Habari za Punde

Aliedaiwa kumpa ujauzito mtoto wa mkewe aachiwa huru

Asya Hassan na Khamis Amani
Mahakama ya Mkoa Mwera, imemuachia huru mshitakiwa,Nasu Kassim Chande (30) mkaazi wa Muyuni ‘C’ wilaya ya kusini Unguja, alieshitakiwa kwa kosa la kumuingilia mtoto wa mkewe, kutokana na ushahidi kutopatikana.

Hakimu wa mahakama hiyo, Hamisa Suleiman Hemed, alimwachia huru mshitakiwa huyo kutokana na ushahidi uliotolewa na mashahidi kutobainisha ukweli wa kosa lililokuwa likimkabili.

Akitoa hukumu, hakimu huyo alisema  anamuachia huru mshitakiwa chini ya kifungu cha 219 cha sheria namba 7 ya mwaka 2004.

“Kutokana na kutokuwepo ushahidi wa kutosha ambao ungeweza kuishawishi mahakama kukubali shitaka dhidi yake, mahakama hii inamuachia huru mshitakiwa,” alisema.

Mshitakiwa huyo alishitakiwa kwa kosa la kumuingilia kimwili mtoto wa mkewe na  kumsababishia ujauzito, ingawa ushahidi wa daktari haukueleza kwamba ujauzito umepatikana  lini na kama ni wa mshitakiwa.


Sababu nyengine iliyosababisha mshitakiwa aachiwe huru ni makosa ya mashtaka, ambapo mshitakiwa alishtakiwa kwa kumuingilia maharimu wake wakati kifungu 160 namba 7 ya mwakja 2014, kinaeleza kwamba maharimu  ni mju kuu wa kike, dada na mama na wala sio mtoto wa kambo.

 “Mazingira ya kosa hili yapo yana utata kwa kuwa kesi hii ni kubwa ushidi wake pia ulipaswa uwe mzito na wa kuridhisha,” alisema.

Awali kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyowasilishwa mahakamani hapo ilildaiwa kuwa mshitakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo Oktoba 29 mwaka 2012 kujibu shutuma hizo.


Ilidaiwa tukio hilo lilitokea mwezi usiofahamika ambapo mshitakiwa alimuingilia mtoto wa mkewe wa ndoa na kumsababishia ujauzito kitendo ambacho ni kosa kisheria. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.