Habari za Punde

Balozi Seif akutana na Uongozi wa Kampuni ya Lucky Export ya India

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akizungumza na Meneja wa Kampuni ya Kimataifa ya uwekezaji vitega uchumi  wa Kampuni ya Lucky Exports kutoka Nchini India Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Balozi Seif akisalimiana na Menaja wa Kampuni ya Lucky Exports ya India inayoptaka kuwekeza katika sekta za Afya na Viwanda vidogo vidogo vyua mazao ya Baharini.
Balozi Seif akisalimiana na Mwakilishi wa Kampuni ya Lucky Exports Tawi la Tanzania Bwana Kim Mghaya.Kati kati yao ni Meneja wa Kampuni hiyo yenye makao makuu yake Nchini India Bwana Ravi  Rai.Picha na Hassan Issa wa – OMPR 


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikutana kwa mazungumzo na ujumbe wa Kampuni ya uwekezaji vitega uchumi vya sekta za Afya, Kilimo, Umeme, viwanda vidogo vya mazao ya Baharini ya Lucky Exports kutoka Nchini India.

Kampuni hiyo ambayo imefungua Matawi yake katika mataifa mbali mbali Barani Afrika tayari imeshapata usajili wa kufungua Tawi lake Nchini Tanzania.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar  Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar  Meneja wa Kampuni hiyo Bwana Ravi Rai  alisema Taasisi yake imelenga kutoa huduma za afya pamoja na viwanda vidogo vidogo vya mazao ya Baharini.

Bwana Ravi Rai alisema wakati Uongozi wa Taasisi yake ukisubiri kuanza na hatimae kukamilisha taratibu zote za uwekezaji uwekaji wa miradi hiyo umekusudia kusaidia kutoa ajira kubwa kwa wazalendo pamoja na kuongeza mapato ya Taifa.


Alifahamisha kwamba utafiti  wa wataalamu wa Taasisi hiyo utafanywa ili kuangalia miradi ambayo kampuni hiyo inaweza kuiwekeza hapa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

“ Tunafarajika kuona kwamba miradi yoyote tutakayoamuwa kuitekeleza  kwenye uwekezaji wa mataifa mbali mbali duniani na hasa tukilenga zaidi Bara la Afrika inafadhiliwa na Serikali ya India “. Alisema Meneja huyo wa Lucky Exports.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema miradi iliyofikiriwa kuanzishwa na Uongozi wa Kampuni hiyo hapa Zanzibar  ya Sekta ya Afya na Viwanda Vidogo vidogo vya mazao ya Baharini  itasaidia kustawisha maisha naustawi wa Jamii Nchini.

Balozi Seif aliuagiza  Uongozi wa Kampuni hiyo ya Lucky Exports kutoka Nchini India kurahisisha maombi yao ya uwekezaji ili taasisi zinazohusika na uwekezaji ziweze kuyapitia na kutoa maamuzi yanayostahiki kwa wakati muwafaka.

Kampuni ya Uwekezaji ya Lucky Exports ya Nchini India ambayo tayari imeshafungua matawi yake katika Mataifa ya Ethiopia, Guinea BisauMalawi na Tanzania inajihusisha zaidi na uwekezaji wa miradi ya Afya, Kilimo, Viwanda vya mazao ya Baharini, Umeme pamoja na huduma za Reli.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.