Na
Fatina Mathias, Dodoma.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema atawafukuza kazi madereva wa
treini watakaobainika kuiba mafuta au kutumia vibaya mali ya shirika la Reli
Tanzania.
Alitoa
onyo hilo alipokuwa akizungumza na madereva wa shirika hilo katika semina
iliyowakutanisha madereva wote kwa lengo ya kupeana mikakati ya kuliendesha
shirika hilo kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwajengea uelewa na uaminifu
madereva hao.
Alisema
ni ukweli kwamba madereva wengi wanatuhumiwa kwa wizi wa mafuta pamoja na
kutumia vibaya mali ya shirika hilo jambo ambalo linasababisha kuwepo uharibifu
mkubwa wa mali ya serikali.
Alisema
hakuna dereva atakaeonewa aibu atakapobainika anahusika na wizi au uharibifu wa
mali ya shirika.
Alisema
pamoja na serikali kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika shirika hilo, bado kuna
watumishi wanaoendelea na tabia zao za wizi wa mafuta, kutokuwa waaminifu
katika kuendesha vichwa vya treini pamoja na mabehewa jambo ambalo linasababisha
hasara kubwa.
Alisema
pamoja na kuwepo wizi wa mafuta bado serikali imeweka utaratibu wa kuboresha
maisha ya
madereva
wa treni ambao watafikisha mizigo yao vizuri katika vituo vyao.
Hata
hivyo, madereva hao wamelilalamikia shirika hilo kwa madai kuwa wafanyakazi
wana masilahi duni kuliko hata madereva wa daladala.
Mmoja
wa madereva hao, Adrof Mwabugale, alisema maisha ya madereva wa treni yamekuwa magumu
zaidi kutokana na shirika kutowathamini.
No comments:
Post a Comment