Na Himid Choko.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mheshimiwa Pandu Ameir
Kificho leo jioni amelazimika kuahirisha kikao cha baraza la
wawakilishi kwa muda wa dakika 15
kutokana na wajumbe wengi kucherewa kufika katika kikao hicho.
Akizungumza baada ya kurejea tena katika kikao hicho Mhe
Kificho amewataka wajumbe hao kuacha mara moja tabia mbaya ya utoro na
ucherewaji katika vikao vya baraza .
Amesema chombo cha baraza la wawakilishi ni chombo
kikubwa katika nchi hivyo kinapaswa kuwa
kioo, hivyo si nyema kwa wajumbe wa baraza hilo kucherewa au kutoroka katika
vikao hivyo ambayo vinaonyeshwa na
kutangazwa moja kwa moja kupitia vyombo
vya habari.
Amesema amewaomba wawakilishi hao kutoendelea kujipa sura
mbaya kwa wananchi na badala yake
watekeleze ipasavyo majukumu waliyokabidhiwa na wananchi kwa faida yao na taifa kwa ujumla.
Aidha spika kificho amewaomba radhi wananchi kutokana na
kitendo kilichofanywa na wawakilishi wao .
Wakati huo huo katibu wa BLW
Yahya khamis Hamadi amesema
Baraza la Wawakilishi limelazimika kuitisha Kikao cha Dharura cha Kamati
ya Uongozi ya Baraza ili kujadili
kitendo hicho cha leo.
Amesongeza kusema kwamba kitendo kilichoonyeshwa na waheshimiwa wawakilishi hao hii leo si
nidhamu wala si cha haki hivyo Kamati ya
uongozi ya baraza itakutana jumatau ijayo kuangalia uwezekano wa kubadilisha
Kanuni ili kudhibiti nidhamu ya Baraza.
Amesema cha kusikitisha zaidi hii leo wakati mhesimiwa Spika
anaakhirisha kikao hicho kwa muda hata wanadhimu wa vyama na serikali nao hawakuwemo wakati huo.
No comments:
Post a Comment