Habari za Punde

Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani katika viwanja vya Kidongochekundu Zanzibar.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk. Mohammed Jidawi akimkabidhi zawadi Muuguzi Ramla Kombo  wa Kituo cha Afya Unguja Ukuu kwa kuwa miongoni mwa wauguzi waliofanya vizuri zaidi  mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani yaliyofanyika Kidongochekundu. 
Muuguzi Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Bi. Wanu Bakari Khamis akisoma risala ya siku ya wauguzi Duniani katika maadhimisho yaliyofanyika katika hospitali ya Kidongochekundu.
Wauguzi wa Zanzibar wakiimba nyimbo ya siku ya wauguzi Duniani katika maadhimisho yaliyofanyika Hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongochekundu.
Wauguzi wa  Zanzibar wakila kiapo cha Utii katika maadhisho ya siku ya wauguzi Duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 12 Mei.  Maadhimisho hayo yalifanyika Hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongochekundu . 
Muuguzi Rajab Khamis Rajab akipokea zawadi kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya ya Zanzibar kwa  kuwa miongoni mwa wauguzi waliotekeleza wajibu wao kwa ufanisi zaidi mwaka huu.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk. Mohammed Jidawi akimkabidhi zawadi Muuguzi Ramla Kombo  wa Kituo cha Afya Unguja Ukuu kwa kuwa miongoni mwa wauguzi waliofanya vizuri zaidi  mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani yaliyofanyika Kidongochekundu.
Wauguzi  wa Zanzibar wakimsikiliza Katibu  Mkuu wa Wizara ya Afya Dk. Muhammed Jidawi (hayupo pichani) katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani yaliyfanyika Hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongochekundu.(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.