Habari za Punde

JUKITA: Baadhi ya Kamati BMK zinafanya semina

Na Fatuma Kitima, Dar es Salaam
JUKWAA la Katiba Tanzania (JUKITA), limesema tatizo la mahudhurio katika Bunge Maalum la Katiba, limesababisha baadhi ya kamati za Bunge kuchelewa kuanza kazi au kushindwa kuendelea na kazi.

Hali hiyo imesababisha kamati hizo kuishia kuendesha semina zisizotarajiwa ili kuhalalisha matumizi ya fedha za wavuja jasho wa Tanzania.

Waraka wa JUKITA uliosainiwa na Kaimu Mwenyekiti, Hebron Mwakagenda, imesema taarifa hizo zimepatikana kufuatia ufuatiliaji uliofanywa kuanzia Agosti 11 hadi 23 mwaka huu.

Aidha Jukwaa hilo limesema  Bunge la Katiba limetaja kuwa juma la wajumbe 441 walihudhuria vikao vya bunge, lakini uchunguzi umebaini wajumbe hao ni wale wote ambao waliwahi kufika na kusaini kitabu cha mahudhurio na wengi wao takribani wajumbe 100 waligundulika hawapo bungeni, wakiwemo mawaziri wa serikali zote mbili.

Taarifa hiyo imesema pamoja na ofisi ya Katibu wa Bunge Maalum kuonesha imebana mianya kwa wajumbe ambao husaini na kutofanya kazi, lakini fedha zimeendelea kuvuja kwa kutumia mianya mengine ikiwemo Mawaziri na Manaibu Mawaziri ambao hutoa taarifa za kutohudhuria bungeni kwa Waziri Mkuu 
kutokana na shughuli nyingine za kiserikali.

Alisema hali hiyo inasababisha viongozi hao kulipwa posho mara mbili; kutoka bunge la katiba na kule wanakokwenda kutekeleza majukumu mengine.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tayari shilingi bilioni 6.3 zimeshatumika mpaka kufikia Agosti 23 mwaka huu.

Kuhusu rais kutokuwa na uwezo wa kusitisha bunge la katiba, taarifa ilisema wasaidizi wake wanajaribu kutumia jina la Rais 
kwa manufaa yao.


Imesema pamoja na kwamba rais hakuwa na mamlaka ta kuanzisha mchakato wa kuandika katiba kisheria mwaka 2010, 
lakini aliuanzisha kupitia upenyo wa kisiasa kwa kuwa yeye ni 
kiongozi mkuu wa nchi.

Hivyo, imesema JUKATA inaamini Rais hawezi kuacha mambo yaharibike na kukaa kimya kwa sababu tu kisheria hana 
mamkalaka.

Kuhusu kupatikana theluthi mbili (2/3) hasa kutoka Zanzibar ili kupitisha katiba mpya, Jukwaa hilo limesema hoja sio idadi ya kura au wajumbe, bali ni maridhiano ya kitaifa na kwamba kama haiwezekani kupata kupatikana hakuna sababu ya kufuja fedha 
za walipa kodi maskini ambazo zingefanya mambo mengine.



Jukwaa hilo pia limesema kitendo kinachofanywa na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta na Makamu wake, Samia Suluhu Hassan cha kupokea maoni mapya, ni kunyume na sheria ya mabadiliko ya katiba kifungu 9(1) ambacho kinaeleza kazi za tume ambazo ni kukusanya, kuchambua, kuandika na kuwasilisha kwenye bunge maalum la katiba na kwamba kazi ya bunge ni kupitisha katiba. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.