Habari za Punde

JK, Bilal wawajulia hali Waziri Haroun, mzee Msuya

Na Mwandishi wetu
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemjulia hali Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Haroun Ali Suleiman, anaepatiwa matibabu katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Rais Kikwete alifanya ziara hiyo juzi akiambatana na mkewe, mama Salma Kikwete.
Aidha Rais Kikwete alimtembelea na kumkagua Waziri Mkuu Mstaafu, mzee Cleopa David Msuya aliyelazwa hospitali hiyo akiendelea na matibabu.
Ziara kama hiyo imefanywa na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal.
Awali Dk. Bilal akiambatana na mkewe mama Zakia Bilal alimtembela mzee Msuya, aliyelazwa hospitalini hapo na baadae alimjulia hali Waziri Haroun.
Januari 13, Rais Kikwete alimtembela kumjulia hali Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour nyumbani kwake Migombani

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.