ya Mazingira na Washindi wa mashindano mbali mbali yalioandaliwa na Idara ya Mazingira katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliofanyika Kitaifa hapo katika Viwanja vya Victoria Garden Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment