Na
Hafsa Golo
NAIBU
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili, Juma Ali Juma, amesema Zanzibar ina
nafasi kubwa ya kuinua uchumi na kipato cha wananchi kupitia zao la karafuu.
Aliyasema
hayo jana ofisi kwake Darajani wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema
karafuu zinaweza kupunguza kiwango cha umaskini iwapo zao hilo litaimarishwa.
Alisema serikali inaendelea kutoa msukumo
kuimarisha zao hilo ikiwemo kuwapa wakulima asilimia 80 ya bei katika soko la
dunia.
‘
Aidha
alisema miongoni mwa hatua zinazochukuliwa na serikali kupitia wizara hiyo ni
kuhakikisha wakulima wanapatiwa miche ya mikarafuu ili kuuimarisha kilimo
hicho.
Alisema
mkulima hupatiwa miche 40 ya mikarafuu lakini kiwango hicho huongezwa baada ya
kuthibitishwa mkulima na uwezo na eneo la kuipanda.
Alisema
katika msimu wa mwaka 2014 wizara imeotesha miche 1,000,000 ya mikarafuu kati
ya hiyo 503,560 imefikia umri wa kupandwa.
Alisema
miche 178,540 tayari imepandwa Unguja na miche 325,020 imepandwa Pemba.
Alisema
miongoni mwa changamoto zinazojitokeza
katika uimarishaji wa zao hilo ni pamoja na
ukataji wa miche ya zao hilo na kurejesha nyuma juhudi za wakulima.
Jee karafuu ikianguka bei katika soko la dunia,jee hali za wazanzibari zitakuwa juu kiuchumi au chini.Tafuteni njia mbadala na sio karafuu pekee.
ReplyDelete