Abu
‘Ammaar
Tunapoazimia
kwenda kufanya ibada ya Hajj, hatuna budi kujipanga katika mpangilio ambao
tutahakikisha tutanufaika katika safari yetu hii muhimu katika kila Nyanja ya
maisha yetu.
Ni fursa
ambayo hutokea mara moja katika maisha hivyo si jambo la kulichukulia kiwepesi
wepesi.
Ibaada ya
Hajj ni miongoni mwa ibada muhimu kwa Muislamu ambazo Allaah Subhaanahu
Wata’ala anazipenda na kuziridhia.
Na moja
katika jambo la kulizingatia ni kujiandaa katika kuipata ile aina ya Hajj
ambayo Mtume wetu Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam ameipa jina la Hajj Mabruur.
Tusiende kuhiji tu bali tuazimie kwenda kuhiji hajj hii ya Mabruur.
فعن أبي هريرة – رضي الله عنه- قال: سئل النبي
صلى الله عليه وسلم: أي الأعمال أفضل؟ قال: (إيمان بالله ورسوله)، قيل :ثم ماذا؟
قال: (جهاد في سبيل الله)، قيل : ثم ماذا؟ قال: (حج مبرور) "متفق عليه".
Kutoka kwa Abu Hurayrah , Allaah
amuwie radhi amesema: Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam aliwahi kuulizwa:
‘Amali gani iliyokuwa bora? Akasema: Kumuamini Allaah na Mtume wake’
Pakasemwa:‘kisha kitu gani?’ Akasema: ‘Kupigana jihad kwa ajili ya Allah’
Pakasemwa: ‘ Kisha kitu gani?’ Akasema : ‘ Hajj Mabruur’ Bukhaari na Muslim.
Mtume
Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam amemuhakikishia kila anaekwenda kuhiji kwamba
ikiwa atafanya Hajj ili inayoitwa Mabruur basi malipo yake ni pepo kama
alivyosema katika hadithi
والحج المبرور ليس له جزاء إلا الجنة) "متفق
عليه"
Hakuna malipo mengine kwa Hajj
Mabruur isipokuwa pepo.
Bukhaari na Muslim
Na hata
Ummul Muuminiyna, Mama wa waumini, Aaishah, Allaah amuwie radhi, aliwahi
kumuuliza Mtume Swalla Allaahu ‘alayhi Wasallam
: يا رسول الله،ألا نغزو
ونجاهد معكم، فقال عليه الصلاة والسلام: (لكُنّ أحسن الجهاد وأجمله الحج، حج
مبرور)، قالت: فلا أدع الحج بعد إذ سمعت هذا من رسول الله صلى الله عليه وسلم)
"رواه البخاري".
Ewe Mjumbe
wa Allaah! Kwanini hatuwezi kupigana na kushirikiana nanyi kwenye Jihaad? Mtume
Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam akasema:
‘Lakini Jihaad iliyokuwa bora na nzuri kwenu ni Hajj; Hajj Mabruur’.
Bukhaari
Neno
Mabruur linatokana na asli ya neno Birr katika lugha ya kiarabu na lina maana
pana kwani linajumuisha tabia iliyotukuka, kutekeleza wajibu na kuhakikisha
kila mwenye haki basi anapata haki yake.
Mtume
Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam anasema ‘Birr ni tabia njema’ Pia aliwahi
kuulizwa Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam kwamba kitu gani mtu afanye ili
Hajj yake iwe Mabruur? Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam akasema :
(إطعام
الطعام وإفشاء السلام) "رواه أحمد".
‘kulisha watu chakula na Kudhihirisha (kupeana) salam (baina yenu)’
‘kulisha watu chakula na Kudhihirisha (kupeana) salam (baina yenu)’
Ili
tuweze kuifikia Hajj Mabruur, ni wajibu kwa kila mwenye kujaaliwa kwenda safari
ya Hajj kuhakikisha kila tendo atakalolifanya wakati wa kutekeleza ibada hii
liko sahihi. Hivyo ni lazima ajielimishe vizuri taaluma ya Hajj, fardhi zake,
wajibu wake, sunnah zake, makatazo yake kama vile ambavyo ametufundisha Mtume
wetu Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam. Pia ahakikishe kwa kila jambo
analolifanya anamfuata Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam katika
kulitekeleza.
فعن جابر –رضي الله عنه- قال: رأيت النبي صلى
الله عليه وسلم يرمي على راحلته ويقول: (لتأخذوا مناسككم فإني لا أدري لعلي لا أحج
بعد حجتي هذه) "رواه مسلم".
Kutoka
kwa Jaabir, Allaah amuwie radhi, amesema: Nilimuona Mtume Swalla Allaahu
‘Alayhi Wasallam akirusha (mawe) akiwa katika kipando chake (msimu wa Hajj) na
akasema: ‘Chukueni kutoka kwangu matendo
ya Hajj, kwani sina hakika kama nitahiji (tena) baada ya Hajj yangu hii’
Muslim
Ili
Hajj ifikie darja ya kuitwa Mabruur lazima ifanyike kwa Ikhlaas ya darja ya juu
kabisa. Kwasababu kuwepo Ikhlaas ni moja ya masharti muhimu ya kukubaliwa ibada
ya mja. Ikhlaas ni ile hali ya kufanya ibaada si kwa jambo lengine lolote
isipokuwa kutaka radhi za Allaah Subhaanahu Wata’ala pekee. Ndiyo maana Mtume
Swala Allaahu ‘Alayhi wasallam anatukumbusha wakati tukifanya Ibada hii muhimu
kuomba dua’a
( اللهم حجة لا رياء فيها
ولا سمعة رواه
ابن ماجة
“Ewe Mola
(tunakuomba utuwafikishe kwa) Hajj isiyokuwa na Riyaa (kujionesha) wala majivuno (ya kutajwa na watu) “. Ibnu Maajah.
Masahaba
ambao walimfahamu vyema kigezo cha kuigwa katika matendo mema kwa Mtume Swalla
Allaahu ‘Alayhi Wasallam kwani Anas bin Maalik, Allaah amuwie radhi ,
إذا أحرم لم يتكلم في شيء من أمر الدنيا حتى
يتحلل من إحرامه
Akishahirimia
(kwa ajili ya Hajj) hakuwa akizungumza jambo lolote katika mambo ya kidunia
mpaka anapomaliza Ibada yake.
Tumuombe
Allaah Subhaanahu Wata’ala atujaalie na awajaalie Wageni wa Arrahmaan Hajj
mabruur na Dhambi zilizosamehewa, Sa’ay yenye kushukuriwa.
Tumuombe
Allaah Subhaanahu Wata’ala awafanyei wepesi kwa wote waliotia nia ya kwenda
kuhiji na awawafikishe katika Hajj kwa kuwatakabalia Ibaada zao na maombi yao
Aamiyn Aamiyn.
No comments:
Post a Comment