Habari za Punde

Hadithi ya leo (5)



Amesema Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi wasallam

: " من لم يدع قول الزور والعمل به والجهل فليس لله حاجة في أن يدع طعامه وشرابه " رواه البخاري ومسلم

‘Yule asieacha kuzungumza maneno maovu na huku akiyatenda kwa kughafilika au kutojua,  Allaah (Subhaanahu Wata’ala) hana haja na yeye kuacha chakula chake na kinywaji chake.’

Imepokewa na Bukhaari na Muslim

Kusema uongo, kuzua, kufitini, kutukana yote ni miongoni mwa mambo maovu yaliyokatazwa kwa aliyefunga.

Allaah Subhanahu Wata’ala ametuasa kuchunga ndimi zetu  na kututaka mawazo yetu yaelekee kwenye kuikamilisha funga kwani funga si kuacha kula na kunywa peke yake pamoja na kustarehe bali pia ni kujizuia na maovu na maasi mengine.

Ewe Mola tujaalie siku tunayofunga iwe tofauti kabisa na siku tusiyofunga ili tuweze kuikamilisha funga yako tukitaraji malipo yako uliyotuahidi.

Aamiyn Aamiyn

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.