Habari za Punde

Bajeti ya Wizara ya elimu


 
 
 
 
 
 


HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI.
 
 
 
 
 
MHESHIMIWA ALI JUMA SHAMUHUNA
 
 
 
 
 
KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014

 


YALIYOMO
UTANGULIZI..........................................................
1
MAFANIKIO YALIYOPATIKANA KATIKA MWAKA 2012/2013...............................................................................
 
4
Mpango kazi wa Elimu....................................................... ...
7
IDARA YA SERA, MIPANGO NA UTAFITI......................
9
Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa Mwaka 2012/2013................................................................................
 
9
Mradi wa Upanuzi na Uimarishaji wa Huduma za Maktaba.
10
Mradi wa Uimarishaji wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar..................................................................................
 
10
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi...........................
11
Mradi wa Ujenzi wa Vyuo vya Kiislam ................................
14
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Mbadala na Amali.......................................................................................
 
14
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima...........................
17
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Ufundi............................
19
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi.....................
20
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi kwa Wilaya ya Magharibi................................................................................
 
22
Mradi wa Sayansi na Technolojia...........................................
22
Mpango wa Maendeleo kwa Mwaka 2013/2014....................
23
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi.....................
23
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Msingi................................
24
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi kwa Wilaya ya Magharibi................................................................................
 
25
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima...........................
26
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Ufundi............................
27
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Mbadala na Amali.......................................................................................
 
27
Mradi wa Uimarishaji wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar..................................................................................
 
28
Mradi wa Upanuzi na Uimarishaji wa Huduma za Maktaba..................................................................................
 
28
Mradi wa Ujenzi wa Vyuo vya Kiislam.................................
29
Utafiti.....................................................................................
29
Ukusanyaji na Uchambuzi wa Taarifa za Elimu....................
30
Maendeleo ya Kisera..............................................................
30
Ufuatiliaji na Tathmini...........................................................
31
IDARA YA UENDESHAJI NA UTUMISHI........................
31
IDARA YA ELIMU YA MAANDALIZI NA MSINGI........
34
Elimu ya Madrasa na Vyuo vya Kuran..................................
35
Elimu ya Maandalizi..............................................................
35
Elimu ya Msingi…………………………………………….
36
IDARA YA ELIMU YA SEKONDARI.................................
39
Kazi za Ujasiriamali...............................................................
40
Serikali za Wanafunzi............................................................
40
Huduma za Dakhalia..............................................................
41
IDARA YA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO KATIKA ELIMU.....................................
 
41
Sera ya ICT katika Elimu na Mpango Mkakati wake.............
42
Utekelezaji wa Mradi wa TZ-21 Century Basic Education.................................................................................
 
42
Kuimarisha Njia za Mawasiliano na Usambazaji wa Taarifa kupitia TEKNOHAMA...........................................................
 
42
Kuimarisha Elimu ya Maandalizi kwa Kutumia Vifaa vya ICT..........................................................................................
 
43
IDARA YA ELIMU MBADALA NA WATU WAZIMA................................................................................
 
44
Kisomo ...................................................................................
44
Vituo vya Kujiendeleza..........................................................
45
Vyombo vya Habari................................................................
46
IDARA YA MAFUNZO YA UALIMU.................................
47
Mafunzo ya Ualimu Kazini.....................................................
48
OFISI YA MKAGUZI MKUU WA ELIMU..........................
51
TAASISI YA ELIMU ZANZIBAR........................................
52
MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI...........................
54
TAASISI YA ELIMU YA JUU..............................................
56
CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR...................
56
TAASISI YA KARUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA........................................................................
 
59
CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR.........................................
61
CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU CHUKWANI.....
61
BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU............................
62
BARAZA LA MITIHANI LA ZANZIBAR...........................
64
BODI YA HUDUMA ZA MAKTABA..................................
66
KITENGO CHA UHASIBU...................................................
68
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO....................................................................
 
68
KITENGO CHA UNUNUZI NA UGAVI..............................
70
KITENGO CHA UKAGUZI WA HESABU ZA NDANI.....
71
KITENGO CHA URATIBU WA ELIMU YA JUU..............
72
KITENGO CHA ELIMU MJUMUISHO NA STADI ZA MAISHA ………………………………................................
 
73
Elimu Mjumuisho...................................................................
73
Ushauri Nasaha.......................................................................
75
Mapambano dhidi ya Ukimwi na Madawa ya Kulevya.........
75
Masuala ya Jinsia...................................................................
75
KITENGO CHA URAJISI.....................................................
76
Baraza la Elimu......................................................................
76
Leseni za Walimu...................................................................
77
Maombi ya Usajili wa Skuli za Serikali na Binafsi................
77
Kesi za Ujauzito na Ndoa za Wanafunzi...............................
77
KITENGO CHA MICHEZO NA UTAMADUNI..................
78
MAPATO................................................................................
80
SHUKRANI............................................................................
81
JUMLA YA GHARAMA ZA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI........................................................
 
81
KIAMBATISHO....................................................................
83
 


 

 

HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014

 

UTANGULIZI

1.            Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Baraza lako Tukufu sasa liingie katika Kamati ili niweze kutoa maelezo ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka wa fedha 2013/2014.

 

 

2.            Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana kwa mara nyengine tena katika kikao cha Bajeti cha Baraza lako tukufu tukiwa wenye afya njema na wazima na kuniwezesha kuwasilisha hotuba hii. 

 

3.            Mheshimiwa Spika, pili, naomba kuchukua fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Seif Sharrif Hamad, Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar na Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa mafanikio makubwa yaliopatikana katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya awamu ya saba yenye muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Nawashukuru sana kwa maelekezo, ushauri na ushirikiano mkubwa wanaonipa ambao umeniwezesha kutekeleza majukumu niliyokabidhiwa katika sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa letu.

 

4.            Mheshimiwa Spika, pia, ninakupongeza kwa umahiri na uwezo mkubwa unaouonesha katika kuliongoza Baraza lako tukufu kwa misingi ya uadilifu na uaminifu mkubwa na hatimaye kutufikisha katika kikao hichi cha tatu cha bajeti. Vile vile napenda kumpongeza Mheshimiwa Ali Abdulla Ali Naibu Spika wa Baraza na Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini kwa kukusaidia katika kuliongoza Baraza letu. Pia napenda kuwapongeza Waheshimiwa Wenyeviti wa Baraza Mheshimiwa Mgeni Hassan Juma na Mheshimiwa Mahmoud Mohammed Mussa kwa uongozi wao kwa Baraza. Aidha, napenda kuwapongeza Waheshimiwa Wenyeviti na Makamu wenyeviti wa Kamati za Baraza la Wawakilishi na wajumbe wote walioteuliwa hivi karibuni katika kamati mbali mbali za Baraza lako tukufu. Vile vile napenda kumpongeza Mheshimiwa Hussein Ibrahim Makungu kwa kuchaguliwa kwake kuwa muwakilishi wa jimbo la Bububu kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi.

 

5.            Mheshimiwa Spika, napenda kuipongeza na kuishukuru Kamati ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Wanawake ya Baraza la Wawakilishi ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mheshimiwa Mgeni Hassan Juma kwa kutuongoza vyema na kutushauri ipasavyo. Wajumbe wa Kamati hii waliweza kuichambua na kujadili hotuba ya bajeti kwa undani kabisa na mwishowe kuipitisha.  Pia, ameweza kuishauri Wizara ipasavyo kila walipotembelea shughuli tunazozisimamia.

 

 

6.            Mheshimiwa Spika, shukrani zangu pia ziende kwa Waheshimiwa wajumbe wote wa Baraza lako Tukufu kwa namna walivyokuwa karibu na wizara yangu katika kushajiisha wananchi wa maeneo yao katika kusukuma mbele shughuli za kielimu.

 

7.            Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee, napenda kumshukuru kwa dhati msaidizi wangu, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Mheshimiwa Zahra Ali Hamad kwa juhudi zake, mashirikiano anayonipa katika kutekeleza majukumu tuliopewa na Taifa.  Aidha napenda kuwapongeza watendaji wakuu na wafanyakazi wote wa Wizara yangu wakiwemo Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Kamishna, Wakurugenzi, maafisa wa ngazi mbali mbali za elimu, walimu na wafanyakazi wengineo wote wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kufanya kazi kwa nidhamu, bidii na ushirikiano, hali ambayo imeniwezesha kuwasilisha hotuba hii mbele ya Baraza lako Tukufu.

 

8.            Mheshimiwa Spika,

Vile vile napenda kuwashukuru kwa dhati wananchi wa Jimbo la Donge kwa kunipa ushirikiano mkubwa katika kutimiza majukumu yangu nikiwa Mwakilishi wao.

 

9.            Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kuishukuru kwa dhati kabisa Ofisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo kwa ushirikiano mkubwa uliotupa mwaka 2012/2013. Kwa ujumla upatikanaji wa fedha ulikuwa ni wa kuridhisha kwani hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013 jumla ya T.Sh. 3,016,700,000/- zilipatikana kwa ajili ya utekelezaji wa kazi za maendeleo ikiwa ni sawa na asilimia 59.2 ya makadirio. Kwa upande wa kazi za kawaida, jumla ya T.Sh. 67,691,445,910/- zilipatikana ikiwa ni sawa na asilimia 95.3 ya makadirio. Jadweli namba 10 (a) na (b) zinatoa uchambuzi zaidi. Ni matumaini yangu kwamba ushirikiano huu utaendelezwa na kudumishwa. 

 

10.         Mheshimiwa Spika, kabla ya kuelezea utekelezaji wa shughuli za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kipindi cha mwaka 2012/2013, naomba uniruhusu nieleze kwa ufupi mafanikio yaliyopatikana katika Wizara hii kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

 

MAFANIKIO YALIYOPATIKANA KATIKA MWAKA 2012/2013

 

11.         Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imepata mafanikio makubwa katika sekta ya elimu kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.  Miongoni mwa mafanikio hayo ni :-

 

·         Wizara imesaini hati ya maelewano na Wizara ya Elimu ya Juu ya Falme ya Oman juu ya ushirikiano katika ngazi ya elimu ya juu. Kupitia maelewano hayo Serikali ya Falme ya Oman imeanzisha Mpango wa kuwagharimia masomo ya juu wanafunzi wetu kwa kupitia Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar. Mpango huo unaoitwa “Sultan Qaboos Academic Fellowship for SUZA” (SQF) umeanza kufanya kazi kwani nafasi za masomo ya juu zimetangazwa na vijana mbali mbali wameomba nafasi za udhamini wa masomo katika ngazi ya shahada ya kwanza, shahada ya uzamili na shahada ya uzamivu.

 

·         Idadi ya wanafunzi waliogharimiwa masomo kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ya Zanzibar iliongezeka kutoka wanafunzi 1,086 mwaka 2011/2012 hadi wanafunzi 1,897 mwaka 2012/2013.

 

·         Walimu wapya 578 waliajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi.

 

·         Ujenzi wa skuli mpya za sekondari 13 kati ya 16 umekamilika. Skuli hizo ni Mwanda, Chaani, Matemwe, Uzini na Dole kwa Unguja na Utaani, Ngwachani, Wawi, Kiwani-mauani, Tumbe, Konde, Pandani na Madungu kwa Pemba. Skuli hizi zote zimekamilika na kuanza kutumika

 

·         Ujenzi wa skuli mpya za sekondari za ghorofa katika maeneo ya Kiembesamaki, Kwamtipura, Mpendae (ufadhili wa Benki ya Dunia) Kibuteni na Mkanyageni (ufadhili wa Badea) unaendelea.

 

·         Ukarabati wa skuli za sekondari za Forodhani na Tumekuja kwa Unguja na Utaani na Fidel Castro kwa Pemba umekamilika na skuli hizo hivi sasa zinatumika. Ukarabati wa skuli za sekondari za Hamamni kwa Unguja na Uweleni kwa Pemba unaendelea na uko katika hatua za mwisho.

 

·         Awamu ya pili ya ujenzi wa kampasi ya Chuo cha Ualimu cha Benjamin William Mkapa huko Mchangamdogo, Pemba imekamilika.

 

·         Ujenzi wa skuli mpya ya msingi ya kisasa iliyofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China hapo Mwanakwerekwe imekamilika na kukabidhiwa rasmi.

 

·         Vifaa mbali mbali vya teknolojia ya habari na mawasiliano zikiwemo kompyuta vimefungwa na kusambazwa katika skuli 74 za msingi kupitia mradi wa TZ-21. Kazi ya kufunga na kusambaza inaendelea katika skuli zilizobakia.

 

·         Matokeo ya mtihani kidato cha pili yalikuwa mazuri ambapo kati ya wanafunzi 19,679 (wanawake 11,045 na wanaume 8,644) wa skuli za sekondari za Serikali walifanya mtihani huo mwezi wa Novemba 2012, wanafunzi 11,195 (wanawake 6,768 na wanaume 4,427) wamefaulu na kuchaguliwa kuingia kidato cha tatu mwaka 2013. Idadi hii ni sawa na asilimia 56.9 ya waliofanya mtihani huo. Kiwango hiki cha ufaulu kimepanda kwa asilimia 0.8 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2011.

 

·         Shirika la “Global Partnership for Education (GPE)” lenye makao makuu yake mjini Washington limeidhinisha msaada wa dola za Kimarekani millioni 5.2 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango kazi wa elimu wa Zanzibar kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2013/2014 hadi 2015/2016. Fedha hizo zitatumika katika kuinua ubora wa elimu yetu katika ngazi ya maandalizi na msingi.

 

·         Vipando 230 vimenunuliwa na SACCOS za Elimu, Unguja na Pemba kwa ajili ya kuwakopesha walimu.

 

 

Mpango Kazi wa Elimu

 

12.         Mheshimiwa Spika, Wizara imeandaa mpango kazi wa maendeleo ya elimu kwa kipindi cha miaka minne ya mwisho, kuanzia mwaka 2012/2013 hadi 2015/2016. Mpango kazi huo umezingatia Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020, Awamu ya Pili ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUZA II), na ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2010 hadi 2015. Mpango kazi huo unatoa mwongozo wa njia ya kufikiwa kwa malengo ya Elimu kwa Wote na Malengo ya Milenia kwa upande wa elimu ifikapo mwaka 2015. Shabaha za mpango kazi huo ifikapo mwaka 2016 ni kama hivi ifuatavyo:

·         Uandikishaji safi (NER) wa wanafunzi katika ngazi ya elimu ya maandalizi ifikie asilimia 30.

·         Uandikishaji safi (NER) wa wanafunzi katika ngazi ya elimu ya msingi ifikie asilimia 95.

·         Idadi ya wanafunzi kwa darasa ipunguwe hadi wanafunzi 40 kwa darasa.

·         Asilimia ya wanafunzi wanaofanya mtihani wa Kidato cha Pili na kufaulu na kuchaguliwa kuendelea na masomo ya Kidato cha tatu ifikie asilimia 70. Pia zaidi ya asilimia 50 ya wanafunzi wote wanaoandikishwa kufanya mtihani wa kuingilia Kidato cha tatu waweza kufaulu katika masomo ya Kiingereza, Hisabati, Biolojia, Kemia na Fizikia.

·         Asilimia ya wanafunzi wa kidato cha nne wanaofaulu na kupata sifa za kuendelea na masomo ya kuingia kidato cha tano iongezeke hadi kufikia asilimia 20 ya wanafunzi wote walioandikishwa kufanya mtihani.

·         Idadi ya wanafunzi wanaojiunga na taasisi za  elimu ya juu, iongezeke na kufikia asilimia 20 ya wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita.

·         Asilimia 50 ya waombaji wa mkopo wa elimu ya juu waweze kupatiwa mikopo ya kusoma katika taasisi za elimu ya juu.

·         Wanafunzi wote wa msingi wapatiwe vitabu vyote vya kiada;

·         Wanafunzi wote wenye mahitaji maalum waweze kupatiwa vifaa maalumu kwa ajili ya kusomea na kujifunzia na kuweza kusoma katika mazingira rafiki;

·         Vituo vya elimu ya watu wazima vitowe elimu ya watu wazima kwa mujibu wa mahitaji ya soko la ajira;

·         Walimu wote wa msingi na sekondari wawe wamefuzu mafunzo ya ualimu.

·         Uongozi na usimamizi wa elimu uweze kuimarishwa katika ngazi zote;

·         Skuli zote za msingi na sekondari ziweze kufanyiwa ukaguzi kila mwaka;

·         Miundo mbinu ya Taasisi za elimu ya juu iweze kuimarishwa; na

·         Kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu ya ufundi na mafunzo ya amali.

 

13.         Mheshimiwa Spika, mpango kazi unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, mashirika yasio ya kiserikali, wahisani mbali mbali pamoja na wananchi wote kwa jumla. Baadhi ya shabaha za mpango kazi huu yanatekelezwa kupitia miradi mbali mbali iliyomo katika mipango ya maendeleo na bajeti yetu ya kazi za kawaida.

 

14.         Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, sasa naomba uniruhusu nieleze kuhusu shughuli mbali mbali zilizotekelezwa katika Idara moja moja na taasisi zinazojitegemea katika mwaka 2012/2013 na matarajio na malengo kwa mwaka 2013/2014.

 

IDARA YA SERA, MIPANGO NA UTAFITI

15.         Mheshimiwa Spika, Idara ya Sera, Mipango na Utafiti ina majukumu ya kuandaa mipango ya maendeleo, kuratibu na kufuatilia raslimali na misaada mbali mbali ya wahisani, kusimamia, kufanya mapitio ya tathmini ya sera, mipango programu na miradi mbali mbali inayotekelezwa na Wizara, kuratibu shughuli za utafiti wa kielimu na kusimamia ukusanyaji, uchambuzi na uwasilishaji wa takwimu mbali mbali za kielimu.

 

Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa Mwaka 2012/2013

16.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Wizara ilipanga kutekeleza jumla ya miradi kumi ya maendeleo. Miradi hiyo ilitengewa jumla ya T.Sh. 38,969,291,000/-, kati ya fedha hizo T.Sh.5,100,000,000/- ni za mchango wa SMZ, T.Sh. 3,208,315,000/- ni ruzuku kutoka kwa wahisani mbali mbali wa maendeleo na T.Sh. 30,660,976,000/- ni mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) na Benki ya Dunia. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 2,614,700,000/= za SMZ zilipatikana ikiwa ni sawa na asilimia 59.2 ya makadirio. Kwa upande wa washirika wa maendeleo, fedha zilizopatikana ni T.Sh. 28,559,603,224.68 sawa na asilimia 84.3 ya makadirio.

 

          Utekelezaji halisi wa miradi hiyo ni kama ifuatavyo:-

Mradi wa Upanuzi na Uimarishaji wa Huduma za Maktaba

17.         Mheshimiwa Spika, mradi ulipangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 200,000,000/= kwa ajili ya kutangaza zabuni ya ujenzi wa tawi la Maktaba Kuu Pemba, kumchagua mkandarasi, kujenga msingi wa jengo jipya na kufanya ukarabati wa jengo la Maktaba liliopo. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 55,000,000/= zilipatikana ikiwa ni sawa na asilimia 27.5 ya makadirio.  Kazi zilizofanyika ni kumchagua mkandarasi na kutiliana saini mkataba wa ujenzi.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.

18.         Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa na SMZ kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) na ulikuwa na malengo yafuatayo:-

 

(i)           Kufunga vifaa vya ICT na vipoza hewa katika majengo mawili.

 

(ii)          Kuweka miundombinu kwa ajili ya mawasiliano ya simu na “Internet”.

 

(iii)        Kununua vifaa vya kufundishia kwa ajili ya Kitivo cha Uhandisi.

 

(iv)        Kukamilisha kazi za ujenzi na kusambaza miundo mbinu ya umeme.

 

(v)          Kuanza kutumiwa kwa majengo.

 

Mradi huu ulipangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 1,725,000,000/- za SMZ na T.Sh.4, 332,959,000/- za BADEA.  Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013 jumla ya T.Sh. 1,659,700,000/- za SMZ sawa na asilimia 96.2 ya makadirio zilipatikana. Aidha, kwa upande wa BADEA, T.Sh. 594,833,392/= zilipatikana ikiwa sawa na asilimia 13.7 ya makadirio. Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo:-

 

i)             Vifaa vya ICT na vipoza hewa vimenunuliwa na vimefungwa.

 

ii)            Miundo mbinu kwa ajili ya mawasiliano ya simu na “Internet” imewekwa. Kampasi ya Tunguu imeunganishwa na huduma za Intenet.

 

iii)          Ujenzi wa majengo ya SUZA huko Tunguu umekamilika pamoja na miundo mbinu ya umeme. Majengo mapya ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar yaliyopo Tunguu yalihamiwa mwezi wa Oktoba mwaka wa 2012 na kuanza kutumika rasmi.

 

iv)          Baadhi ya vifaa vya maabara vimepatikana.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi

19.       Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya wananchi, SMZ, Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, Sida, UNICEF, UNESCO na USAID.  Mradi ulitengewa jumla ya T.Sh.800,000,000/- za SMZ na T.Sh. 3,045,061,000/- kutoka Sida, UNESCO na UNICEF na ulikuwa na malengo yafuatayo:-

(i)           Kukamilisha ujenzi wa madarasa 150 kwa kushirikiana na wananchi katika Wilaya tisa za Unguja na Pemba.

(ii)          Kufanya ukarabati katika skuli 15 za msingi.

(iii)        Kuchonga madawati 2,250 na kuyasambaza katika madarasa mapya yaliyojengwa.

(iv)        Kuwapatia walimu mafunzo mbali mbali yakiwemo ya matumizi ya lugha ya Kiingereza kwa ajili ya kufundishia, mafunzo juu ya matumizi ya mtaala mpya wa ngazi ya msingi na mafunzo ya kufundisha katika mfumo wa elimu mjumuisho.

(v)          Kukamilisha ujenzi wa nyumba tatu za walimu.

(vi)        Kuendeleza ujenzi wa skuli moja ya msingi katika eneo la Mwanakwerekwe.

(vii)       Kutoa mafunzo kwa walimu na kamati za skuli juu ya kuimarisha huduma za maji, afya na mazingira katika skuli.

(viii)      Kuendelea na utekelezaji wa mradi wa TZ-21.

 

Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 407,000,000/- za SMZ zilipatikana sawa na asilimia 51 ya makadirio. Kwa upande wa Sida, UNICEF na UNESCO fedha zilizotolewa ni T.Sh. 4,643,963,511.78/- sawa na asilimia 149 ya makadirio. Hii imetokana na kupatikana fedha nyingi zaidi kutoka Sida kuliko ilivyotarajiwa. Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo:-

 

i)     Jumla ya madarasa 51 (Unguja 24, Pemba 27) ya skuli za msingi yamekamilishwa. Ujenzi wa madarasa mengine 118 (Unguja 66, Pemba 52) unaendelea.

 

ii)    Ukarabati wa majengo umefanyika katika skuli za msingi za Chuini, Kidimni, Kitogani, Kilimahewa, Unguja-Ukuu na Micheweni.

 

iii)  Jumla ya madawati 1,782, viti 774 na meza 774 yamechongwa na kusambazwa katika skuli za msingi na sekondari za wananchi.

 

iv)  Ujenzi wa skuli ya msingi ya Urafiki iliyopo Mwanakwerekwe umekamilika kwa hatua zote.  Wizara imekabidhiwa skuli hiyo pamoja na samani za madarasani, ofisini na maktaba tarehe 21 Aprili, 2013.

 

v)    Majaribio (pilot testing) ya matumizi ya miongozo ya maji, afya na mazingira katika skuli yametolewa kwa walimu 36 wa skuli za msingi za Pemba na wajumbe wa kamati za skuli 15 za Unguja. Ujenzi wa vyoo, minara ya maji na sehemu za kukoshea mikono katika skuli 13 (Unguja 05 na Pemba 08) unaendelea.

 

vi)  Mradi wa TZ-21 umeendelezwa kwa kutoa machapisho ya “e-content”, kutathmini miundiombinu ya vyuo vya ualimu, vituo vya walimu na skuli za msingi ili kuona utayari wao wa kupokea vifaa vya ICT na kuunganishwa na huduma ya “internet”. Pia vifaa mbali mbali zikiwemo kompyuta vimefungwa katika skuli 74. Jumla ya nakala 33,884 za vitabu zimechapishwa na kugawiwa katika skuli za msingi, vituo vya walimu na vyuo vya ualimu. Programu mpya (EMIS Database) kwa ajili ya uingizaji na uchambuzi wa takwimu imewekwa Wizarani.  Wafanyakazi 12 wa divisheni ya takwimu wamefundishwa (kwa vitendo) jinsi ya kutumia mfumo mpya wa kompyuta kwa kuingiza na kusafisha data na kutoa ripoti za kitakwimu.

 

Mradi wa Ujenzi wa Vyuo vya Kiislamu

20.       Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa na SMZ pekee na ulikuwa na  malengo yafuatayo:-

(i)           Kujenga uzio kuzunguka eneo la Chuo cha Kiislamu Micheweni na Chuo cha Kiislamu Mazizini.

 

(ii)          Kuendeleza ukarabati wa majengo ya Chuo cha Kiislamu Micheweni.

 

Mradi huu ulitengewa jumla ya T.Sh. 25,000,000/-. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, mradi uliingiziwa T.Sh. 20,000,000/- sawa na asilimia 80 ya makadirio. Kazi za ujenzi wa uzio zinaendelea.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali.

21.         Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa na SMZ kwa mashirikiano na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Mradi ulipangiwa kutekeleza malengo yafuatayo:-

(i)           Kuendelea kutoa mikopo kwa vikundi vya wahitimu kutoka vituo vya mafunzo ya amali.

 

(ii)          Kuendeleza ujenzi wa Kituo cha Elimu Mbadala cha Wingwi Mtemani Pemba.

 

(iii)        Kutafuta washauri elekezi na wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya elimu mbadala vitatu, vituo vya mafunzo ya amali viwili, upanuzi na ukarabati wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, upanuzi na ukarabati wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar na ujenzi wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar.

 

(iv)        Kuandaa mitaala kwa ajili ya mafunzo ya wakufunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar na wakufunzi wa mafunzo ya amali.

 

(v)          Kupitia na kurekebisha mitaala ya mafunzo kwa wanafunzi wa vituo vya Elimu Mbadala.

 

(vi)        Kununua vifaa na magari kwa ajili ya Ofisi ya uratibu wa mradi wa Kamisheni ya Kazi.

 

Jumla ya T.Sh. 100,000,000/- za SMZ na T.Sh. 1,994,098,000/- za AfDB zilitengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu.  Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 65,000,000/- za SMZ sawa na asilimia 65 ya makadirio zilipatikana. Aidha T.Sh. 1,230,072,040/- za AfDB sawa na asilimia 61.7 ya makadirio zilipatikana. Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo:-

 

i)     Wizara imevikopesha vikundi vya kuweka na kukopa (SACCOS) vya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Unguja na Pemba jumla ya T.Sh. 530,500,000/- kwa ajili ya kununua vespa za kuwakopesha walimu. Jumla ya vespa 100 zimekopeshwa kwa walimu wa skuli za Unguja na vespa 130 zimekopeshwa kwa walimu wa skuli za Pemba. Aidha, jumla ya T.Sh. 154,950,000/- zimekusanywa kutoka kwa vikundi vilivyokopeshwa hapo zamani.

 

ii)    Jumla ya T.Sh. 30,000,000/= zimetumika kwa ajili ya kuwalipa fidia ya mazao wananchi wa Vitongoji ambao mazao yao yaling’olewa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Mafunzo ya Amali Vitongoji.

 

iii)  Uchambuzi wa tathmini ya zabuni za kuwaajiri washauri elekezi kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya viwili vya elimu mbadala, vituo viwili mafunzo ya amali, upanuzi na ukarabati wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, upanuzi na ukarabati wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar na ujenzi wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mafunzo ya Amali unaendelea.

 

iv)  Uchambuzi wa tathmini za zabuni za kuwaajiri washauri elekezi kwa ajili ya kazi ya kupitia na kurekebisha mitaala kwa ajili ya mafunzo ya wakufunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar, wakufunzi wa mafunzo ya amali na mafunzo ya wanafunzi wa vituo vya elimu mbadala umekamilika.  Washauri hao wameanza kazi ya kuandika mitaala husika.

 

v)    Vifaa vya ofisi na gari nne za mradi zimenunuliwa.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima.

22.         Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya SMZ, Benki ya Dunia na BADEA.  Mradi huu ulikuwa na  malengo yafuatayo:-

(i)           Kukamilisha ujenzi wa skuli za sekondari za ghorofa za Kiembesamaki, Kwamtipura na Mpendae.

(ii)          Kukamilisha ujenzi wa skuli za sekondari za Miwaleni, Donge, Maungani, Makongeni na Chanjamjawiri zilizoanzishwa na wananchi.

(iii)        Kukamilisha ujenzi wa skuli za sekondari za Paje Mtule, Tunguu na Dimani.

(iv)        Kukamilisha ukarabati wa skuli za sekondari za Tumekuja, Fidel Castro, Forodhani, Uweleni, Hamamni na Utaani.

(v)          Kuchonga seti 2,000 za meza na viti kwa madarasa ya sekondari yaliyomalizika kujengwa.

(vi)        Kuanza ujenzi wa skuli mpya za sekondari za Kibuteni Unguja na Mkanyageni Pemba.

(vii)       Kuandika, kuchapisha na kusambaza vitabu vya kiada na miongozo ya walimu kwa ajili ya madarasa ya kwanza hadi la nne.

(viii)      Kuandika na kuchapisha moduli za kutolea mafunzo kazini kwa walimu wa Sayansi na Hisabati wa msingi.

(ix)        Kutoa mafunzo kwa walimu wa msingi na sekondari.

(x)          Kutoa mafunzo kwa walimu wakuu juu ya uendeshaji wa skuli.

 

Mradi huu ulitengewa jumla ya T.Sh. 900,000,000/- za SMZ, T.Sh. 24,000,000,000/- za Benki ya Dunia na T.Sh. 3,930,054,000/- za BADEA.  Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya TSh. 525,000,000/- za SMZ sawa na asilimia 58.3 zilipatikana. Pia T.Sh. 21,790,084,140.90/- za BADEA na Benki ya Dunia sawa na asilimia 92.3 ya makadirio zimepatikana.  Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo:-

 

i)             Ujenzi wa skuli za sekondari za ghorofa unaendelea katika skuli za sekondari za Mazizini, Kwamtipura na Mpendae. Skuli hizi zote zinatarajiwa kukamilika na kutumika mara tu skuli zitakapofunguliwa katika mwezi Agosti 2013.

 

ii)            Ujenzi wa skuli mpya za sekondari za Paje Mtule, Tunguu na Dimani umefikia asilimia 94.

 

iii)          Ukarabati wa skuli za sekondari za Utaani, Fidel-Castro, Forodhani na Tumekuja umekamilika na skuli hizo hivi sasa zinatumika. Ukarabati wa skuli za sekondari ya Uweleni na Hamamni unaendelea.

 

iv)          Ujenzi wa skuli mpya za sekondari za Kibuteni, Unguja na Mkanyageni, Pemba unaendelea vizuri.

 

v)            Jumla ya samani 80,806 zimepokelewa kwa ajili ya skuli mpya za sekondari za Mwanda, Chaani, Matemwe, Uzini, Dole, Paje-Mtule, Dimani na Tunguu kwa Unguja na Utaani, Ngwachani, Wawi, Madungu, Kiwani-Mauani, Chwaka-Tumbe, Konde, Pandani na Chuo cha Ualimu Benjamin Mkapa (awamu ya kwanza).

 

vi)          Wizara imetiliana saini mikataba na wazabuni watano wa kuandika na kuchapisha vitabu na miongozo ya walimu kwa ajili ya wanafunzi wa madarasa ya kwanza hadi la nne. Kazi ya uandishi na uhariri wa miswada ya vitabu hivyo inaendelea.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Ufundi

23.      Mheshimiwa Spika, mradi huu umetekelezwa na SMZ pekee na ulikuwa na malengo yafuatayo:-

 

(i)           Kuanza ujenzi wa dakhalia mpya ya skuli ya sekondari ya ufundi Kengeja.

(ii)          Kuipatia skuli ya sekondari ya ufundi Kengeja vifaa vya karakana

(iii)        Kuendelea na ukarabati wa majengo, kununua vifaa vya kufundishia na vitabu kwa ajili ya Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia.

 

Jumla ya T.Sh. 400,000,000/- za SMZ zilitengwa kwa ajili ya kukamilisha malengo yaliyowekwa.  Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 50,000,000/- zimepatikana ikiwa ni sawa na asilimia 25 ya makadirio. Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo:-

 

i)     Wizara imetiliana saini na kampuni itakayopeleka vifaa vya karakana ya umeme katika skuli ya sekondari ya ufundi ya Kengeja.

 

ii)    Ukarabati wa mfumo wa maji safi katika eneo la Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia umekamilika. Pia, vifaa mbali mbali vya kufundishia vikiwemo “multimedia” tatu na vitabu 150 vya somo la Hisabati vimenunuliwa.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi.

24.      Mheshimiwa Spika, mradi huu ulitengewa jumla ya T. Sh. 150,000,000/- za SMZ na T.Sh. 491,200,000/- za UNICEF. Malengo ya mradi huu yalikuwa ni :-

i)     Kuendelea kutoa mafunzo ya mtaala mpya kwa walimu wa elimu ya maandalizi.

ii)    Kuandika na kuchapisha moduli kwa ajili ya wakufunzi wa walimu wa maandalizi kwa njia ya redio.

iii)  Kuanza kutoa mafunzo ya walimu wa maandalizi 1,000 kwa njia ya redio.

iv)  Kununua vifaa vya kufundishia.

v)    Kujenga na kuchonga samani za skuli mbili mpya za maandalizi.

 

Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 50,000,000/- za SMZ sawa na asilimia 33.3 ya makadirio zilipatikana na kutumika. Kwa upande wa UNICEF, T.Sh. 23,357,300/- sawa na asilimia 22.9 zimepatikana. Utekelezaji halisi wa mradi ulikuwa kama ifuatavyo:-.

 

i)     Walimu 210 wa elimu ya maandalizi wa skuli za Unguja na Pemba wamepatiwa mafunzo juu ya utumiaji wa mtaala mpya wa elimu ya maandalizi

 

ii)    Ujenzi wa skuli ya maandalizi Jongowe umeanza na ujenzi wa skuli ya maandalizi Konde umeendelezwa.

 

iii)  Ukarabati wa madarasa matatu na vyoo vya skuli ya maandalizi Machomanne umefanyika.

 

iv)  Moduli ya tatu kwa ajili ya kutolea mafunzo kwa wakufunzi wa walimu wa maandalizi imeandikwa. Mafunzo kwa walimu yatatolewa baada ya kukamilika kwa uandishi na kuchapishwa kwa moduli ya nne hadi ya sita.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi kwa Wilaya ya Magharibi

25.      Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa na SMZ pekee na ulikuwa na malengo yafuatayo :-

i)     Kukamilisha ujenzi wa madarasa 70 yaliyoanzishwa na wananchi.

ii)    Kuchonga madawati 1,050.

 

Mradi huu ulitengewa jumla ya T.Sh. 800,000,000/- kwa ajili ya kukamilisha malengo yaliyowekwa.

 

Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 135,000,000/= zimepatikana ikiwa ni sawa na asilimia 16.9 ya makadirio. Jumla ya madarasa 18 katika skuli za Chuini, Kianga, Fuoni-Birikani na Kinuni yamekamilika.

 

Mradi wa Sayansi na Teknolojia

26.      Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kwa mashirikiano na Benki ya Dunia na ulikuwa na malengo yafuatayo:-

i)     Kununua vifaa vya maabara za Sayansi na ICT.

ii)    Kusomesha wakufunzi katika ngazi ya shahada ya pili na ya tatu.

 

Mradi ulitengewa jumla ya T.Sh. 830,529,600/- za Benki ya Dunia. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T.Sh. 277,292,840/- sawa na asilimia 34.1 ya makadirio zimepatikana na kutumika.  Utekelezaji halisi wa malengo ni kama ifuatavyo:-

i)     Vifaa mbali mbali vya kufundishia vikiwemo vitabu, vifaa vya maabara na vya ICT vimenunuliwa.

ii)    Jumla ya wafanyakazi 56 (31 shahada ya uzamivu, 21 shahada ya uzamili, 02 shahada ya kwanza na 02 stashahada wanaendelea na masomo katika vyuo mbali mbali. Ada za masomo na stahiki nyengine zimelipwa.

 

Mpango wa Maendeleo kwa Mwaka 2013/2014

27.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014, Wizara imepanga kutekeleza miradi tisa yote ikiwa ni miradi inayoendelea. Kati ya miradi hiyo, minne inatarajiwa kutekelezwa kutokana na bajeti ya SMZ pekee na miradi mitano itatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na washirika wa maendeleo wa ndani na nje ya nchi.  Jumla ya T.Sh. 5,350,000,000/- za SMZ na T.Sh.8,779,632,000/- ambazo ni ruzuku kutoka kwa washirika mbali mbali wa maendeleo na TSh. 21,417,987,000/- ni mkopo kutoka Benki ya Dunia, Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (Badea) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa malengo ya miradi hiyo. Jadweli namba 46 inatoa uchambuzi zaidi.

 

Malengo ya miradi mbali mbali itakayotekelezwa ni kama ifuatavyo:-

 

    Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi.

28.       Mheshimiwa Spika, mradi huu utatekelezwa kwa mashirikiano kati ya SMZ, GPE na UNICEF.  Malengo ya mradi huu ni kama hivi ifuatavyo:-

 

i)     Kuendelea kutoa mafunzo ya mtaala mpya kwa walimu wa elimu ya maandalizi.

ii)    Kukamilisha ujenzi wa skuli za maandalizi za Jongowe na Konde.

 

iii)  Kununua samani kwa skuli za maandalizi za Jongowe, Konde na Tunduni.

 

iv)  Kuwapa mafunzo walimu wa skuli za maandalizi kwa kupitia vipindi vya redio.

 

v)    Kuandika na kuchapisha moduli ya 4 na ya 5 kwa ajili ya kutolea mafunzo kwa wakufunzi wa walimu wa maandalizi kwa njia ya redio.

 

vi)  Kununua vifaa vya kufundishia watoto wa vituo vya Tucheze Tujifunze.

 

Mradi umetengewa jumla ya T.Sh. 150,000,000/- za SMZ na T.Sh. 1,567,600,000/- za UNICEF na GPE.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya msingi

29.         Mheshimiwa Spika, mradi huu utatekelezwa kwa mashirikiano kati ya wananchi, mashirika ya maendeleo yakiwemo Sida, UNICEF, UNESCO, GPE na USAID. Mradi huu utakuwa na   malengo yafuatayo:-

 

i)             Kukamilisha ujenzi wa madarasa 480 kwa kushirikiana na wananchi katika wilaya tisa za Unguja na Pemba.

ii)            Kufanya ukarabati wa majengo katika skuli 12 za msingi.

iii)          Kuchonga madawati 10,000 na kuyasambaza katika madarasa mapya yaliyojengwa.

iv)          Kuwapatia walimu mafunzo mbali mbali yakiwemo ya matumizi ya lugha ya Kiingereza kwa ajili ya kufundishia, mafunzo juu ya mtaala mpya wa ngazi ya msingi na mafunzo juu ya kufundisha katika mfumo wa elimu mjumuisho.

v)            Kukamilisha ujenzi wa nyumba tatu za walimu.

vi)          Kuendelea na utekelezaji wa mradi wa TZ-21.

 

Mradi umetengewa jumla ya T.Sh. 1,000,000,000/- za SMZ, T.Sh. 7,212,032,000/- kutoka Sida, UNICEF, UNESCO na GPE.

                    

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi Wilaya ya Magharibi.

30.         Mheshimiwa Spika, mradi huu una madhumuni ya kuimarisha utoaji wa elimu ya msingi kwa skuli za Wilaya ya Magharibi kwa kuongeza madarasa na samani kwa lengo la kupunguza wingi wa wanafunzi madarasani. Mradi huu utatekelezwa na SMZ na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.  Mradi utakuwa na malengo yafuatayo:-.

 

i)     Kujenga skuli mbili mpya za msingi.

 

ii)    Kukamilisha madarasa 20 ya skuli za msingi yaliyoanzishwa na wananchi.

 

iii)  Kununua samani za skuli za msingi zitazojengwa

 

Mradi umetengewa jumla T.Sh. 850,000,000/- za SMZ.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima

31.         Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano kati ya SMZ, Benki ya Dunia na BADEA. Mradi huu utakuwa na malengo yafuatayo:-

i)     Kukamilisha ujenzi wa skuli za sekondari za Kibuteni na Mkanyageni.

 

ii)    Kukamilisha ujenzi wa madarasa katika skuli nne za sekondari yalizoanzishwa na wananchi.

 

iii)  Kuchonga na kusambaza samani katika skuli za sekondari zilizokamilishwa kujengwa.

 

iv)  Kujenga “grills” katika vyumba vya maabara vya skuli mpya za sekondari 16.

 

v)    Kukamilisha ujenzi wa skuli za sekondari za Paje mtule, Dimani na Tunguu na kujenga ukuta kuzunguka skuli mbili mpya za sekondari kati ya skuli zilizojengwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Mradi umetengewa jumla T.Sh. 1,000,000,000/- za SMZ na T.Sh. 17,647,160,000/- kutoka Benki ya Dunia na Badea.

 

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Ufundi.

32.         Mheshimiwa Spika, mradi huu utatekelezwa na SMZ pekee. Malengo ya mradi huu ni kama ifuatavyo:-

 

i)                    Kuanza ujenzi wa dakhalia mpya ya skuli ya sekondari ya ufundi, Kengeja.

ii)                  Kununua vifaa vya kufundishia kwa ajili ya skuli ya sekondari ya ufundi, Kengeja na Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia.

 

Mradi umetengewa jumla ya T.Sh. 500,000,000/-.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali

33.         Mheshimiwa Spika, mradi huu utatekelezwa na SMZ kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Mradi utakuwa na malengo yafuatayo:-

 

i)             Kukamilisha uandaaji wa mitaala kwa ajili ya mafunzo ya wakufunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar na wakufunzi wa mafunzo ya amali.

ii)            Kukamilisha mapitio na marekebisho ya mitaala ya mafunzo kwa  wanafunzi wa vituo vya Elimu Mbadala

iii)          Kuchagua mshauri elekezi, kuandaa michoro ya ujenzi wa vituo vitatu vya elimu mbadala na vituo viwili vya mafunzo ya amali na kutangaza zabuni za ujenzi.

iv)          Kuchagua mshauri elekezi na kuandaa michoro ya ukarabati na utanuzi wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, Chuo cha Utalii Maruhubi na ujenzi wa makao makuu ya Mamlaka ya Mafunzo ya Amali. Pia kutangaza zabuni za ujenzi.

v)            Kulipa sehemu ya fidia ya vipando kwa wananchi wa eneo la Kituo cha Mafunzo ya Kazi za Amali, Vitongoji ambao mazao yao yalig’olewa wakati wa ujenzi wa kituo.

 

Jumla ya T.Sh. 700,000,000/- za SMZ na T.Sh. 1,529,906,000/- za AfDB zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi.

 

Mradi wa Uimarishaji wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.

34.         Mheshimiwa Spika, mradi huu utatekelezwa na SMZ kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (Badea) na unakusudia kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) kwa kukamilisha malipo ya wakandarasi wa ujenzi na wazabuni wa samani, vifaa vya maabara na vifaa vya ICT. Pia mradi utaanza maandalizi ya awamu ya pili ya ujenzi wa Chuo.

 

Mradi huu umetengewa T.Sh. 850,000,000/- za SMZ na T.Sh. 2,240,921,000/- kutoka Badea.

 

Mradi wa Upanuzi na Uimarishaji wa Huduma za Maktaba.

35.         Mheshimiwa Spika, mradi huu unatekelezwa na SMZ pekee na utakuwa na lengo la kuendelea na ujenzi wa maktaba kuu, tawi la Pemba. Mradi umetengewa T.Sh. 400,000,000/- za SMZ.

Mradi wa Ujenzi wa Vyuo vya Kiislamu:

36.       Mheshimiwa Spika, mradi huu utatekelezwa na SMZ pekee na utakuwa na malengo yafuatayo:-

(i)           Kuendelea na ujenzi wa uzio kuzunguka eneo la Chuo cha Kiislamu Micheweni na kuanza maandalizi ya ujenzi wa uzio katika Chuo cha Kiislamu, Mazizini.

 

(ii)          Kuendeleza ukarabati wa majengo ya Chuo cha Kiislamu Micheweni yaliyopo.

 

Jumla ya T.Sh.100,000,000/- za SMZ zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha malengo hayo.

 

Utafiti

37.         Mheshimiwa Spika, Wizara imefanya utafiti wa majaribio wa SACMEQ IV wenye lengo la kupima uwezo wa mwanafunzi wa msingi katika kusoma na kufanya Hisabati. Jumla ya wanafunzi 450, walimu 50 na walimu wakuu 15 wameshiriki utafiti huo. Taarifa za utafiti huu zinafanyiwa uchambuzi kwa kutumia kompyuta na zimepelekwa katika Kituo cha Uratibu wa Kazi za “SACMEQ” kilichopo katika Taasisi ya Kimataifa cha Mipango ya Elimu (IIEP) huko Paris kwa matayarisho ya utafiti mkuu unaotarajiwa kufanyika katika mwezi Septemba 2013. Wizara pia imefanya utafiti wa hali ya kisomo (literacy survey) ili kubaini maendeleo na changamoto zinazokikabili kisomo cha watu wazima. Taarifa za utafiti huo zimefanyiwa uchambuzi na uandishi wa ripoti unaendelea.

 

Pia, Wizara imekamilisha uandishi wa rasimu ya kwanza ya Ripoti ya Tathmini ya miaka 10 ya Elimu kwa Wote (EFA-End of Decade Assessment). Uandishi wa rasimu ya mwisho unaendelea baada ya kupata maoni ya Mshauri Elekezi kutoka UNESCO.

 

38.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara imekusudia kukamilisha utafiti mkuu wa SACMEQ IV, kukamilisha uandishi wa ripoti ya hali ya kisomo Zanzibar pamoja na kukamilisha uandishi ripoti ya tathmini ya miaka 10 ya Elimu kwa Wote. 

 

Ukusanyaji na Uchambuzi wa Taarifa za Elimu

39.         Mheshimiwa Spika, Idara inaendelea kuchambua na kutoa takwimu za elimu zinazoonesha maendeleo ya sekta ya elimu Zanzibar kupitia Divisheni yake ya Elimu. Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Misaada la Marekani (USAID) inaendelea na zoezi la matayarisho ya programu maalum ya uchambuzi kwa kutumia kompyuta (data base) kwa ajili ya kurahihisha uchambuzi na utoaji wa takwimu kwa wakati.  Aidha, skuli zote za msingi za serikali, Afisi za Elimu za Wilaya na Vituo vya walimu (TCs) zitapatiwa programu hii pamoja na kompyuta kwa ajili ya mfumo huo. Vile vile Wizara inafanya mazungumzo na mashirika hisani ili kuwezesha mfumo huo kutumika pia katika skuli za sekondari. Mfumo huo utazisaidia skuli kuweza kuweka kumbukumbu za mwanafunzi mmoja mmoja pamoja na kutathmini maendeleo yao ya kielimu. Pia utaziunganisha skuli zote na “database” iliyopo Wizarani.

 

Maendeleo ya Kisera

40.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Wizara iliandaa mpango kazi wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Elimu Zanzibar wa miaka minne kwa kipindi cha mwaka 2012/2013 hadi 2015/2016. Mpango-kazi huo utatekelezwa kwa ushirikiano kati ya SMZ, Mashirika yasio ya kiserikali, Jumuiya za Kimataifa.

 

        Wizara inakusudia kuitafsiri sera ya elimu ya mwaka 2006 kwa lugha ya Kiswahili ili kuweka mazingira mazuri ya utekelezaji wake. Wizara pia imepanga kuwasilisha sera ya elimu ya mwaka 2006 kwa watoaji wa elimu  wa skuli binafsi ili kupata uelewa mzuri na wenye uhakika wa mfumo mpya wa elimu wa Zanzibar.

 

          Ufuatiliaji na Tathmini

41.         Mheshimiwa Spika, ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa malengo ya Wizara ulifanyika katika kipindi chote cha mwaka 2012/2013.  Maafisa 30 wa Wizara walipatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo.

 

42.         Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Wizara imepanga kuendelea na kazi za ufuatiliaji na tathmini ya mipango ya kazi mbali mbali ya Wizara pamoja na kuandaa na kutoa ripoti za ufuatiliaji na tathmini hizo. Wizara pia itaandaa mkutano mkubwa wa kufanya tathmini ya elimu (Joint Education Sector Review) itayoshirikisha wadau mbali mbali wa elimu.

 

43.         Mheshimiwa Spika, Idara ya Mipango, Sera na Utafiti imepangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 2,170,000,000/- kwa Unguja na T.Sh 871,000,000/- kwa Ofisi ya Pemba kwa kazi za kawaida.

 

         IDARA YA UENDESHAJI NA UTUMISHI

44.         Mheshimiwa Spika, Idara hii inahusika na masuala yote ya kiutumishi na uendeshaji, kusimamia kanuni za kazi na maslahi ya wafanyakazi.  Idara pia inahusika na shughuli za kuratibu safari za wafanyakazi wote ndani na nje ya nchi, utunzaji wa kumbukumbu za wafanyakazi pamoja na utunzaji wa majengo. Vile vile, Idara inaratibu mafunzo mbali mbali ya wafanyakazi kulingana na mahitaji.

 

45.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, jumla ya walimu 578 (343 Unguja, 235 Pemba) waliajiriwa baada ya kupata kibali cha uajiri kutoka Tume ya Utumishi Serikalini. Kati yao, walimu 200 ni wa shahada ya kwanza, mmoja ni wa shahada ya pili, 59 ni wa stashahada ya sayansi na walimu 184 ni wa stashahada ya sanaa. Pia Wizara imepata kibali cha uajiri wa walimu wa cheti 150 kwa ajili ya skuli za msingi katika Mikoa 4 ya Unguja na Pemba. Walimu hawa hivi sasa wanakamilisha taratibu za ajira na wataajiriwa rasmi mara tu skuli zitakapofunguliwa katika mwezi Agosti 2013.

 

Katika jitihada za kuwaendeleza watumishi wa Wizara, jumla ya wafanyakazi 821 walipatiwa fursa ya kujiunga na masomo katika ngazi tofauti kuanzia cheti hadi shahada ya uzamivu katika vyuo mbali mbali vya ndani na nje ya nchi.

 

46.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, jumla ya wafanyakazi 110 walistaafu kazi kwa mujibu wa sheria,wafanyakazi 03 walifukuzwa kazi kutokana na makosa mbali mbali, 04 waliacha kazi kwa hiari zao 13 walifariki dunia. Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema peponi, Amin. Aidha wafanyakazi 43 walipewa uhamisho kwenda kuendelea na kazi katika Wizara na Taasisi mbali mbali za Serikali na wafanyakazi 17 walichukua likizo bila ya malipo.

Hadi kufikia mwezi Juni, 2013, Wizara ilikuwa na jumla ya wafanyakazi 13,677, kati yao, 8,381 ni wanawake na 5,296 ni wanaume. Wafanyakazi 9,991 wapo Unguja (wanawake 6,542 na wanaume ni 3,449). Kwa upande wa Pemba wapo wafanyakazi 3,686 (wanaume ni 1,847 na wanawake ni 1,839).  Kati ya wafanyakazi wote, 12,128 ni wa kada ya ualimu na 1,448 ni wafanyakazi wasiokuwa wa kada ya ualimu.

                  

47.         Mheshimiwa Spika, katika kuendeleza juhudi za kuwasaidia wafanyakazi wetu katika kujikwamua na matatizo ya kimaisha, Wizara imeweza kuwadhamini wafanyakazi 457 (378 Unguja na 79 Pemba) kupata mikopo ya fedha taslimu, vifaa vya ujenzi, vipando na vifaa vya matumizi ya nyumbani.  Wafanyakazi hawa walifaidika na mikopo yenye thamani ya T.Sh. 706,677,397/-.

 

48.         Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii, kuushukuru uongozi wa Benki ya Watu wa Zanzibar, Benki ya Posta Tanzania, CRDB, Benki ya Barclays na Saccos zote kwa kuwapatia watumishi wa Wizara yangu mikopo hii ya fedha taslimu na vifaa mbali mbali ili waweze kujikwamua kimaisha. Nawaomba waendelee na utaratibu huu nasi tutatoa ushirikiano mkubwa kufanikisha azma hii.

 

49.         Mheshimiwa Spika, ninafuraha kulijulisha Baraza lako tukufu kuwa Wizara itaanza kulipa viwango vipya vya maposho kwa Wakuu wa Vyuo, Walimu Wakuu na wasaidizi wao, Maafisa Wa Elimu wa Mikoa na Wilaya na Wakaguzi wa Elimu kuanzia mwezi Julai 2013, baada ya kupitishwa rasmi na Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Viwango hivyo vinatarajiwa kuongeza ari, juhudi na tija katika utekelezaji wa kazi zao. Pia, katika mwaka 2013/2014, Idara itaendelea kuwapatia walimu na wafanyakazi wasiokuwa walimu mbali mbali nafasi za masomo ili kuimarisha utendaji wa kazi zao. Pia, itatoa mafunzo kwa maofisa utumishi wa Idara na Taasisi mbali mbali za Wizara na walimu wakuu kuhusu sheria na kanuni za utumishi Serikalini, kuboresha ‘database’ la wafanyakazi, kukamilisha utayarishaji wa mpango mkuu wa rasilimali watu wa Wizara, kuwapatia huduma bora na vitendea kazi wafanyakazi ili kuimarisha utendaji kazi. Vile vile, itawapatia likizo na huduma wafanyakazi 3,210 kwa kadiri hali ya fedha itakavyoruhusu. 

 

50.         Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Idara imepangiwa jumla ya T.Sh. 38,215,000,000/- kwa Unguja na T.Sh. 15,790,000,000/- kwa Pemba kwa kazi za kawaida.

 

          IDARA YA ELIMU YA MAANDALIZI NA MSINGI

51.         Mheshimiwa Spika, Idara ya Elimu ya Maandalizi na Msingi ina majukumu ya kusimamia utoaji wa elimu bora kwa ngazi ya maandalizi na msingi pamoja na uratibu wa elimu katika vyuo vya Kur-ani na madrasa hapa nchini. Aidha husimamia skuli binafsi za maandalizi na msingi ili kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa na skuli hizi inafuata mtaala uliokubalika na Serikali. Pia, Idara ina jukumu la kusimamia ustawi wa huduma za wanafunzi.

 

          Elimu ya Madrasa na Vyuo vya Kuran

52.         Mheshimiwa Spika, Idara hii inashughulikia jumla ya madrasa/vyuo vya Kur-ani 2,251.  Aidha zipo skuli za maandalizi za madrasa 84, Unguja na Pemba zinazosimamiwa na kuhudumiwa kupitia Kituo cha Zanzibar Madrasa Resource Centre (ZMRC), ambazo ufundishaji wake unafuata misingi ya dini ya kiislamu.

 

53.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/204, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la UNICEF inakusudia kutoa mafunzo kwa walimu wa madrasa/vyuo vya Kur-ani 350, Unguja 200 na Pemba 150. Pia itaendelea kufanya ziara mbali mbali za kikazi katika madrasa na vyuo vya Kur-ani pamoja na kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili pamoja na kushajiisha kufanya ziara za pamoja za kubadilishana uzoefu.

 

          Elimu ya Maandalizi

54.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, elimu ya maandalizi ilikuwa inatolewa katika skuli 278 zilizosajiliwa, kati ya hizo skuli 34 ni za Serikali na skuli 244 ni za binafsi.  Aidha zipo skuli 41 za msingi na 21 za msingi na kati zenye madarasa ya maandalizi na vituo 176 vya Tucheze Tujifunze (TUTU), ambavyo vinatoa mafunzo ya maandalizi kwa njia ya redio vyenye jumla ya watoto 4,097 na wasimamizi wa vituo 360. Vituo hivi vipo katika Wilaya ya Kaskazini ‘A” na Magharibi kwa Unguja na Wilaya ya Micheweni kwa Pemba. Vipindi hivyo vinarushwa kwa kupitia ZBC redio kwa watoto wa maandalizi na darasa la kwanza na la pili.  Kwa mwaka 2012/2013, idadi ya wanafunzi wa skuli za maandalizi imefikia 30,912 wakiwemo wanaume 15,008 na wanawake 15,904. Jadweli namba 13(a) – (c) zinatoa ufafanuzi zaidi.

 

55.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Idara iliendelea na juhudi za kuielimisha jamii kuwapeleka watoto wenye umri wa miaka minne kuandikishwa kwenye skuli za maandalizi.  Kazi hiyo ilifanywa kupitia mikutano na masheha, maafisa tawala wa Mikoa, wenyeviti wa bodi za elimu za mikoa na kamati za skuli za Unguja na Pemba.

 

56.         Mheshimiwa Spika, Idara ilitoa mafunzo kwa walimu 201, kati yao 115 Unguja na 95 Pemba wanaofundisha madarasa ya maandalizi yaliyomo ndani ya skuli za msingi kuhusu mbinu za kufundishia watoto wadogo.  Pia, walimu 30 wa skuli za maandalizi wamepatiwa mafunzo kwa ajili ya kuwaandaa kuwa wakufunzi wa elimu ya maandalizi katika vituo vya walimu vilivyoko katika maeneo yao.

 

          Elimu ya Msingi

57.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, elimu ya msingi ilitolewa katika skuli za msingi 342 zikiwemo skuli 263 za serikali na 79 za binafsi.  Idadi ya wanafunzi katika ngazi hii ya elimu imefikia 247,353 sawa na asilimia 124.4 ikilinganishwa na asilimia 121.5 ya mwaka 2011/2012. Aidha, watoto wote 35,703 walioandikishwa kuanza darasa la kwanza katika skuli za Serikali wamepatiwa nafasi.  Miongoni mwa watoto hao, 17,860 ni wanawake na 17,843 ni wanaume. Jadweli namba 14 na 15 zinatoa ufafanuzi zaidi.  

 

58.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, walimu wa skuli za msingi walipatiwa mafunzo juu ya elimu ya mazingira, afya na huduma ya kwanza ili kuweza kuzifanya skuli ziwe na mazingira rafiki kwa vijana, yatakayowezesha kupatikana kwa elimu bora.  Pia, Idara imetoa mafunzo kwa walimu wa darasa la kwanza 150 (65 Pemba, 85 Unguja) wanaowapokea watoto wanaotoka maandalizi juu ya kutumia mbinu bora za kufundisha watoto wadogo. Vile vile, Idara imezipatia vifaa vya kufundishia na kujifunzia skuli za msingi 120 (72 Unguja na 48 Pemba) zilizo katika mazingira magumu zaidi ya kiuchumi.

 

59.         Mheshimiwa Spika, Idara kwa kushirikiana na Jumuiya ya Lions Club imetoa mafunzo kwa walimu 30 wa ushauri nasaha skulini kwa ajili ya kuwajengea uwezo juu ya mbinu bora za kuwashauri na kuwanasihi wanafunzi. Vile vile, Wizara ikishirikiana na jeshi la Polisi inaendelea kutoa mafunzo juu ya somo la usalama wetu kwanza katika skuli 10 za Wilaya ya Mjini kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi kuzielewa sheria mbali mbali za nchi, kutambua wajibu wao kwa jamii, kujilinda dhidi ya vitendo vya uvunjaji wa amani na kujilinda dhidi ya vitendo vya unyanyasaji na kuleta ustawi na maendeleo katika jamii.

 

60.         Mheshimiwa Spika, Idara kwa kushirikiana na Shirika la Save the Children linaendelea na majaribio ya mradi wa adhabu mbadala katika skuli za msingi 20 (12 Unguja na 8 Pemba). Mpango wa uhamasishaji jamii juu ya uimarishaji na ukuzaji wa matumizi ya adhabu mbadala unaendelezwa katika skuli zetu za Unguja na Pemba.

 

61.         Mheshimiwa Spika, Idara, kwa kushirikiana na Umoja wa Serikali za wanafunzi wa Zanzibar (USEWAZA) ilifanya ziara katika skuli mbali mbali za Unguja kwa lengo la kutoa taaluma juu ya utendaji wa serikali zao.  Pia, USEWAZA imeandaa na kurusha vipindi mbali mbali katika kituo cha ZBC TV vya kuelimisha jamii juu ya maendeleo ya elimu, ushauri nasaha, nafasi ya watoto wenye ulemavu katika jamii, mapambano dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia, umuhimu wa jamii kuchangia gharama za elimu kwa lengo la kuimarisha mazingira ya skuli na kupatikana kwa elimu iliyobora.

 

62.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara itaendelea kuzifanyia kazi changamoto mbali mbali zilizoko katika elimu hasa uhaba wa madarasa na msongamano wa wanafunzi, ukosefu wa vitabu na uhaba wa walimu wa baadhi ya masomo ili kuinua kiwango cha elimu katika ngazi za maandalizi na msingi. Pia, Idara itaendelea kuhamasisha jamii kuwapeleka watoto wao katika skuli za maandalizi na msingi, kuendelea kuzisaidia skuli zilizoko katika mazingira magumu ya kiuchumi ili kuzipatia vifaa vya kujifunzia na kufundishia vikiwemo madaftari, chaki, penseli, vifutio, rangi na vibao vya kusomea kadri ya hali ya upatikanaji wa fedha itakavyoruhusu.

 

63.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, kitengo cha Malaria inatarajia kutoa mafunzo kwa walimu na wanafunzi kupitia vituo vya walimu kuhusu kuondoa malaria Unguja na Pemba.

 

64.         Mheshimiwa Spika, Idara hii imepangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 237,945,000/- kwa Unguja na T.Sh. 81,055,000/- kwa Pemba kwa kazi za kawaida.

 

          IDARA YA ELIMU YA SEKONDARI

65.         Mheshimiwa Spika, Idara ya Elimu ya Sekondari inajukumu la kusimamia utekelezaji kazi za ufundishaji kwa ujumla na ufuatiliaji wa utendaji kazi maskulini, kupanga walimu katika skuli zote za serikali za sekondari na kuwapangia skuli wanafunzi waliofaulu katika ngazi mbali mbali za elimu, shughuli za uzalishaji mali na uwekaji wa kumbukumbu za mapato na matumizi ya skuli, kufuatilia utendaji wa serikali za wanafunzi na huduma za dakhalia.

 

66.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, elimu ya sekondari ilikuwa inatolewa katika skuli 252 kati ya hizo skuli 205 ni za serikali na 47 ni za binafsi.  Skuli hizo zilikuwa na wanafunzi 78,956 kuanzia kidato cha kwanza hadi kidato cha sita kati yao wanaume ni 36,162 na wanawake ni 42,794.  Katika ngazi ya elimu ya lazima (FI hadi FII) walikuwepo wanafunzi 49,977 ambao ni asilimia 84.5 ya watoto wenye umri wa miaka 14 – 15 wanaotarajiwa kuwepo skuli.  Kwa upande wa sekondari, kidato cha tatu hadi cha sita walikuwepo wanafunzi 27,139 na michepuo (kidato 1 – 4) walikuwepo wanafunzi 4,070. Jadweli namba 17, 18 na 22  zinatoa uchambuzi zaidi

 

67.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Idara, imetoa mafunzo kwa walimu kuhusu miiko na maadili katika kazi ya ualimu, mafunzo ya uongozi kwa walimu wakuu wapya pamoja na wasaidizi walimu wakuu wapya. Pia, Idara imetoa mafunzo kuhusu utunzaji vifaa vya maabara na kemikali na ununuzi wa vifaa kwa walimu wa sekondari wa masomo ya sayansi kwa skuli 70 za Unguja na Pemba. Mafunzo pia yalitolewa kwa walimu wa paneli za masomo kwa skuli 74 na uimarishaji wa somo la Kiingereza na Hisabati kwa skuli 50 za Unguja na Pemba.          

 

68.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara, inakusudia kuendelea kutoa mafunzo kwa walimu wapya watakaoajiriwa pamoja na kutoa mafunzo ya uongozi kwa walimu wakuu wapya na wasaidizi walimu wakuu wapya. Pia, Idara inakusudia kuendelea kutoa mafunzo zaidi kwa walimu wa paneli za masomo ya uimarishaji wa somo la Kiingereza, Hisabati na Sayansi pamoja na utumiaji na utunzaji wa vifaa vya maabara kwa walimu wa masomo ya Sayansi.

 

          Kazi za Ujasiriamali

69.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, shughuli za ujasiriamali zimeendelezwa katika skuli zetu.  Skuli zetu nyingi zimeweza kukusanya mapato kutokana na miradi iliyobuniwa ambapo fedha zinazopatikana husaidia katika kutatua matatizo madogo madogo yanayozikabili skuli hizo. 

 

70.         Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2013/2014, Idara inakusudia kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa walimu husika na itaendelea kuzisaidia skuli kubuni miradi ambayo itasaidia skuli hizo kuweza kujitegemea.

 

Serikali za Wanafunzi

71.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa 2012/2013, Serikali za wanafunzi katika skuli zimetekeleza majukumu yake kwa kiwango kinachoridhisha.  Serikali hizo zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuwasaidia walimu kusimamia kazi za usafi wa mazingira ya skuli, kudumisha nidhamu za wanafunzi na kuwaandaa wanafunzi katika kazi za uongozi baada ya kumaliza skuli. 

 

Katika mwaka 2013/2014, Idara inakusudia kuandaa mafunzo kwa viongozi wa serikali kwa skuli za Serikali na binafsi ili kukuza uelewa wao.

 

Huduma za Dakhalia

72.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, idadi ya wanafunzi walioishi dakhalia ilifika 1,774, kati yao wanaume 839 na wanawake 917. Katika kuimarisha dakhalia zetu, Idara imeupitia upya mwongozo wa kuchukua wanafunzi watakaoishi dakhalia. Vile vile imeandaa mikakati madhubuti ya kuziendesha dakhalia kwa ubora na uendelevu ili kuwawezesha wanafunzi kujifunza wakiwa katika mazingira mazuri na yaliyo bora. Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wazazi wa wanafunzi wanaoishi dakhalia kwa kuendelea kuwahudumia watoto wao.

 

73.         Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Idara imepangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 1,706,700,000/- kwa Unguja na T.Sh. 113,300,000/- kwa Pemba kwa kazi za kawaida.

 

IDARA YA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO KATIKA ELIMU

74.         Mheshimiwa Spika, Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika Elimu huratibu na kutoa mafunzo ya TEKNOHAMA kwa watendaji wa Wizara, kusimamia matumizi sahihi ya TEKNOHAMA katika kusoma na kufundishia katika ngazi mbali mbali za elimu. Pia inajukumu la kutayarisha na kusimamia programu mbali mbali  za usambazaji wa taarifa mbali mbali za elimu na kulinda usalama wa taarifa na rasilimali za wizara kwa kutumia TEKNOHAMA.

 

Sera ya ICT katika Elimu na Mpango Mkakati wake

75.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Idara iliandaa rasimu ya Sera ya ICT katika elimu na kuanza maandalizi ya mpango mkakati wa sera hiyo. Wadau mbali mbali wa elimu walipata fursa ya kutoa michango yao kupitia warsha na mikutano iliyofanyika kwa nyakati tofauti.  Rasimu ya Sera hiyo itapitishwa katika vikao vya ngazi mbali mbali vya Serikali kabla ya kutumika rasmi.

 

Utekelezaji wa Mradi wa “TZ-21 Century Basic Education”.

76.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, elimu ya msingi imeimarishwa kwa matumizi ya TEKNOHAMA chini ya mradi wa “21ST  Century Basic Education” kwa kutoa machapisho mbali mbali kwa mtindo wa “e-content” pamoja na kuendesha mafunzo kwa walimu wa masomo ya lugha, hisabati na sayansi. Aidha, walimu wa masomo ya lugha 1,201 wamepatiwa mafunzo juu ya “e-content”, kati ya hao walimu 911 ni wanawake na 190 wanaume.

 

Kuimarisha njia za Mawasiliano na Usambazaji wa Taarifa kupitia TEKNOHAMA.

77.         Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha njia za mawasiliano na usambazaji wa taarifa kupitia TEKNOHAMA, Idara ilifanya marekebisho ya tovuti ya Wizara kutokana na ile ya mwanzo kukabiliwa na matatizo ya kiufundi na kwa muda mwingi kutokuwepo hewani.  Pia yalifanyika mabadiliko ya “Hosting na Domain” mpya ya tovuti hiyo ili kuleta ufanisi zaidi. Anuani yetu ya sasa ni www.moez.go.tz. Kwa kutumia tovuti hiyo, Wizara imekuwa ikitoa taarifa mbali mbali zinazohusu maendeleo ya kielimu kama vile utoaji wa matokeo ya mitihani ya kidato cha pili, darasa la saba na kidato cha nne.  Pia tovuti imetumika kutangaza zabuni, mikopo ya elimu na taarifa za ajira kwa kadri hali inavyoruhusu. Aidha, Ofisi kuu Pemba imefungiwa mtandao ili kuweza kuhaulisha taarifa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyengine kwa urahisi zaidi.

 

Kuimarisha Elimu ya Maandalizi kwa kutumia    vifaa vya ICT

78.         Mheshimiwa Spika, Idara iliandaa mafunzo ya walimu wasaidizi wanaosimamia vituo vya utoaji wa elimu ya maandalizi kwa njia ya redio. Jumla ya washiriki 180 wamepatiwa mafunzo ya uendeshaji wa vituo vya Tucheze Tujifunze (TUTU), kati ya hao 91 kutoka Pemba na 80 kutoka Unguja.  Pia Idara kwa kushirikiana na shirika la habari la Zanzibar (ZBC) inaendelea kurusha hewani vipindi cha Tucheze Tujifunze (TUTU) na hadi kufikia mwezi wa Juni tayari vipindi 119 vimerushwa hewani.

 

79.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara inakusudia kuandaa mpango mkakati wa Sera ya ICT, kutoa mafunzo ya ICT kwa walimu 90 na watendaji wengine 36 wa Wizara kulingana na kada zao, kuanzisha vituo 40 vya Tucheze Tujifunze (TUTU) kwa Wilaya ya Kaskazini B, Wilaya ya Magharibi na Wilaya ya Mkoani, kuimarisha matumizi sahihi ya TEKNOHAMA kwa ajili ya kujifunza na kufundisha na kuimarisha njia za mawasiliano na usalama wa taarifa kupitia TEKNOHAMA.

 

80.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara hii imepangiwa kutumia T. Sh. 300,000,000/- kwa Unguja na T.Sh. 100,000,000/- kwa Pemba kwa kazi za kawaida.

 

                    IDARA YA ELIMU MBADALA NA WATU WAZIMA

81.         Mheshimiwa Spika, Idara hii inawajibu wa kuondoa tatizo la kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa wananchi wote wa visiwa vya Zanzibar, kuwapatia Elimu Mbadala vijana walioacha masomo njiani na wale ambao hawakubahatika kuandikishwa kabisa na kuwaendeleza kielimu wale wote wenye nia ya kufanya hivyo.

 

Kisomo

82.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Jumla ya madarasa mapya 23 ya kisomo yamefunguliwa mjini na vijijini Unguja na Pemba. Madarasa hayo yana wanakisomo 463 wakiwemo wanawake 411 na wanaume 52. Jumla ya wanakisomo 5,617 wamefanyiwa upimaji katika hatua zote nne. Katika upimaji huo jumla ya wanakisomo 4,671 wakiwemo wanawake 3,968 na wanaume 703 wamefaulu na 434 wamekombolewa.

 

83.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara itaendelea na jitihada zake za kushajihisha na kuhamasisha wananchi ambao hawajui kusoma na kuandika kujiunga katika madarasa ya kisomo hasa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja na Kaskazini Pemba ambako kuna idadi kubwa ya wananchi wasiojua kusoma na kuandika ukilinganisha na mikoa mengine. Pia kufungua na kuziendeleza maktaba za kisomo kwa kuzipatia nyezo stahiki.

 

84.         Mheshimiwa Spika, Elimu Mbadala inatolewa kwa vijana wenye umri kati ya miaka 10 hadi 15 walioko nje ya skuli, wakiwemo walioacha njiani kutokana na sababu mbali mbali. Idadi ya madarasa ya Elimu Mbadala ni 34 kwa Unguja na Pemba yenye jumla ya wanafunzi 839 (Pemba 376 na Unguja 463) kati ya wanafunzi hawa, wanawake ni 211 na wanaume ni 628.

 

85.         Mheshimiwa Spika, kituo cha Elimu Mbadala Rahaleo kina vijana 309 (wanawake 92 na wanaume 217). Wanafunzi wanaosoma katika kituo hiki licha ya kusoma masomo ya kawaida pia wanafundishwa fani mbali mbali zikiwemo ushoni, upishi, umeme, uchongaji na utunzaji nyumba. Kituo kimeshatoa wahitimu 323 wa fani za umeme na uchongaji tokea kuanzishwa kwake wakiwemo wanaume 237 na wanawake 86 ambao wametunukiwa vyeti.  Wengi wa wahitimu wetu wameweza kuajiriwa katika taasisi mbali mbali binafsi na wengine wamejiajiri wenyewe.

 

86.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara inakusudia kupanua wigo wa kuhamasishaji vijana kujiunga na madarasa ya Elimu Mbadala katika skuli za msingi na pia kuongeza wanafunzi katika Kituo cha Elimu Mbadala, Rahaleo.

 

Vituo vya Kujiendeleza

87.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka, 2012/2013, jumla ya wanafunzi 3,522 (wanawake 1,776 na wanaume 1,745) wamesajiliwa katika vituo mbali mbali vya kujiendeleza Unguja na Pemba. Katika mwaka huu wanafunzi 11,396 wamefanya mitihani ya faragha wa kidato cha nne na wanafunzi 1,935 wamefaulu, sawa na asimilia 17.0 ya watahiniwa wote. 

 

Pia, jumla ya wanafunzi 653 wa kidato cha sita wametahiniwa, kati yao 213 wamefaulu sawa na asilimia 32.6

 

88.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara itahamasisha vijana wengi zaidi kujiunga na vituo vya kujiendeleza hasa katika maeneo ambayo yana idadi kubwa ya vijana ambao wameshindwa kuendelea na masomo baada ya mitihani yao ya Kidato cha pili na Kidato cha nne.

 

89.         Mheshimiwa Spika, Idara ina jumla ya vikundi 64 vya programu za wanawake ambavyo 44 kati ya hivyo viko Unguja na 20 Pemba.  Vikundi hivyo vina jumla ya kinamama 757 ambao wanajishughulisha na shughuli mbali mbali za uzalishaji mali zikiwemo kilimo, ususi na ushoni.

 

90.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara inakusudia kuviimarisha zaidi vikundi hivyo kwa kuvipatia mafunzo ya ujasiriamali na utunzaji wa fedha.

 

Vyombo vya Habari

91.         Mheshimiwa Spika, vyombo vya habari ni nyenzo muhimu sana katika kuendeleza programu za Idara.  Katika mwaka 2012/2013, Idara imeweza kurusha hewani vipindi 19 vya redio kwa Unguja na 4 kwa Pemba.  Pia ilirusha hewani vipindi 5 vya Televisheni kwa Unguja na vipindi 4 kwa Pemba. Aidha Idara iliandaa makala tatu zilizochapishwa katika gazeti la Zanzibar leo.

 

92.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara itaendelea na juhudi za kuwaelimisha wananchi na wanakisomo kwa kutumia vyombo vya habari, vipeperushi, majarida, makongamano pamoja na kuzitumia maktaba zilizopo mjini na vijijini ipasavyo.

 

93.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Idara hii imepangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 252,000,000/- kwa Unguja na T.Sh. 50,000,000/- kwa Pemba kwa kazi za kawaida.

 

IDARA YA MAFUNZO YA UALIMU

94.         Mheshimiwa Spika, Idara ina jukumu la kusimamia mafunzo ya ualimu vyuoni na kazini. Mafunzo ya ualimu hutolewa katika vyuo vya ualimu vitatu ambavyo ni Chuo cha Kiislamu Mazizini, Chuo cha Kiislamu Micheweni na Chuo cha Benjamin William Mkapa Pemba. Vyuo hivi hutoa mafunzo ya Stashahada ya sanaa sekondari, Stashahada ya sayansi sekondari, Stashahada ya Ualimu Msingi, Stashahada ya Dini na Kiarabu na cheti cha ualimu wa Elimu Mjumuisho. Kwa mwaka 2012/2013, vyuo hivyo vilikuwa na jumla ya wanafunzi 745 (wanaume 161 na wanawake 584). Kati ya wanafunzi hao, wanafunzi 37 (wanawake ni 29 na wanaume 9) walichukua mafunzo ya cheti cha Ualimu wa Elimu Mjumuisho katika Chuo cha Kiislamu Mazizini. Jadweli namba 30 (a) – (c) zinatoa ufafanuzi zaidi.

 

95.         Mheshimiwa Spika, mtaala mpya wa mafunzo ya Stashahada ya Ualimu Msingi umeanza kutumika mwaka 2012/2013. Mtaala huo umeingiza masomo mapya yakiwemo teknolojia ya habari na mawasiliano (TEKNOHAMA), mafunzo ya amali, uongozi na michezo.

 

96.         Mheshimiwa Spika, Idara ilishirikiana na Taasisi ya Elimu kuendesha mafunzo kwa wakufunzi wa vyuo kuhusu uelewa na matumizi ya mtaala mpya wa Stashahada ya ualimu msingi.  Pia, UNESCO ilidhamini mafunzo kwa wakufunzi 75 Unguja na Pemba juu ya mbinu bora za ufundishaji ikiwemo ufundishaji wa uweledi na matumizi ya TEKNOHAMA. FAWE Zanzibar iliendesha mafunzo kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu juu ya mbinu za kufundisha kwa kuzingatia jinsia (gender responsive pedagogy). British Council iliendesha mafunzo maalum ya ufundishaji wa lugha ya Kiingereza katika vyuo na skuli za sekondari kwa walimu na wakufunzi wa lugha ya Kiingereza.

 

97.         Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha mafunzo ya ualimu, wanafunzi wapya watakaojiunga na Vyuo vya ualimu watasomeshwa Kiingereza cha mawasiliano kwa muda wa wiki nne kabla ya kuanza masomo waliyochagua. Lengo ni kuwapa msingi wa lugha ya Kiingereza ambayo itatumika kama lugha ya kusomeshea kuanzia darasa ya tano.

 

        Mafunzo ya Ualimu Kazini

98.         Mheshimiwa Spika, Vituo vimeendelea kutoa mafunzo ya ualimu kazini kwa mujibu wa mahitaji ya maeneo yao. Pia mafunzo ya ualimu kwa njia ya elimu masafa yameendelea kutolewa katika vituo tisa ambapo jumla ya walimu 675 (wanaume 119, wanawake 556) wamemaliza mafunzo ya cheti daraja la IIIA mwezi wa Aprili 2013.

 

99.         Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuimarisha ufundishaji wa masomo ya Sayansi, walimu saba walishiriki mafunzo mbali mbali yaliyotolewa na SMASSE huko Nairobi na walimu watatu wameshiriki mafunzo huko Lusaka, Zambia.

 

100.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Idara imeendesha mafunzo ya ualimu kazini.  Mafunzo yaliyotolewa ni kama ifuatavyo:-

i)     Walimu 150 wa sekondari (Unguja 100 na Pemba 50) wamepatiwa mafunzo ya kuinua uwezo wao wa kufundisha masomo ya Hisabati na Sayansi.

ii)    Walimu 468 (wanawake 276 na wanaume 192) wanaosomesha Kiingereza madarasa ya 5 na 6 walipata mafunzo ya kuinua lugha ya Kiingereza.

iii)  Walimu 387 (wanaume 151 na wanawake 236) wanaofundisha somo la Sayansi darasa la 5 na 6 walipatiwa mafunzo ya kukuza lugha ya Kiingereza na mawasiliano katika vituo 10 Unguja na Pemba.

iv)  Walimu 1,038 wa Hisabati na Sayansi katika skuli za msingi (Unguja 611 na Pemba 427) wamepatiwa mafunzo ya kuinua uwezo wao wa kufundisha masomo hayo.

v)    Walimu 16 walishiriki mafunzo ya lugha ya Kiingereza na mbinu za kufundisha kwa njia ya mtandao (online study).

vi)  Walimu wakuu 50 wa skuli teule za msingi na sekondari, maafisa wa elimu wilaya 6, waratibu wa vituo 5 na mkaguzi wa elimu 1 walipatiwa mafunzo ya siku 2 juu ya usimamizi wa mafunzo kazini.

vii) Walimu wa Kiingereza sekondari, wakufunzi wa vyuo, wakaguzi na washauri wa lugha 232 (wanaume 152 na wanawake 80) Unguja na Pemba walishiriki mafunzo ya kufundisha stadi ya kusikiliza kwa kutumia redio za kufundishia “life player” (MP3).

viii)  Mafunzo ya awali ya kompyuta yalitolewa kwa washiriki 20 ambao ni walimu wakuu na wasaidizi walimu wakuu wa skuli za Unguja.

ix)  Wakufunzi wa TAP 19 (Unguja 12 na Pemba 6) walipatiwa mafunzo maalumu.

 

101.      Mheshimiwa Spika, Idara imechukua juhudi za kuwaelimisha wafanyakazi wake. Wakufunzi wanane wa vyuo vya ualimu wamekwenda masomoni, wakufunzi watano wamejiunga na masomo ya shahada ya uzamili na wawili wamejiunga na shahada za uzamivu na mmoja shahada ya kwanza ya Elimu Mjumuisho. Wafanyakazi wawili walipata mafunzo ya uzamili kupitia Chuo Kikuu Huria. Pia wafanyakazi watatu wamepata mafunzo mafupi ya ufundishaji wa uongozi wa vijana, wafanyakazi 2 wamejiunga na Chuo cha Utumishi wa Umma kwa mafunzo ya cheti, na wafanyakazi wawili wameshiriki katika mafunzo mafupi nchini China na India.

 

102.      Mheshimiwa Spika, Idara inatarajia kukamilisha Sera ya Mafunzo ya Ualimu Kazini, kutoa mafunzo kwa walimu wa Sayansi na Hisabati kupitia mradi wa TAP na kuwafuatilia walimu wote waliopata mafunzo mbali mbali katika mwaka uliyopita.

103.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Idara imepangiwa kutumia jumla ya T. Sh. 250,000,000/- kwa Unguja na T.Sh. 50,000,000/- kwa Pemba.

 

          OFISI YA MKAGUZI MKUU WA ELIMU

104.      Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu inajukumu la kuzikagua skuli zote za Serikali na binafsi ili kufuatilia utekelezaji wa mitaala,  pamoja na   kutoa mafunzo mafupi na maelekezo kwa walimu wakuu na walimu juu ya kufanikisha kazi zao.

 

105.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu ilipanga kuzikagua skuli 300 zikiwemo za Serikali na binafsi na iliweza kukagua   skuli 321.

 

106.      Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la UNICEF imechapisha moduli 600 za viwango sanifu vya elimu ya msingi na kusambazwa katika skuli za serikali na binafsi.  Vile vile, Ofisi kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) imetayarisha moduli ya mafunzo ya ukaguzi kwa wakaguzi wapya. Moduli hiyo ilitumika kuwapa mafunzo mafupi wakaguzi wapya walioteuliwa na itatumika pia kwa watakaoteuliwa hapo baadaye.

 

107.      Mheshimiwa Spika, Ofisi ilifanya mapitio ya mfumo ya ukaguzi wa elimu hapa Zanzibar kwa kukusanya maoni ya wadau mbali mbali, wakiwemo wakaguzi, wajumbe wa bodi za elimu, kamati za skuli, waratibu wa vituo vya walimu, walimu wakuu, viongozi wa serikali za wanafunzi. Ripoti hio itasaidia katika kuandaa muundo mpya wa ukaguzi. 

108.      Mheshimiwa Spika, Katika kujenga uwezo wa wakaguzi, mafunzo mbali mbali yalitolewa yakiwemo mafunzo ya kompyuta na mafunzo ya ukuzaji mitaala.  Wakaguzi wanne walifanya ziara nchini Rwanda kujifunza na kuona mifumo mbali mbali ya ukaguzi wa skuli ambayo Rwanda inaitumia ili kuongeza maarifa yatakayosaidia katika kurekebisha mfumo wetu wa ukaguzi.

 

109.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu inatarajiwa kukagua skuli 342 zikiwemo skuli 267 za serikali na 75 za binafsi. Ili kuwa na usimamizi wa ukaguzi wa elimu wenye tija, Ofisi imelenga kuwawezesha walimu wakuu na wasaidizi walimu wakuu kufanya ukaguzi wa skuli (School Based Inspection) uliofanisi zaidi. Ofisi itaendelea kutoa mafunzo kwa walimu wakuu wapya, wasaidizi walimu wakuu na baadhi ya wakuu wa seksheni juu ya usimamizi na utekelezaji wa dhamana zao.  Pia Ofisi itatayarisha muundo mpya wa Ukaguzi pamoja na Sheria ya Ukaguzi.

 

110.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu imepangiwa ruzuku ya T.Sh. 106,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

          TAASISI YA ELIMU ZANZIBAR

111.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Taasisi ya Elimu Zanzibar, ilitoa mafunzo ya mtaala mpya wa stashahada ya ualimu kwa ngazi ya msingi kwa wakufunzi 56 wa vyuo vya ualimu. Vile vile, Taasisi iliwasilisha mtaala mpya wa Stashahada ya ualimu ngazi ya msingi kwa Baraza la Elimu.

 

112.      Mheshimiwa Spika, Taasisi iliendelea kutoa mafunzo ya awali ya matumizi ya mihutasari mipya ya msingi kwa walimu 720 wa darasa la nne kupitia vituo tisa vya walimu Unguja na Pemba. Mihutasari mipya ya madarasa ya 5 na 6 na mihutasari mipya ya maandalizi ilisambazwa kwa skuli zote za maandalizi na msingi za Unguja na Pemba. Pia, Taasisi ilifanya warsha ya uandishi wa vitabu kwa madarasa ya kwanza hadi la sita.

 

113.      Mheshimiwa Spika, Taasisi ilifanya ufuatiliaji na tathmini juu ya utekelezaji wa mihutasari ya darasa la kwanza katika skuli 72.  Taasisi ilitayarisha muongozo wa kuandaa Sera ya Ukuzaji Mitaala, Mpango wa Mafunzo kwa watumishi wa Taasisi, rasimu ya muongozo kwa ajili ya kutathmini vitabu na rasimu ya viwango vya kujifunza kwa elimu ya msingi kwa madarasa ya 1-4.

 

114.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Taasisi itaandika, kuchapisha na kusambaza vitabu vya kiada na miongozo ya walimu wa madarasa ya 5 na 6 kwa masomo 6 kati ya masomo 12. Pia itaandaa viwango vya kujifunza kwa elimu ya msingi kwa madarasa ya 5 na 6. Aidha, Taasisi itaandaa mtaala wa stashahada kwa walimu wa maandalizi na mtaala wa mafunzo kazini ya wasaidizi wa maabara wa skuli za sekondari.

 

115.      Mheshimiwa Spika, Taasisi vile vile itabuni vifaa vya kufundishia masomo ya Sayansi na Hisabati, itavifanyia uhariri vitabu vya wanafunzi wa skuli za maandalizi pamoja na kuendesha mafunzo ya uandishi na utunzaji wa vitabu kwa washauri wa masomo. Aidha, Taasisi itafanya utafiti juu ya sababu ya matokeo mabaya ya mitihani kwa masomo ya Sayansi na Hisabati kwa skuli za msingi na sekondari.

 

116.      Mheshimiwa Spika, Taasisi inakusudia kukamilisha Sheria ya kuanzishwa kwake na kuandaa mpango mkakati pamoja na kutayarisha muongozo wa utaratibu wa utoaji wa elimu ya sekondari utakaokidhi mahitaji ya Sera ya Elimu ya mwaka 2006. 

 

117.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Taasisi imepangiwa ruzuku ya T. Sh. 100,000,000/- kwa kazi za kawaida.

    

MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI

118.      Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Mafunzo ya Amali ina majukumu ya kutoa, kusimamia na kuratibu shughuli zote za mafunzo ya amali hapa Zanzibar. 

 

119.      Katika mwaka 2012/2013, jumla ya wanafunzi 784 (269 wanawake na 515 wanaume) wanapatiwa mafunzo ya amali katika Vituo vya Mafunzo ya Amali Mkokotoni, Vitongoji na Mwanakwerekwe. Wanafunzi hawa wanajifunza katika fani mbali mbali za ufundi.  Jadweli namba 40(a) inatoa ufafanuzi zaidi.

 

120.      Mheshimiwa Spika, Mamlaka pia inaratibu shughuli mbali mbali za maendeleo ya mafunzo ya amali ikiwemo Mitihani ya Taifa ya Uhasibu na Biashara (NABE), mitihani ya ufundi stadi “Trade Test” na “Competency Based Education and Training” (CBET) inayotahiniwa na Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) ya Tanzania Bara. Jumla ya wanafunzi 428 (102 wanawake na 326 wanaume) walifaulu ikiwa ni sawa na asilimia 95. Wanafunzi 265 (wanawake 63) walifaulu mitihani ya “Competency Based Education and Training” kati ya vijana 302 (wanawake 73) waliofanya mitihani hiyo, ikiwa ni sawa na asilimia 87.7. Jadweli namba 41 (c) na (d) zinatoa ufafanuzi zaidi.

 

121.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2012/2013, Mamlaka imeendelea kusajili vituo vinavyotoa mafunzo ya amali vya Zanzibar vya umma na binafsi.  Jumla ya vituo vya amali 63 vimekaguliwa na 21 kati yao vimesajiliwa katika hatua mbali mbali. Jadweli namba 40 (b) inatoa ufafanuzi zaidi.

 

122.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Mamlaka ina malengo makuu mawili ambayo ni kuimarisha Mamlaka ya Mafunzo ya Amali na kuimarisha utoaji wa mafunzo ya amali. Katika kufikia malengo hayo, Mamlaka inakusudia kuzipitia na kuzifanyia marekebisho Sera ya Elimu na Mafunzo ya Amali ya 2005 na Sheria ya Mafunzo ya Amali namba 8 ya 2006 iliyofanyiwa marekebisho 2007. Pia, inakusudia kuajiri wafanyakazi wapya, kuvipatia vituo vya mafunzo ya amali vifaa na zana za kutendea kazi na kuongeza ujuzi na utaalamu wa walimu wake. Aidha, Mamlaka inakusudia kuimarisha uzalishaji na uwekezaji kwa lengo la kuongeza mapato yake.

 

123.      Mheshimwa Spika, Kwa mwaka 2013/2014, Mamlaka ya Mafunzo ya Amali imepangiwa ruzuku ya T. Sh. 2,300,000,000/-.

 

 

 

        TAASISI ZA ELIMU YA JUU

124.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, zilikuwepo jumla ya taasisi nne za elimu ya juu. Kati ya taasisi hizo, mbili zinamilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambazo ni Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar na Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia na taasisi binafsi ambazo ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chukwani na Chuo Kikuu cha Zanzibar.

 

          CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR

125.      Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kimepata mafanikio makubwa tangu kuanzishwa kwake miaka kumi na mbili iliyopita.  Kwa sasa Chuo kina jumla ya wanafunzi 703 wa shahada ya kwanza katika fani ya sayansi na ualimu, sanaa na ualimu na sayansi na kompyuta. Kati yao wanafunzi 365 ni wanaume na 338 ni wanawake. Vile vile, Chuo kina jumla ya wanafunzi 892 katika ngazi ya Stashahada ya sayansi na ualimu, lugha na ualimu, sayansi na kompyuta na habari na mawasiliano. Kati yao wanaume ni 340 na wanawake ni 552. Katika mwaka wa masomo 2012/2013, Chuo pia kimeanzisha Stashahada ya kozi za jamii ambapo wanafunzi 46 wamejiunga na kozi hiyo. Jadweli Namba 26(a) inatoa ufafanuzi.

 

126.      Mheshimiwa Spika, Chuo kimefanya mabadiliko ya mfumo wake kwa kuwa na skuli nne badala ya skuli moja na kuweka Idara na vitengo mbali mbali. Skuli zenyewe ni Skuli ya Elimu Endelezi na Utaalamu, Skuli ya Elimu, Skuli ya Kiswahili na Lugha za Kigeni na Skuli ya Sayansi Asili na Jamii. Chuo kupitia skuli ya elimu endelezi na utaalamu inatoa huduma za kuwapatia elimu wananchi katika fani mbali mbali zikiwemo Ukutubi, Kompyuta, Lugha ya Kiingereza na Kichina na masomo ya Benki.

 

127.      Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Taifa kimeanzisha kozi ya uzamivu ya Kiswahili (PhD) na kwa sasa wanafunzi wanane wamejiunga na kozi hiyo. Pia, skuli inafundisha Kiswahili kwa wanafunzi wa kigeni ambapo kwa mwaka wa masomo 2012/2013 jumla ya wanafunzi wageni 163 (wanaume 105 na wanawake 58) wamejiunga kujifunza lugha ya Kiswahili.

                  

128.      Mheshimiwa Spika, Chuo kilifanya mahafali yake ya nane tarehe 22 Disemba, 2012. Katika mahafali hayo, Mkuu wa Chuo ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohammed Shein aliwatunuku shahada, stashahada na vyeti wahitimu 504, wanaume 233 na wanawake 261 katika fani mbali mbali. Miongoni mwao, wanafunzi 208 walitunukiwa shahada ya sanaa na elimu, wanafunzi 46 walitunukiwa shahada ya sayansi na elimu, wanafunzi 17 walitunukiwa shahada ya sayansi ya kompyuta. Vile vile wanafunzi 121 walitunukiwa stashahada ya mawasiliano na habari, wanafunzi 13 walitunukiwa vyeti vya kompyuta, 23 vyeti vya ukutubi na 21 vyeti vya habari na mawasiliano.

 

129.      Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kimehamishia shughuli zake katika kampasi ya Tunguu. Uzinduzi wa kampasi hii ulifanywa na Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa niaba ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi tarehe 20 Juni, 2013.  Tunaishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na BADEA kwa michango iliyotolewa katika kufanikisha mradi huu na kukiweka Chuo katika mazingira mazuri ya kufundishia, kujisomea na kufanyia kazi.

 

130.      Mheshimiwa Spika, kutokana na ushirikiano ulioanzishwa kati ya Wizara na Wizara ya Elimu ya Juu ya Oman, Chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar kimepata msaada wa ufadhili wa masomo ya juu kupitia “Sultan Qaboos Academic Fellowship (SQAF)”.  Pia, Wizara ya Elimu ya Juu ya Oman imekubali kusaidia mafunzo ya walimu wa sekondari katika nyanja za Sayansi, Hisabati na Kiingereza ambayo yataendeshwa na wataalamu wa Chuo Kikuu chetu.

 

131.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Chuo kimeajiri wafanyakazi 35 kati yao 12 wanataaluma na 23 wafanyakazi wa uendeshaji. Vile vile chuo kimeendelea kuwalipia ada za masomo wafanyakazi wake 56 ambao wapo masomoni kwa ngazi na fani tofauti.

 

132.  Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Chuo kina lengo ya kuanzisha skuli ya Tiba kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na wanataaluma kutoka Cuba. Pia kitaanzisha kozi mpya zikiwemo shahada ya uzamili ya Kiswahili, shahada ya uzamili ya sayansi kemia na Stashahada ya afya ya mazingira. Vile vile, chuo kitajenga kituo cha afya, kitafanya ukarabati wa mkahawa na kuweka kituo kidogo cha Polisi huko Tunguu. Aidha, Chuo kinakusudia kuyafanyia ukarabati majengo ya kampasi za Vuga na Nkrumah kwa kuimarisha miundombinu ya maji na dakhalia za wanafunzi.  Vile vile, Chuo kinakusudia kuanzisha TV Channel (SUZA TV) kwa kutumia mfumo wa digitali kwa ajili ya kutoa elimu kwa jamii.

 

133.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Chuo kimetengewa ruzuku ya T.Sh. 4,900,000,000/- kwa kazi za kawaida

 

TAASISI YA KARUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

134.      Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia ni taasisi inayotoa huduma za kielimu za uhandisi katika ngazi ya stashahada (NTA 6). Mafunzo ya uhandisi ambayo yanatolewa katika ngazi ya stashahada ni uhandisi mitambo, uhandisi magari, uhandisi ujenzi na usafirishaji, uhandisi mawasiliano ya anga, elektroniki na kompyuta na uhandisi umeme.

 

135.      Mheshimiwa Spika, Taasisi ina jumla ya wafanyakazi 96, wakiwemo wakufunzi 51 (wanaume 31 na wanawake 20) na wafanyakazi wasiokuwa wakufunzi 28 (wanaume 18 na wanawake 10). Pia kuna wafanyakazi ambao si wa kudumu wakiwemo wakufunzi watano wa muda, wafanyakazi 10 wa mkataba na wawili kutoka Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo.

 

136.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Taasisi ilifanya usajili wa wanafunzi 272, kati yao wanaume 219 na wanawake 53 kwa Idara zote, ambazo wanachukuwa stashahada ya uhandisi. Jadweli Namba 29 inatoa ufafanuzi zaidi.  Kwa upande wa mafunzo ya kujiendeleza ya ufundi stadi, stashahada ya ICT, mafunzo ya Sayansi na Hisabati kwa elimu ya msingi na kidato cha nne jumla ya wanafunzi 996 wanahudhuria mafunzo hayo wakiwemo wanaume 798 na wanawake 198.  Hali hii inafanya Taasisi ya Karume iwe na jumla ya wanafunzi 1,215.

 

137.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Taasisi ilifanya ukarabati wa miundo mbinu ya maji safi katika eneo lote la Taasisi, kukarabati dakhalia za wanafunzi wa kike na kiume kwa kuweka vyoo vipya, wavu wa mbu na vyandarua, kukamilisha ujenzi wa madarasa mapya matatu na ofisi mbili za walimu. Pia, Taasisi, ilianzisha mafunzo mapya ya walimu wa Sayansi na Hisabati ngazi ya msingi, mafunzo ya ICT, kuimarisha mafunzo ya matayarisho kwa wanafunzi wa NTA na kuendeleza mafunzo ya amali. Pia Taasisi ilifanya tathmini ya miaka mitano ya Taasisi juu ya utoaji wa huduma za elimu.

 

138.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Taasisi inakusudia kutekeleza malengo makuu sita. Malengo hayo ni uendelezaji wa matengenezo ya majengo ya Taasisi, kuongeza mashirikiano na Taasisi rafiki za elimu za ndani na nje ya nchi, kuanzishwa kwa mafunzo mapya ya kuiendeleza Taasisi na yale ya kuisaidia jamii kwa kutumia Sayansi na Teknolojia kama vile ya” business incubator” na kuwaendeleza walimu wa Sayansi wa Sekondari, kuanzisha shughuli za utafiti, kuandaa mpango kazi wa miaka mitatu ijayo na kufanya uhakiki wa mali za Taasisi (fixed asset valuation).

 

139.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Taasisi imetengewa ruzuku ya T.Sh. 1,366,000,000/-.

 

 

CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR

140.      Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka 2012/2013, Chuo Kikuu cha Zanzibar kilikuwa na jumla ya wanafunzi 1,297 kati yao wanaume ni 659 na wanawake 638.  Wanafunzi 395 wanasomea shahada ya kwanza ya Sheria na Sharia, 317 Shahada ya Biashara, 333 Shahada ya Uongozi wa Umma, 132 Shahada ya Uchumi, 120 Shahada ya mawasiliano ya Kompyuta na Biashara. Pia wapo wanafunzi 554 wa masomo ya ngazi za Diploma.  Jadweli namba 28 inatoa uchambuzi zaidi. Chuo kina wahadhiri 39 wazalendo na 8 kutoka nchi za nje.  Wahadhiri wanne wazalendo wapo masomoni katika kiwango cha shahada ya uzamivu na jitihada zinaendelea kuwapeleka wahadhiri wengine masomoni kwa lengo la kukiwezesha chuo kujitosheleza kwa wahadhiri wake. Wahadhiri wawili wamekamilisha masomo yao hivi karibuni na tayari wamerejea na kuendelea na kazi.

 

141.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa masomo 2013/2014, Chuo kitaanzisha mafunzo ya Shahada ya Uzamili katika Uongozi wa Umma na Sayansi ya Uchumi na Fedha. Pia kinatarajia kuanza kutoa mafunzo ya shahada ya kwanza katika fani za “Islamic Banking and Finance”, “Procurement and Logistics Management” na “IT with Education” ili kuendana na kasi ya maendeleo ya nchi na mahitaji ya wataalam

 

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU CHUKWANI

142.      Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu kiliopo Chukwani kinaendelea kuimarika katika kukuza taaluma na ujenzi wa majengo mapya. Chuo kimekamilisha ujenzi wa jengo la madarasa na ofisi ya ghorofa moja. Ujenzi wa jengo la kuishi wafanyakazi ambalo lina uwezo wa kuishi familia sita umefikia asilimia 98 ya ukamilishaji wake.

 

143.      Mheshimiwa Spika, Chuo kina jumla ya wanafunzi 1,523 wakiwemo wanawake 915 na wanaume 608. Wanafunzi 1,328 wanasoma shahada ya kwanza ya ualimu na 195 wapo katika mafunzo ya matayarisho (Pre-university course) ya kujiunga na shahada ya kwanza. Jadweli Nmaba 27 inatoa ufafanuzi zaidi.

 

144.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa masomo 2012/2013, wanafunzi 242 wakiwemo wanawake 84 na wanaume 158 walihitimu masomo yao. Chuo kimekamilisha taratibu mbali mbali za kukipandisha daraja ili kiwe Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Zanzibar (Zanzibar International University) badala ya kuwa tawi la Chuo Kikuu cha Kimataifa kilichopo Sudan. Taratibu zinaendelea kwa Chuo kupata kibali kutoka Kamisheni ya Vyuo Vikuu Tanzania.

 

145.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa masomo wa 2013/2014, Chuo kimepanga kusajili wanafunzi 700 wa fani mbali mbali na kuajiri wahadhiri sita ili kuondosha tatizo la kutumia wahadhiri wa muda. Pia, Chuo kimekusudia kufanya matengenezo ya Kituo cha Afya ili kiweze kuimarisha huduma zake na kuweka vifaa vya kisasa. Vile vile,

 

BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU.

146.      Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar ni chombo kilichopewa jukumu la kuwapatia mikopo ya gharama za elimu wanafunzi na wafanyakazi wanaojiunga na vyuo vya elimu ya juu. Aidha Bodi hiyo pia imepewa jukumu la kukusanya madeni kutoka kwa wanafunzi waliohitimu masomo yao kuanzia mwaka 2006 na kuanza kazi.

 

147.      Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2012/2013, Bodi iliwapatia mikopo wanafunzi wapya 881. Bodi pia imewalipia ada ya masomo na posho la kujikimu wanafunzi 161 wanaoendelea na masomo katika vyuo vya nje na wanafunzi 851 wanaoendelea na masomo kwa vyuo vya ndani ya Tanzania. Jumla ya wanafunzi waliohudumiwa kwa mikopo kwa mwaka 2012/2013 ni 1,897. Jadweli namba 25(a) – (b) zinatoa ufafanuzi.  

 

148.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Bodi inakusudia kutoa mikopo kwa vijana wapya 1,000, kati ya hao, 850 wa shahada ya kwanza, 185 wa shahada ya uzamili na 15shahada ya tatu. Idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 25 ikilinganisha na wanafunzi 800 waliopangwa katika mwaka 2012/2013. Vijana 363 wanatarajiwa kumaliza masomo yao katika vyuo mbali mbali vya ndani na nje ya nchi katika mwaka huu.   

 

149.      Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imeendelea na kukusanya marejesho ya mikopo kutoka kwa wahitimu wa taasisi za elimu ya juu waliopatiwa mikopo. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2013, jumla ya T. Sh. 105,167,000/- zimekusanywa kutoka kwa wanafunzi waliohitimu na kuajiriwa. Kiwango hicho ni kikubwa ukilinganisha na makusanyo ya T.Sh. 8,200,000/- kilichofikiwa katika mwaka 2011/2012. Katika mwaka 2013/2014, juhudi zaidi zitachukuliwa kuongeza kasi ya marejesho ya madeni.

 

150.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Bodi imepangiwa ruzuku ya T. Sh. 9,113,000,000/- kwa ajili ya udhamini wa wanafunzi wapya na wanaoendelea pamoja na gharama za uendeshaji.

 

BARAZA LA MITIHANI LA ZANZIBAR.

151.      Mheshimiwa Spika, Baraza la Mitihani la Zanzibar lina jukumu la kusimamia shughuli zote zinazohusu mitihani ya SMZ ikiwemo utungaji, uchapishaji, usimamizi na usahihishaji wa mitihani ya darasa la saba, kidato cha pili na mafunzo ya Ualimu stashahada ya msingi na Dini na Kiarabu. Pia Baraza lina jukumu la kutathmini mwenendo mzima wa malengo ya utowaji elimu pamoja na kutathmini mwenendo wa mitihani hiyo.

 

152.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Baraza lilisimamia ufanyaji wa mitihani ya SMZ ambapo jumla ya skuli za msingi 233 (114 Unguja, 74 Pemba) zilifanya mitihani ya darasa la saba na skuli 188 (114 Unguja, 74 Pemba) zilifanya mtihani wa kidato cha pili. Jumla ya wanafunzi 23,039 walifanya mtihani wa darasa la saba katika mwezi Novemba 2012, kati yao wanafunzi 1,501 sawa na asilimia 6.5 walichaguliwa kuingia  mchepuo katika skuli mbali mbali za Zanzibar.  Kwa upande wa mtihani wa kidato cha pili kati ya wanafunzi 19,679 waliofanya mtihani wanafunzi 11,195 ikiwa ni sawa na asilimia 56.9 walifaulu na kuchaguliwa kuendelea na masomo kidato cha tatu. Jadweli namba 31 na 32 inatoa ufafanuzi zaidi.

 

153.      Mheshimwa Spika, kwa upande wa mtihani ya Taifa wa kidato cha nne, kati ya wanafunzi 13,051 wa skuli za Serikali na binafsi waliofanya mtihani huo mwezi wa Oktoba 2012, wanafunzi 6,935 wamefaulu ikiwa ni sawa na asilimia 53.1. Kiwango cha ufaulu kwa kidato cha nne kimeshuka ikilinganishwa na matokeo ya 2011 ambapo asilimia ya ufaulu ilikuwa 75.9. Aidha, kati ya wanafunzi waliofaulu, wanafunzi 1,054 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika skuli za Serikali mwaka 2013/2014, wakiwemo 719 kutoka skuli za Serikali, 60 wa skuli za binafsi na 275 wanafunzi wa faragha. Jadweli namba 22 inatoa ufafanuzi zaidi.

 

154.      Mheshimiwa Spika, kati ya wanafunzi 2,067 waliofanya mtihani wa kidato cha sita mwezi Februari 2013, wanafunzi 1,636 sawa na asilimia 79.1 walifaulu. Kiwango hiki cha ufaulu kimepanda ikilinganishwa na matokeo ya Februari 2012 ambapo asilimia ya ufaulu ilikuwa 74.0. Jadweli namba 6 (c) iii inatoa ufafanuzi zaidi.

 

155.      Mheshimiwa Spika, kwa  upande wa mitihani ya Ualimu ya Juni 2012, kati ya wanafunzi 68 waliofanya mtihani wa marudio  ya Stashahada ya Ualimu Dini ya Kiarabu na Stashahada ya msingi katika Chuo cha Kiislamu Mazizini, Chuo cha Kiislamu Kiuyu Micheweni na Benjamin William Mkapa, wanafunzi 54 sawa na asilimia 79.4% walifaulu na wanafunzi 14 hawakufaulu mitihani yao.  Jumla ya wanafunzi 110 wamefanya mitihani ya ualimu ngazi ya Stashahada  ya Sekondari  ya Baraza la Mitihani la Tanzania mwezi wa Mei 2013 na wanafunzi 263 wamefanya mitihani ya ualimu ya Stashahada ya Msingi na Dini na Kiarabu ya  Baraza mwezi Juni, 2013.

 

 

156.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Baraza limepanga kufanya tathmini ya mtaala mpya wa elimu ya msingi ambapo wanafunzi wa darasa la nne watafanyiwa mtihani wa pamoja ili kujua ufanisi wa mtaala husika. Katika kufanikisha shughuli hii Baraza litaandaa mitihani ya masomo ya Hisabati, Kiingereza, Kiswahili, Sayansi na Elimu jamii. Stadi zitakazopimwa kwenye tathmini hii ni kuangalia kwa kiasi gani mwanafunzi anaweza kusoma, kuandika na kuhesabu.    

         

157.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Baraza limekusudia kuimarisha taratibu za usimamizi wa mitihani ya SMZ, ikiwemo kuendelea kuweka kumbukumbu zote za wanaotarajiwa kufanya mtihani katika mfumo wa kompyuta na kuongeza udhibiti wa mitihani hiyo. Pia, Baraza litakamilisha kanuni  na miongozo ya uendeshaji wa mitihani kwa mujibu wa Sheria ya Baraza. 

 

158.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014, Baraza limetengewa ruzuku ya T.Sh. 1, 570, 000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

BODI YA HUDUMA ZA MAKTABA

159.      Mheshimiwa Spika, Bodi ya Huduma za Maktaba ni chombo kinachotekeleza majukumu yake kupitia Shirika la Huduma za Maktaba.  Chombo hiki kina jukumu la kuanzisha, kusimamia na kusambaza huduma za maktaba Unguja na Pemba.

 

160.      Mheshimiwa Spika, Shirika linaendelea kushajiisha na kutoa ushauri juu ya kuanzisha maktaba katika maeneo mbali mbali yakiwemo maeneo ya skuli na maeneo ambayo jamii zinaishi. Katika mwaka 2012/2013, skuli zilizomo katika mradi wa maktaba za sanduku zimeongezeka kufikia 35 kutoka skuli 25 mwaka 2011/2012. Katika mwaka 2013/2014, Shirika linategemea kuongeza skuli 20 nyengine zitakazoingia katika mradi wa maktaba za sanduku.

 

161.      Mheshimiwa Spika, Shirika kwa kushirikiana na jumuiya isiyo ya kiserikali MJUKIZA limeanzisha utaratibu wa kuwa na maktaba za jamii.  Maktaba hizi zinasaidia sana kutoa huduma kwa jamii kwa ukaribu zaidi.  Hadi hivi sasa, ziko maktaba 8 za jamii katika maeneo ya Chumbuni, Welezo, Kiembesamaki, Mpapa, Uzini, Fumba, Bweleo na Tumbatu. Aidha, Shirika linaendelea kugawa vitabu vya kiada na ziada katika taasisi mbali mbali za elimu zikiwemo skuli za msingi, sekondari, vyuo na vituo vya walimu.

 

162.      Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuwasaidia watoto kuandika, kusoma na kujifunza, Shirika linaendesha programu ya watoto ndani ya Maktaba Kuu ya Maisara Unguja na Maktaba Kuu ya Chachani Chake chake Pemba.  Aidha, programu hii huendeshwa katika skuli husika, hususan kwa skuli ambazo ziko nje ya mji.  Idadi ya wanachama imekuwa ikiongezeka siku hadi siku. Kwa mwaka 2012/2013 idadi imefikia 18,360, kati yao 17,391 kwa Unguja na 969 kwa Pemba .Kwa mwaka 2013/2014 Shirika linatarajia kuendesha programu 80 nchini kote. 

 

163.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Shirika limetengewa ruzuku ya  T.Sh. 400, 000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

 

KITENGO CHA UHASIBU

164.      Mheshimiwa Spika. Kitengo kimesimamia ulipaji wa mishahara ya wafanyakazi wote wa Wizara pamoja na mahitaji mengine ya Wizara.  Kwa upande wa fedha za maendeleo, Kitengo kimesimamia ulipaji wa fedha za wakandarasi na wazabuni wa ujenzi na wazabuni wa vifaa na huduma mbali mbali. Kitengo kimekuwa na mashirikiano mazuri na Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo katika matumizi ya mtambo wa IFMS  ambao husaidia kwa kiwango kikubwa usimamizi wa matumizi kwa mujibu wa bajeti ya Wizara na hivyo kuimarisha udhibiti wa fedha za umma.

                  

165.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Kitengo kitaendelea kusimamia matumizi yote ya fedha za kawaida na fedha za maendeleo kwa mujibu wa  bajeti iliyotengwa. Aidha, Kitengo kinakusudia kutoa mafunzo kwa wahasibu na wakuu wa vitengo kuhusu usimamizi wa fedha. Kitengo pia kitatoa mafunzo kwa wakurugenzi na maofisa mipango wa Idara zote za Wizara juu ya utayarishaji wa bajeti kwa mfumo wa “Medium Term Expenditure Framework” na Program Based Budgeting.”

 

Kwa mwaka 2013/2014, Kitengo kimepangiwa kutumia jumla ya T.Sh. 66, 000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA UHUSIANO

166.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2012/2013, Kitengo cha Habari Elimu na Mahusiano kiliendelea kutekeleza majukumu ya kuratibu shughuli za utoaji habari za Wizara na mahusiano ya Wizara na taasisi na nchi mbali mbali katika nyanja ya elimu. Miongoni mwa shughuli zilizotekelezwa katika kukuza na kuimarisha mashirikiano na nchi mbali mbali ni kukutana na mabalozi wa nchi za nje waliopo Tanzania pamoja na kuhudhuria mikutano na makongamano ya kimataifa.

 

167.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013 niliweza kukutana na na kufanya mazungumzo na mabalozi wa Nigeria, Misri, India, Iran, Sudan, China, Uingereza na Cuba. Kwa upande wa mashirika ya Kimataifa ni USAID, UNICEF, UNESCO na Global Partnership for Education (GPE). Aidha, nilihudhuria mikutano na makongamano mbali mbali, miongoni mwao ni “Education World Forum” huko London Uingereza na Mkutano wa Mawaziri wa Elimu wa Nchi za Jumuiya ya Madola huko Mauritius. Pia, nilitembelewa na Mheshimiwa Dk. Rawya Saud Al-Busaidi, Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman ambae alifanya ziara ya siku sita hapa Zanzibar. Katika ziara hiyo tumeweza kuzungumzia utelezaji wa mkataba wa maelewano baina ya pande zetu uliotiwa saini mwaka 2012 nchini Oman wakati wa ziara ya Mheshimiwa Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na kuzindua mradi wa utoaji mafunzo wa SQAF. Pia niliweza kukutana na Mheshimiwa Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Tanzania Bara na kujadiliana masuala mbali mbali ya kuendeleza elimu katika sehemu zetu mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Napenda kumshukuru sana kwa mashirikiano makubwa anayonipa.

 

168.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kimeweza kutangaza maendeleo ya Wizara kwa kupitia vyombo vya habari vya hapa nchini, pia kimeandaa kipindi cha kusheherekea miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Vile vile kwa kushirikiana na BBC Swahili tumeweza kurusha kipindi cha kwanza cha TV kiitwacho Haba na Haba.

 

169.      Kwa mwaka wa 2013/2014, Kitengo kitaendelea kuratibu mashirikiano na kutoa habari za maendeleo ya Wizara pamoja na kutayarisha programu maalum ya miaka 50 ya maendeleo ya elimu Zanzibar.

 

Katika mwaka wa 2013/2014, Kitengo kinatarajia kutumia jumla ya T.Sh. 50,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

KITENGO CHA UNUNUZI NA UGAVI

170.      Mheshimiwa Spika, Kitengo cha Ununuzi na Ugavi kimeendelea kufanya kazi zake vizuri.  Katika mwaka 2012/2013, Kitengo kwa kushirikiana na Bodi ya Zabuni ya Wizara kilitayarisha, kutangaza na kuzifanyia tathmini jumla ya zabuni 39 za manunuzi ya bidhaa, huduma na kazi za ujenzi zenye thamani ya jumla ya T.Sh. 14,089,000,000/-.

 

171.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Kitengo kinakusudia kutayarisha, kutangaza na kuzifanyia tathmini zabuni za ujenzi na ununuzi wa vifaa. Pia kitengo kitatangaza zabuni za kutafuta washauri elekezi kwa kazi mbali mbali za Wizara.

 

Katika mwaka 2013/2014, Kitengo kinatarajia kutumia jumla ya T.Sh. 55,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

 

 

KITENGO CHA UKAGUZI WA HESABU ZA NDANI

172.      Mheshimiwa Spika, Kitengo hiki kina jukumu la kukagua hesabu zinazohusiana na matumizi pamoja na mapato katika Taasisi na Idara zote za Wizara.  Kitengo pia kinafanya ukaguzi wa kuangalia michango yote inayotolewa na wazee na wanafunzi kwa skuli zote za Unguja na Pemba. Kwa mwaka 2012/2013, Kitengo kimeweza kukagua hesabu zote za fedha za kawaida na fedha za maendeleo kuanzia Makao Makuu ya Wizara pamoja na kufuatilia vifaa vilivyopelekwa katika skuli mbali mbali ambavyo hununuliwa kutokana na bajeti husika ya mwaka wa fedha na pia fedha za miradi ya maendeleo kulingana na thamani halisi ya bidhaa zilizopokelewa na ujenzi uliofanyika. 

 

173.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kimeweza kuzifanyia ukaguzi skuli 194 zikiwemo 120 za Unguja na 74 za Pemba. Pia Kitengo kimefanya ukaguzi wa Taasisi tano ambazo hupatiwa ruzuku. Taasisi hizo ni Shirika la Huduma za Maktaba, Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, Mamlaka ya Mafunzo ya Amali, Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia na Taasisi ya Elimu Zanzibar.  Kitengo i pia kilifanya ukaguzi katika Ofisi ya Wizara Pemba. Aidha, Kitengo kinaratibu vikao vya kamati ya ukaguzi wa hesabu za ndani (Audit Committee) ambayo hupokea na kujadili ripoti za ukaguzi kwa kila robo mwaka.

 

174.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Kitengo kitaendelea kufanya ukaguzi wa mahesabu ya Taasisi na Idara zote za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali pamoja na Taasisi na skuli zake mbali mbali za Unguja na Pemba. Pia kitengo kitaendelea na utaratibu wake wa kutoa mafunzo ya uwekaji wa kumbukumbu za hesabu na uwekaji wa rekodi za vitabu kwa  wenyeviti wa kamati za skuli, walimu wakuu wa skuli pamoja na washika fedha wa skuli ili kuwajengea uelewa kuhusiana na kazi zao.  Pia, Kitengo kitakagua jumla ya skuli 200.

 

Katika mwaka 2013/2014, Kitengo kinatarajia kutumia jumla ya T.Sh. 60,000,000/- kwa ajili ya kazi za kawaida.

 

KITENGO CHA URATIBU WA ELIMU YA JUU

175.      Mheshimiwa Spika, Kitengo hiki kiliendelea na jukumu lake la kuratibu maendeleo ya elimu ya juu na kuwa na mashirikiano ya karibu na Idara ya Elimu ya Juu ya Tanzania Bara na taasisi nyengine za elimu ya juu. Katika mwaka 2012/2013, Kitengo kimetangaza nafasi za masomo kutoka nchi za Oman, Jumuiya ya Madola, China, Egypt, Cuba, Russia, Misri na Algeria.  Jumla ya wanafunzi 20 wamewasilisha maombi ya masomo nchini Oman, wanafunzi 3 Jumuiya ya Madola, wanafunzi 20 nchini China, Algeria 15, Cuba 9, Russia 2 na Misri 2.

 

Aidha, Kitengo kimeweka kumbukumbu za wahitimu wanaorejea masomoni. Jumla ya wanafunzi 536 waliomaliza masomo katika fani mbali mbali wameripoti wakiwemo wanaume 286 na wanawake 250. Wahitimu hao wamepelekwa Tume ya Utumishi kwa ajili ya kutafutiwa ajira.

 

176.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Kitengo kinatarajia kufanya mikutano na Taasisi mbali mbali za elimu ya juu ili kujadili maendeleo ya mipango ya Taasisi hizo, kuendelea kuratibu nafasi za masomo ndani na nje ya nchi na kuweka kumbukumbu za wahitimu wanaorudi masomoni.

 

177.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Kitengo kimepangiwa jumla ya T.Sh. 50,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

KITENGO CHA ELIMU MJUMUISHO NA STADI ZA MAISHA

178.      Mheshimiwa Spika, Kitengo cha Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha kimepewa dhamana ya kusimamia na kuhakikisha kwamba lengo la Elimu kwa Wote linafikiwa kwa watoto wote kupata haki yao ya msingi ya elimu  wakiwemo  wenye mahitaji maalum, kutoa ushauri nasaha, kusimamia mapambano dhidi ya UKIMWI na madawa ya kulevya na kuwapatia stadi za maisha walimu na wanafunzi.

 

Elimu Mjumuisho

179.      Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2012/2013, Kitengo kilitoa mafunzo mbali mbali kwa walimu wa skuli ili waweze kuwafundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum katika madarasa ya kawaida kwa ufanisi.  Miongoni mwa mafunzo hayo ni ya maandishi ya nukta nundu, lugha ya alama na mbinu mbali mbali za urekebishaji wa tabia za wanafunzi.  Jumla ya walimu 689 wa Unguja na Pemba walifaidika na mafunzo yaliyotolewa. Aidha, mafunzo ya elimu mjumuisho yalitolewa kwa walimu 176 wa skuli binafsi za Unguja.

 

180.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kilishirikiana na Kitengo cha Elimu Maalum cha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi cha Tanzania Bara katika kutafsiri kivunge (Toolkit) cha moduli sita ambacho kiliandaliwa na UNESCO kwa matumizi ya nchi za Mashariki ya mbali.  Tool-kit” hiyo, ilifanyiwa marekebisho ili iendane na mazingira ya Tanzania na iweze kutumika katika kuandaa mazingira rafiki ya ufundishaji na ujifunzaji.  Pia, Kitengo kimefanya ufuatiliaji wa skuli zinazotekeleza programu ya elimu mjumuisho kwa lengo la kutathmini utekelezaji wake. Jumla ya skuli 35 (26 za Unguja na skuli 9 za Pemba) zilihusika na ufuatiliaji huo.

 

181.      Mheshimiwa Spika, katika kuhamasisha na kuelimisha jamii katika suala zima la elimu mjumuisho, vipindi kumi vya radio vilirushwa kupitia Shirika la Utangazaji la Zanzibar ambapo wananchi walipata fursa ya kuchangia kuhusu maendeleo ya elimu mjumuisho katika skuli zetu.  Aidha, Kitengo kimefanya utafiti wa kupata takwimu za wanafunzi wenye mahitaji mbali mbali ya kielimu, wakiwemo wenye ulemavu katika skuli 334 za Serikali za Unguja na Pemba kati ya skuli zote 420. Jumla ya wanafunzi 73,241 wamegunduliwa kuwa na mahitaji maalumu, miongoni mwao 37,152 wa kike na 36,089 wa kiume.

 

182.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kinaendelea kuwapatia mafunzo watendaji wake ili kuwajengea uwezo zaidi katika utendaji wa kazi zao. Watendaji wawili na mwalimu mmoja wanaendelea na masomo ya shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Kampala Uganda. Aidha walimu wawili pia wanaendelea na masomo ya shahada ya kwanza ya fani ya elimu mjumuisho katika ‘Sebastian Kolowa Memorial University, huko Lushoto Tanga.

 

 

Ushauri Nasaha

183.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kimefanya utafiti juu ya idadi ya walimu washauri waliopata mafunzo ya ushauri nasaha kwa upande wa Unguja. Kati ya walimu wote wa ushauri nasaha 350 (175 wanawake na 175 wanaume) ni walimu washauri 119 tu ndio waliopatiwa mafunzo (59 wanaume na 60 wanawake). Utafiti kama huo unatarajiwa kufanyika Pemba katika mwaka 2013/2014.

 

184.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kilifuatilia  kesi 11 za udhalilishwaji wa wanafunzi na kwa kushirikana na Idara ya Ustawi wa Jamii ilitoa mafunzo kwa wanafunzi wa skuli walizotoka juu ya namna ya kujikinga na matokeo ya udhalilishaji na kuweza kutoa taarifa pindi tatizo linapotokezea. Mafunzo kama hayo yataendelea kutolewa katika skuli nyengine. 

 

Mapambano Dhidi ya UKIMWI na Madawa ya Kulevya

185.      Mheshimiwa Spika, katika mapambano dhidi ya UKIMWI na madawa ya kulevya, Kitengo kimetoa mafunzo ya stadi za maisha kwa walimu 140 (walimu 80 Unguja na 60 Pemba).  Lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha walimu kusimamia vyema shughuli za stadi za maisha katika klabu za afya za skuli.  Aidha mafunzo mengine yalitolewa kwa wanafunzi 300 (180 Unguja na 120 Pemba).

 

Masuala ya Jinsia

186.      Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha masuala ya kijinsia, Kitengo kilishirikiana na FAWE Zanzibar kutoa mafunzo kwa walimu 40 (wanawake 22 na wanaume 18) kutoka katika skuli mbali mbali za Unguja na Pemba. Lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha walimu kuelewa mbinu mbali mbali za ufundishaji kwa muitikio wa jinsia (gender responsive pedagogy) na kuwapa ujuzi wakufunzi wa vyuo vya ualimu ili waweze kutoa mafunzo kwa walimu wanafunzi juu ya ufundishaji kwa kuzingatia muitikio wa kijinsia.

 

187.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014,  Kitengo kitaendeleza masuala ya elimu mjumuisho  na stadi za maisha kutoa mafunzo ya mbinu za ufundishaji katika elimu mjumuisho kwa walimu zaidi, kuhamasisha jamii kuhusu haki ya elimu kwa watoto wote hasa wale wenye mahitaji maalum, kutoa mafunzo ya stadi za maisha kwa walimu na wanafunzi ili waweze kupambana na changamoto mbali mbali, kufanya utafiti kwa skuli 86, kutoa mafunzo kwa walimu washauri nasaha na kuwajengea uwezo wafanyakazi wa Kitengo.

 

Kwa mwaka 2013/2014, Kitengo kimepangiwa kutumia jumla ya T. Sh. 99,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

KITENGO CHA URAJIS

Baraza la Elimu

188.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Baraza la Elimu lilifanya kikao kimoja ambacho wajumbe walijadili na kupitisha ada mpya za leseni za walimu na usajili wa skuli za binafsi.  Pia, wajumbe wapya walielimishwa kuhusu Sera ya Elimu ya 2006 na Sheria ya Elimu pamoja na kupitia mtaala mpya wa Stashahada ya Ualimu ya Msingi.

 

 

 

Leseni za Walimu

189.      Mheshimiwa Spika, jumla ya walimu 383 walipatiwa leseni za kusomeshea. Kati ya walimu hao 251 waliosomea na 132 wasiosomea. Pia, maofisa wa Kitengo walitembelea skuli za serikali 47 na binafsi 39 kuhakiki na kukagua leseni za walimu, usajili wa skuli, sera, sheria, kanuni na miongozo ya kazi  na mambo mengine yanayohusu skuli. Vile vile, Kitengo kinaendelea kushirikiana na wakaguzi wa elimu katika kukagua skuli za binafsi na Serikali ili kufuatilia utekelezaji wa kazi.  

 

Maombi ya Usajili wa Skuli za Serikali na Binafsi

190.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Wizara ilisajili skuli 29 za Serikali na skuli 20 za Binafsi. Katika mwaka 2013/2014, Ofisi ya Mrajis wa Elimu itaendelea kushughulikia maombi ya usajili wa skuli na leseni za walimu kutoka skuli zote za serikali na binafsi.

 

Kesi za Ujauzito na Ndoa za Wanafunzi

191.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, kesi 18 za ujauzito wa wanafunzi ziliripotiwa, ambapo kesi moja ilikuwa ya mwanafunzi kwa mwanafunzi. Kesi 4 kati ya hizo zilijadiliwa na wanafunzi watatu walikubali kuendelea na masomo.

 

192.      Mheshimiwa Spika, katika kipindi hiki kesi 23 za ndoa za wanafunzi ziliripotiwa na kati ya kesi hizi moja ilikua baina ya mwanafunzi kwa mwanafunzi. Kwa mujibu wa Sheria ya Elimu namba 6 ya mwaka 1982 kifungu cha 20 (3), wanafunzi 23 wa kike na mwanafunzi mmoja wa kiume walifukuzwa skuli.  Katika mwaka 2013/2014, Kitengo cha Urajis kitaendelea kushughulikia kesi za ujauzito na ndoa na pia kuwapatia elimu juu ya umuhimu wa elimu kwa wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa skuli.

 

Kwa mwaka 2013/2014 Kitengo kimepangiwa jumla ya T.Sh. 60,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

KITENGO CHA MICHEZO NA UTAMADUNI

193.      Mheshimiwa Spika, Kitengo cha Michezo na Utamaduni kimeundwa ili kusaidia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya michezo Zanzibar ndani ya skuli na kukuza vipaji vya watoto ili kupata wanamichezo bora.

 

194.      Mheshimiwa Spika, katika kufufua vugu vugu la michezo lililokuwepo zamani katika skuli zetu zote sambamba na kuhamasisha vijana katika shughuli za michezo, Wizara yangu imeshirikiana kwa karibu sana na Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo. Mikutano mbali mbali imeandaliwa baina ya viongozi wa Wizara hizi mbili ili kupanga mikakati ya pamoja katika kuinua michezo katika skuli. Katika kuendeleza ushirikiano huo, Baraza la Michezo la Zanzibar, limeipatia Wizara yangu mipira 20,000 kwa ajili ya kuendeleza michezo ya mpira wa miguu na netboli kwa skuli zote za Serikali na binafsi. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo na Baraza la Michezo la Zanzibar kwa msaada huo na mashirikiano makubwa na Wizara yangu. Kitengo kiliandaa mashindano ya riadha kwa mbio za nyika (cross country) kwa wanafunzi wa skuli za sekondari na msingi ambapo jumla ya wanafunzi 400 walishiriki.  Mbio hizi za “Elimu cross country” zilizoshirikisha pia, wanafunzi kutoka skuli ya Filbert Bai ya Kibaha. Kitengo kinakusudia kuyaendeleza mashindano ya “Elimu cross country “kila mwaka na kuzishirikisha skuli zaidi kutoka nje ya Zanzibar ili kuleta hamasa kubwa zaidi.

 

195.      Mheshimiwa Spika, timu zetu zilishiriki katika mashindano ya UMISSETA huko Kibaha Tanzania Bara.  Timu zilizoshiriki ni mpira wa miguu (wanaume na wanawake), mpira wa kikapu, mpira wa wavu, netiboli, mpira wa mikono, riadha, mpira wa meza na bao. Katika mashindano hayo, tumeweza kuwa mshindi wa kwanza katika mpira wa kikapu na mchezo wa bao, mshindi wa pili katika mpira wa miguu na mpira wa mikono na mshindi wa tano katika riadha. Zanzibar imekuwa watano kati ya kanda kumi na mbili zilizoshiriki.

 

196.      Mheshimiwa Spika, Kitengo kimeendelea kutoa mafunzo mbali mbali ya michezo kwa kushirikiana na taasisi nyengine zinazojishughulisha na michezo hapa Zanzibar na Tanzania kwa jumla. Kwa kushirikiana na “British Council” kupitia mradi wake wa “International Inspiration” ilitoa mafunzo kwa walimu 90 kutoka skuli mbali mbali za Unguja kwa michezo ya mpira wa wavu (30), riadha (30) na mpira wa miguu kwa wanawake (30). Mradi huo unaotekelezwa hivi sasa katika Mkoa wa Mjini Magharibi katika skuli ya Regezamwendo, Langoni na SOS utakuwa wa miaka mitatu ambao umekuja kufuatia nchi ya Uingereza kuteuliwa kuandaa michezo ya Olimpiki mwaka 2012. Kabla ya kuteuliwa kwake Uingereza iliahidi kutoa mafunzo kwa wanamichezo millioni 23 katika kipindi cha miaka mitatu duniani. 

 

197.      Mheshimiwa Spika, Kitengo pia kiliendelea kutoa mafunzo kwa walimu wa skuli za msingi wanaofundisha somo la michezo kwa darasa la kwanza na la pili katika Wilaya za Mkoani na Micheweni ili kupata wataalamu na wanamichezo bora wenye uelewa wa masuala ya  michezo.  Jumla ya walimu 60 wa madarasa hayo walipatiwa mafunzo ambayo yatawasaidia kupata mbinu mbali mbali za kufundisha somo la michezo kwa ufanisi. 

 

198.      Mheshimwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Kitengo kina lengo la kuendelea kuwapatia taaluma ya michezo walimu wa fani mbali mbali za michezo katika skuli zetu za Unguja na Pemba kwa kushirikiana na taasisi nyengine za michezo ndani na nje ya nchi yetu kadiri hali ya kifedha itakavyoruhusu. Pia, Wizara itaendelaea kuandaa mashindano ya michezo maskuli na kushiriki katika michezo itakayoandaliwa na umoja wa michezo na sanaa skuli za sekondari Tanzania (UMISSETA) na na Shirikisho la Michezo ya skuli za sekondari Afrika ya Mashariki (FEASSSA) kwa lengo la kuibua, kuinua, kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana wetu na kuitangaza Zanzibar kupitia midani za michezo  nje ya mipaka yake.

 

Kwa mwaka 2013/2014, Kitengo kimepangiwa jumla ya T.Sh. 120,000,000/- kwa kazi za kawaida.

 

MAPATO

199.      Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ilikadiriwa kukusanya T.Sh. 22,500,000/- kutoka vianzio vya ada za leseni za walimu pamoja na uandikishaji wa skuli binafsi. Hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2013, jumla ya T.Sh. 30,192,900/- zilikusanywa na kuwasilishwa ikiwa sawa na asilimia 134.2 ya makadirio.  Kuongezeka kwa makusanyo kunatokana na mabadiliko ya ada ya leseni na usajili wa skuli binafsi na kupatiwa leseni walimu wapya. Katika mwaka 2013/2014, Wizara inakusudia kukusanya jumla ya T.Sh. 15,000,000/- ikiwa ni mapato ya usajili wa skuli za binafsi na leseni za walimu na kuziwasilisha Hazina.

 

          SHUKRANI

200.      Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa washirika wote wa sekta ya elimu wakiwemo wananchi, nchi wahisani na mashirika ya misaada ya kimataifa kwa kutuunga mkono katika jitihada zetu za kuendeleza elimu. Napenda kutoa shukrani zetu za pekee kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, Serikali ya Oman, Serikali ya India, Serikali ya Nigeria, Serikali ya Marekani, Sweden na Uingereza. Pia, napenda kuyashukuru mashirika mbali mbali yakiwemo Sida, British Council, USAID, UNICEF, UNESCO, GPE, VSO, Peace Corps, JICA na KOICA. Pia shukrani zetu ziende kwa Aga Khan Foundation, Benki ya Dunia, Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika na Benki ya Maendeleo ya Afrika. Pia napenda kuyashukuru mashirika yasio ya kiserikali ya FAWE, Takotof, Save the Children Fund, Sazani Associates na Book Aids International.

 

JUMLA YA GHARAMA ZA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI.

201.      Mheshimiwa Spika, ili Wizara yangu iweze kutekeleza majukumu yake iliyojipangia katika mwaka wa fedha 2013/2014 kwa ufanisi, naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe matumizi ya jumla ya T.Sh. 115,747,619,000/-. Kati ya fedha hizo T.Sh. 80,200,000,000/- ni kwa matumizi ya kawaida, T.Sh. 5,350,000,000/- za SMZ na T.Sh. 30,197,619,000/- za washirika wa maendeleo kwa matumizi ya miradi ya maendeleo. Jadweli namba 46 na 47 zinatoa uchambuzi.

 

 

 

 

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

KIAMBATISHO


 

 

 

 

(Takwimu za Maendeleo ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali

       Kwa Kipindi cha 2008 - 2013 na Hali Halisi ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa Mwaka 2013)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.