Habari za Punde

Sala na Baraza la Iddi el Fitr 1435/2014

KUH: SALA NA BARAZA LA IDDI EL FITRI 2014
 
Kwa heshima naomba uhusike na mada ya hapo juu.
Swala ya Iddi El Fitri inatarajiwa kuswaliwa 1:00 asubuhi katika viwanja vya Maisara siku ya Jumatatu tarehe 28 au Jumanne ya tarehe 29 Julai 2014 itategemea na kuandama kwa mwezi.
Iwapo itanyesha Mvua itaswaliwa katika Mskiti wa Mwembe-Shauri .
 
 Aidha, Baraza la Iddi linatarajiwa kufanyika siku hiyo hiyo saa 4:00 za asubuhi katika ukumbi wa Salama, Hoteli ya Bwawani
Mgeni Rasmi katika shughuli hizo za Sala na Baraza la Iddi anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dkt. Ali Mohamed Shein.
 
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.