Na Hafsa Golo
MALAKA ya Kuzuia Rushwa
na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) imemtia mbaroni askari wa usalama
barabarani, Koplo Ramadhan Sheha akishawishi na kupokea rushwa ya shilingi
10,000 kutoka kwa mpanda pikipiki.
Mkurugenzi wa Mamlaka
hiyo, Mussa Haji, alisema askari huyo alimatwa na maofisa wa ZAECA akipokea
rushwa hiyo ili asimfikishe katika vyombo vya sheria mpanda pikipiki huyo.
Tukio hilo lilitokea
Mwanakwerekwe Agosti 19 mwaka huu saa 7:00 mchana.
Alisema mpanda pikipiki
ambae ni raia mwema anaepinga rushwa, alitoa ushirikiano kwa taasisi hiyo
kuweza kufanikisha kukamatwa kwake.
Alisema tayari jalada la
kesi linalomuhusu askari huyo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka na atafikishwa
mahakamani baada ya taratibu kukamilika.
Kuhusu mtu alietoa fedha
hizo, hatashtakiwa kwa sababu ni raia mwema ambae hakuwa na dhamira ya kutoa
rushwa na kwamba anaonekana kuchukia dhambi hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa
wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alisema taarifa hizo zipo, lakini
hazijafikishwa rasmi na kumtaka mwandishi wa habari hizi awafuate ZAECA.
Aidha alisema vitendo
vya rushwa kwa askari wa usalama barabarani vimekuwa vikishamiri katika maeneo
ya Unguja na Pemba, hivyo wananchi wawe tayari kumfichua askari yeyote atakae
kiuka utaratibu wa majukumu yake ya kazi.
Aliwataka wananchi kutoa
ushirikiano kukomesha vitendo hivyo kwa sababu Zanzibar bila rushwa inawezekana.
sawa wananchi watoe mashirikiano lakini hao wahusika mtawapa adhabu gani ili wakome?, au atasomewa shtaka halafu siku mbili aje atutie adabu tena barabarani? (ataendelea na kazi yake kama kawaida halafu alipize kisasi kwa huyo raia mwema).
ReplyDelete