Na Kadama Malunde, Shinyanga
MATUKIO ya ukatili dhidi
ya watoto yameendelea kujitokeza mkoani Shinyanga ambapo mtoto wa miaka 9 ambae
ni mwanafunzi wa darasa la tatu katika skuli ya msingi Negezi iliyopo kata ya
Ndala manispaa ya Shinyanga, ameuawa kwa kubakwa kisha kutobolewa macho.
Tukio hilo limetokea
Agosti 25 mwaka huu saa saba mchana katika kitongoji cha Kashampa kijiji cha
Nhelegani kata ya Kizumbi tarafa ya Shinyanga mjini, ambapo mtoto huyo alikutwa
kwenye kichaka vilivyo karibu na shamba la Mwandu Misona.
alioshuhudia tukio hilo walisema mtoto huyo
alikutwa akiwa amefariki dunia huku mwili wake ukiwa umetobolewa sehemu mbali mbali.
Akielezea zaidi kuhusu
tukio hilo baba mazazi wa mtoto huyo Kashindye Mayala alisema mwanawe alikuwa
anaishi na shangazi yake Mahegi Mayala na aliaga kwenda kunyoa nywele saluni
majira ya saa tisa alasiri siku ya Jumapili na baada ya hapo hakurudi tena
nyumbani.
Alisema siku ya Jumatatu
walipata taarifa kuwa kuna mtoto ametupwa vichakani karibu na shamba la Mwandu
Misona na walipofika eneo la tukio hawakumkuta mtoto huyo na kudaiwa kuwa
amepelekwa na wasamaria wema hospitali ya mkoa wa Shinyanga.
Alisema kufuatia taarifa
hizo aliamua kuufuatilia mwili huo hospitalini hapo,ili kubaini kama ni mtoto
wake na alipofika chumba cha kuhifadhia maiti alibaini mwili huo kuwa ni wa
mtoto wake.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa
hospitali ya mkoa wa Shinyanga, Dk. Daniel Maguja, alisema waliupokea mwili wa
mtoto huyo Agosti 25, mwaka huu majira ya saa 10:30 jioni na kuongeza kuwa
vipimo vilionesha mtoto huyo alibakwa na kutobolewa.
Kamanda wa polisi mkoani, Shinyanga SACP Justus
Kamugisha, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa chanzo
kinachunguzwa ili kuwabaini wahusika.
No comments:
Post a Comment